Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali nyingi zinazotokana na vitendo vya baadhi ya Askari Polisi maarufu kama PT kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa kwenye mwendo huku wakiwa wamebeba abiria. Hali hiyo hupelekea waendesha bodaboda na abiria kupata ajali mara kwa mara:- Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kuwa ajali za kizembe zinazosababishwa na baadhi ya Askari Polisi zinakomeshwa?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa hawa baadhi ya maaskari wetu ambao wamekuwa wakiwakamata hawa bodaboda wakiwa kwenye mwendo na kuwasababishia ajali ambapo wengine wamepata ulemavu mkubwa na hata kusababisha kifo. Sijui Serikali pale inapokuwa imethibitisha kwamba uzembe ulikuwa ni wa askari na yakatokea madhara kwa muendesha bodaboda, sijui huwa wanakuwa na mpango gani wa kuwapa fidia hawa waendesha bodaboda? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili, kuna malalamiko mengi ya waendesha bodaboda kwamba mara nyingi wanapokuwa wamekamatwa huwa wanabadilishiwa mashtaka wanapofika kituoni. Sasa kwa kuwa hatuna CCTV camera za kuangalia hasa yule wa bodaboda alikamatwa kwa kosa gani, je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba kosa lile alilokamatiwa yule mhusika ndilo analoshtakiwa nalo? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuleta swali hili kwa sababu ni kweli ni jambo ambalo linajitokeza katika baadhi ya maeneo na linaleta malalamiko.
Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba maisha ya vijana wetu yakipotea hayana fidia ya kusema umeweza kufidia maisha. Kwa hiyo, jambo ambalo tunafanya kama Wizara kwa kweli sisi kiutawala tunaelekeza utaratibu wa kiustaarabu wa ukamataji wa vijana hawa ili isisababishe ajali ambazo zinapoteza maisha kwa vijana wetu. Pia, tumeendelea kuwaelezea vijana wetu kwa sababu wamekuwa na uongozi kwenye vituo vyao kuhakikisha kwamba nao wanatoa ushirikiano, kwa wale ambao wamefanya makosa ni haki yao kufika kwenye adhabu ili kuweza kupunguza makosa hayo yanayojitokeza.
Mheshimiwa Spika, kuhusu yale ya kubambika kesi hilo ni kosa la kimaadili na sisi kama Wizara wale wote wanaofanya haya kwa wananchi wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa utaratibu wa ufanyaji kazi wa Jeshi la Polisi.

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali nyingi zinazotokana na vitendo vya baadhi ya Askari Polisi maarufu kama PT kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa kwenye mwendo huku wakiwa wamebeba abiria. Hali hiyo hupelekea waendesha bodaboda na abiria kupata ajali mara kwa mara:- Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kuwa ajali za kizembe zinazosababishwa na baadhi ya Askari Polisi zinakomeshwa?

Supplementary Question 2

MHE. ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali moja kuhusiana na bodaboda hapa nchini.
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na mapendekezo ya kuleta mabadiliko ya baadhi ya sheria za usalama barabarani, ikiwepo bodaboda. Kwa sababu, takwimu zinaonesha kwamba vifo vinavyosababishwa na ajali barabarani bodaboda zinaongoza. Chama cha Wabunge kimetoa mapendekezo ya kuleta hapa Bungeni mabadiliko ya sheria hiyo. Ni lini Wizara au Serikali italeta mabadiliko hayo ili yaweze kufanyiwa kazi ili kupunguza hizi ajali za barabarani, hususan, bodaboda?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Adadi Rajab kwa swali zuri la nyongeza na yeye ni dictionary yetu kwenye Wizara kwa sababu ana kumbukumbu nzuri ya masuala ya Wizara hii.
Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba jambo hilo analolisemea limeshapita ngazi ya Wizara na liko ngazi ya vikao vya Makatibu Wakuu na baada ya hapo litapitia Baraza na tutaleta Bungeni kwa ajili ya ukamilishwaji wa hatua hiyo anayoiomba Mheshimiwa Mbunge.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali nyingi zinazotokana na vitendo vya baadhi ya Askari Polisi maarufu kama PT kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa kwenye mwendo huku wakiwa wamebeba abiria. Hali hiyo hupelekea waendesha bodaboda na abiria kupata ajali mara kwa mara:- Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kuwa ajali za kizembe zinazosababishwa na baadhi ya Askari Polisi zinakomeshwa?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri wakati akijibu hoja zangu za kuhusu fine kwa madereva wa bodaboda alikiri kweli haiwezekani bodaboda anabeba abiria mmoja, anatozwa fine Sh.30,000 wakati basi linalobeba abiria 60 fine ni ile ile Sh.30,000. Tunaomba atuhakikishie katika hayo mabadiliko ya sheria, je, hii sheria ya fine kwa ajili ya madereva bodaboda itakuwepo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimempata vizuri mwakilishi na msemaji/mtetezi wa vijana, Mheshimiwa Mlinga. Niseme tu suala la fine sheria yake inapitishwa na Bunge kupitia Finance Bill ambayo itakuja kwenye mapendekezo ya Wizara ya Fedha. Sisi kama Wizara tumependekeza hivyo hivyo kwamba kwa kweli, ni vyema fine ya bodaboda itofautishwe na fine ya mabasi na coaster kwa sababu fine ya bodaboda kuwa sawasawa na ya magari makubwa yanayobeba abiria wengi ndiyo inayosababisha bodaboda nyingi zinarundikana kwenye vituo vya polisi kwa kushindwa kulipia fine zile. Kwa hiyo, tuliona ni vyema ikawa fine inayoweza kulipika ili kuweza kuwa na mantiki ile ya kutoa onyo badala ya kuwa chanzo cha fedha.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali nyingi zinazotokana na vitendo vya baadhi ya Askari Polisi maarufu kama PT kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa kwenye mwendo huku wakiwa wamebeba abiria. Hali hiyo hupelekea waendesha bodaboda na abiria kupata ajali mara kwa mara:- Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kuwa ajali za kizembe zinazosababishwa na baadhi ya Askari Polisi zinakomeshwa?

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Ni kweli kwamba kuna tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii hasa kwa vijana na vijana wengi wamejiajiri kupitia njia ya bodaboda na nyingi wamekopeshwa kwa mikataba mbalimbali na watu wenye fedha zao. Ukizunguka katika vituo vya polisi nchi hii, hata hapa Dodoma, bodaboda zimejaa kila mahali.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anakiri kwamba fine ni kubwa kweli kweli, kwa hiyo, kuna kesi nyingi za vijana hawa na wenye bodaboda zao wanawadai fedha. Ni nini kauli ya Serikali na hasa Mheshimiwa Waziri, kuondoa bodaboda katika vituo vya polisi, kwa maana ya kupunguza gharama, ili vijana hawa waendelee kujiajiri na wapunguze kesi ambazo wameshtakiwa na watu wenye bodaboda zao ambao wamefunga nao mikataba? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, sikumpata vizuri babu yangu, Mheshimiwa Mwita, Wanyiramba tulishaondoka siku nyingi Mara, kwa hiyo, lafudhi kidogo imenishinda.
Mheshimiwa Spika, lakini ambacho tunafanya, moja, tunatoa elimu kuweza kuhakikisha kwamba wanafuata taratibu, kwa sababu kwa kweli maisha ya vijana wetu wengi sana yanakatika kutokana na wao kutokuzingatia taratibu za kujifunza maana bodaboda ni vyombo vya moto kama vyombo vingine na vimekuwa vikisababisha sana ajali. Kwa hiyo, tumeweka mkazo sana kwenye kutoa elimu lakini hata wao tumewaelekeza sana kuhakikisha kwamba nao wanaliongelea jambo hili kama moja ya jambo la hatari ambalo linasababisha madhara haya.
Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu kupunguza mishtuko hiyo pamoja na bodaboda nyingi kwenye vituo vya polisi, hilo tumeelekeza moja kwenye hili la upande wa fine, lakini la pili tumeelekeza hata kiutawala tu kwamba, kuwe na utaratibu wa kuwaandikisha na kuwaruhusu wawe na hivyo vifaa vyao ili waweze kulipa baada ya muda ambao wataweza kupewa. Nchi nyingine ambazo zimeendelea taratibu zote za mambo ya fine za usalama barabarani wanafanya kuandikisha na kumpa muda mtu aliyekutwa na kosa wa kufanya malipo hayo punde atakapokuwa ameshaanza kufanya kazi na hicho chombo chake.
Mheshimiwa Spika, utaratibu ambao umekuwa unatumika muda huu ni wa kushikilia bodaboda hiyo na kusema mpaka atakapokuwa amelipa ndipo atakapewa. Tumeelekeza tu zile bodaboda ambazo zinatakiwa kutumika kama sehemu ya ushahidi, kwa mfano, kwenye makosa makubwa kama ya madawa ya kulevya, mambo ya uhalifu wa kutumia silaha, hivyo ndivyo ambavyo tunaweza tukashikilia kwa sababu makosa yake kwa kweli haturuhusu yaendelee kufanyika kwa kutumia bodaboda hizo.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali nyingi zinazotokana na vitendo vya baadhi ya Askari Polisi maarufu kama PT kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa kwenye mwendo huku wakiwa wamebeba abiria. Hali hiyo hupelekea waendesha bodaboda na abiria kupata ajali mara kwa mara:- Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kuwa ajali za kizembe zinazosababishwa na baadhi ya Askari Polisi zinakomeshwa?

Supplementary Question 5

MHE. MARTH M. MLATA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa hivi karibuni Serikali imewaondoa madereva wengi ambao ni wazoefu kwa sababu wao ni darasa la saba na kuwaajiri vijana wadogo kwa sababu wao wana-qualify ama kidato cha nne na kuendelea, lakini bila uzoefu na tumeshuhudia sasa ajali zimeanza kuwamaliza viongozi wetu. Serikali haioni sasa hilo ni bomu kubwa sana inatengeneza kwa ajira za vijana ambao hawana uzoefu kwa kuwamaliza watu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana dada yangu Mheshimiwa Martha Mlata kwa swali nzuri na swali lenye mantiki. Nachoweza kusema tu ni kwamba Idara yetu ya Usalama Barabarani itaendelea kufuatilia masuala ya uzoefu kuhusu uendeshaji wa vyombo hivi vya moto. Hata kwenye swali la msingi tulipotoka kwenye upande wa bodaboda ndivyo vitu ambavyo tumeendelea kuwasisitizia kwamba mtu anajifunza ndani ya robo saa na baada ya hapo anabeba watu watatu kwenye pikipiki yake. Kwa maana hiyo hata upande wa magari tutaendelea kuongea na wenzetu kwa upande wa magari haya ya Serikali ambayo ameyaongelea, waweze kuzingatia suala la uzoefu wa anayeendesha gari hiyo pamoja na mwendo ambao anatakiwa kuendesha gari hiyo.