Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya halmashauri bado zinalalamikiwa kwamba utekelezaji huu ni mdogo au wakati mwingine haufanyiki kabisa. Je, malalamiko haya yanapotokea katika baadhi ya halmashauri, hawa vijana, walemavu na akina mama, ni wapi wanapaswa waende kulalamika ili kuhakikisha utaratibu huu unafanyika? Ahsante sana.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kama alivyosema hapo awali, ni kweli kwamba hatua ya kwanza kabisa ya kusemewa ni kwa Mheshimiwa Diwani, lakini vilevile kupitia Baraza la Madiwani ambacho ndicho kikao cha kwanza kabisa kuhoji kuhusu mgawanyo wa fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake.
Mheshimiwa Spika, lakini katika ukaguzi ambao wamekuwa wakiufanya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali amekuwa akionesha kwamba halmashauri ambazo hazitengi fedha kikamilifu kama ambavyo mapato ya ndani yanaonesha zimekuwa zinaandikiwa madeni. Kwa hiyo, uwajibikaji unaanzia hapo na hatua hizi tutaendelea kuzifuatilia. Kama nilivyosema katika jibu la msingi kwamba tunatarajia kuweka kipengele kwenye sheria ambacho kitalazimisha sasa kila halmashauri itenge asilimia 10 ya mapato yake ya ndani na itoe fedha hizo kwa ajili ya vikundi vya vijana na wanawake. (Makofi)

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati huu ni Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi, ni sera, sheria na kule kwenye halmashauri zetu lisipotekelezwa ni hoja ya ukaguzi lakini bado kuna changamoto za utekelezaji. Je, ni lini sasa Serikali itatoa waraka mkali kabisa ambao utaelekeza halmashauri zote zitekeleze na zisipotekeleza ziweze kuwajibishwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la rafiki yangu Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, jambo hili tumelitolea maelezo hapa mara kadhaa na hata tukifanya rejea wakati nawasilisha bajeti yetu ya mwaka wa fedha 2018/2019 tulisema wazi kwamba katika ajenda hii ya mikopo ya akina mama na vijana sasa suala hili linakuwa si la hiari tena. Nimesema wazi mara kadhaa kwamba jamani fedha hizi hazifiki Hazina zinaishia katika halmashauri zetu. Jukumu letu kubwa sisi kuhakikisha tunasimamia katika Kamati za Fedha ili fedha hizi ziweze kufika kwa vijana na akina mama, hilo ndilo jambo la msingi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ndiyo maana katika Finance Bill ya mwaka huu tumeleta kifungu maalum kwa ajili ya enforcement ya jambo hilo. Ni imani yangu kwamba baada ya Sheria hiyo ya Fedha kufika hapa, Wakurugenzi wote, lakini niwatake Madiwani wote na Wabunge wote katika halmashauri zetu tuweze kuwa imara kuhakikisha utaratibu wa fedha hizi ambazo zinatengwa na katika bajeti ni lazima zitengwe, ziweze kuwafikia vijana na akina mama wetu. Kwa hiyo, hili ni jambo letu sisi sote na si jambo la mtu mmoja na kwa vile sheria inakuja nadhani hapa itakuwa hakuna suala la negotiation, tutakwenda kwa mujibu wa sheria itakavyotuongoza. (Makofi)

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama?

Supplementary Question 3

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Manispaa ya Iringa ni moja ya Manispaa ambazo zinatekeleza kwa ukamilifu na kwa uaminifu suala hili la asilimia 10 kwa vijana na akina mama. Na kwa kuwa Serikali imekuwa ikichelewa wakati fulani kuleta pesa zinazotoka Serikali Kuu kwa ajili ya maendeleo, Wizara haioni ni muhimu sasa kuziona halmashauri kama Manispaa ya Iringa ambazo zinafanya vizuri ili ziwape kipaumbele kupeleka hela za kimaendeleo kwa sababu zinatekeleza wajibu wake?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la rafiki yangu, Mheshimiwa Mchungaji Msigwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, naomba nikiri wazi kuna manispaa nyingi sana zafanya vizuri hapa nchini kwetu katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Miongoni mwa manispaa inayofanya vizuri vilevile ni Manispaa ya Kinondoni ukiachana na Iringa na juzi juzi waliweza kutoa fedha zaidi ya shilingi bilioni 2 kwa ajili ya mikopo ya akina mama na vijana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini katika suala zima la upelekaji wa fedha za maendeleo tumejipanga na ndiyo maana hapa katikati unaona jinsi tunavyojitahidi kwa kadri iwezekanavyo na tuna matarajio kwamba kabla mwaka huu wa fedha haujafika, si Halmashauri ya Iringa peke yake isipokuwa manispaa zote na halmashauri zote kuhakikisha zinapata fedha na especially kwa ajili ya kwenda kukamilisha yale majengo yetu ya hospitali na madarasa. Tunawasiliana na wenzetu wa Hazina ikibidi tutatumia force account kuhakikisha kiwango kikubwa cha fedha kinapatikana katika halmashauri zetu ili miradi hii ya maendeleo iweze kutekelezeka katika eneo yetu.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hii asilimia 10 ya vijana na akina mama hii ni revolving fund, mtu anakopa, anarejesha. Nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri, hawa tunaowakopesha, je, wanarejesha na kama hawarejeshi, wanachukuliwa hatua gani? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lubeleje, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba fedha hizi wanapokopeshwa vikundi vya vijana na wanawake wanatakiwa kurejesha na mratibu mkuu wa marejesho ni Afisa Maendeleo ya Jamii katika halmashauri husika. Kwa hiyo, kama kuna sehemu hawarejeshi kabisa, huo utakuwa ni udhaifu mkubwa sana wa kikazi wa huyo Afisa Maendeleo ya Jamii pamoja na Kamati yake ya Mikopo ya Halmashauri. Wito ambao tunautoa ni kwamba ni lazima wanaokopeshwa warejeshe, vinginevyo hatua zitachukuliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo zuri kabisa ambalo amelifanya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI wakati anawasilisha hotuba ya bajeti ni kutoa tangazo kwamba kuanzia mwakani atafuta au amefuta riba kwenye mikopo ya wanawake na vijana. Kwa hiyo, hiyo iwe kichocheo cha mwananchi yeyote atakayekopeshwa mikopo hiyo arudishe fedha kama alizokopa bila riba. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama?

Supplementary Question 5

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kumekuwa na Mifuko mingi ya Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi, mingine iko Ofisi ya Waziri Mkuu na mingine iko TAMISEMI; na kwa kuwa sheria/ takwa hili la kutaka kutengwe asilimia 10 kwenye Serikali za Mitaa, muda mwingi katika ripoti za CAG imeonekana ufanisi ni hafifu, kama kweli mna lengo la kuwawezesha wananchi kiuchumi, kwa nini msifikirie kuunganisha mifuko hii uwe mfuko mmoja ili kuwepo na ufanisi?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika, naomba nitoe majibu ya nyongeza kwenye swali la msingi sana aliloliuliza Mheshimiwa Paresso.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa ndani ya Serikali tumeanza kutafakari na kuona ni kwa kiasi gani tunaweza kuitazama kwa kina mifuko hii yote takriban kama 16 ama 19 hivi tuliyonayo, tukaiunganisha na kuipunguza ikajenga nguvu kubwa zaidi na ikawa na impact kubwa zaidi kwa Watanzania wengi na hasa wale ambao wako vijijini. Kwa hiyo, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kazi hii imeshaanza na Ofisi ya Waziri Mkuu inaishughulikia vizuri na baada ya muda mfupi nadhani tunaweza tukaja na sheria ya kuunganisha baadhi ya mifuko na kuibakiza michache ambayo itakuwa na impact kubwa kwa maendeleo ya Watanzania. (Makofi)