Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 307 2018-05-24

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:-
Je, ni kwa kiasi gani Serikali inasimamia suala la asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha halmashauri zote nchini zinatenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Katika Mwaka wa Fedha 2016/2017, jumla ya shilingi bilioni 56.8 zilitengwa na halmashauri zote nchini na jumla ya shilingi bilioni 17.5 sawa na asilimia 31 zilitolewa kwa vikundi vya wanawake na vijana. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi bilioni 61.6 zilitengwa na hadi kufikia Februari, 2018 jumla ya shilingi bilioni 15.6 sawa na asilimia 27 zilikuwa zimetolewa, ambapo jumla ya vikundi 8,672 vya wanawake na vijana vilipatiwa mikopo. Katika mwaka wa fedha 2018/ 2019, shilingi bilioni 53.8 zimetengwa kwa ajili ya Mfuko wa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu katika halmashauri zote nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuongeza uwajibikaji katika kutenga na kupeleka fedha za Mfuko wa Wanawake na Vijana kwa vikundi husika, Serikali itaweka utaratibu katika Sheria ya Fedha (Finance Bill) ya mwaka 2018/2019 utakaohakikisha kwamba halmashauri zote zinatekeleza kikamilifu agizo hilo. (Makofi)