Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:- Je, ni nini faida ya hati miliki za kimila?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ukiangalia majibu ya Mheshimiwa Waziri amesema kwamba waliokopeshwa kwa kutumia hatimiliki za kimila takribani ni shilingi bilioni 59, lakini ukiangalia idadi ya wanaomiliki hati hizo miliki za kijiji wako wengi, sasa hii inaonesha kwamba kuna tatizo katika wakopeshaji.
Sasa je, Waziri atakubali kulifuatilia jambo hili ili kuhakikisha kwamba wale wanyonge ambao hasa ndiyo wanalengwa kwa sasa wanapata mikopo bila usumbufu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Sheria Namba Nne na Namba Tano ya mwaka 1999 ya Ardhi ya Vijiji iko wazi na inatakiwa marekebisho kwa sababu wanaokwenda kutoa haki inapotokea matatizo ya ardhi vijijini ni mabaraza ya kata. Lakini kwa kuwa kuna tatizo pale.
Je, Waziri atakuwa tayari kukutana na Waziri wa TAMISEMI na yeye Waziri wa Ardhi ili kurekebisha kwa sababu haki haitendeki kama ambavyo inatakikana?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anasema imeonekana ni wazi kwamba wahitaji wa mikopo ni wengi, lakini wanaokopeshwa ni wachache. Hapa kuna mambo mawili kuna either watu kuogopa kwenda kuchukua mikopo au benki kutokubali zile hatimiliki za kimila.
Napenda nimthibitishie tu kwa sababu elimu inayotolewa wanapopewa zile hati za haki miliki za kimila wanaambiwa zina sifa sawa sawa na hati zingine na ndiyo maana benki 11 zimeweza kutoa hizo shilingi bilioni tisa na ninawapongeza sana watu wa Mbozi ambao ndiyo wanaongoza kwa kutoa mikopo kwa kutumia hati miliki za kimila. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili ambalo amelizungumzia naomba tu niseme kwamba kweli tunayo changamoto hiyo na hasa ya uelewa, kwa maana katika maeneo mengi tunahitaji kuwa na watu ambao ni waajiriwa wanaoweza kufanya kazi hiyo ya kusimamia Mabaraza ya Ardhi. Sasa kama hilo linaonekana ni tatizo nadhani bado tunaweza tukaliangalia. Ni kweli kuna shida na maeneo mengi Mabaraza ya Ardhi ya Kata hayafanyi kazi yake vizuri pengine kutokana uelewa mdogo au kutokuwa na manpower ya kutosha, kwa hiyo, hili tunalichukua tutalifanyia kazi.