Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 23 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 196 2018-05-07

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:-
Je, ni nini faida ya hati miliki za kimila?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venance Mwamoto kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa fungu la 18, 28 hadi 47 la Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba tano ya mwaka 1999 hati ya hakimiliki za hati ya kumiliki ardhi kwa kuzingatia mila na desturi kwa raia wa Tanzania na ina hadhi sawa na hakimiliki nyingine inayotolewa kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna faida nyingi za hati za hakimiliki ya kimila, miongoni mwa faida hizo ni pamoja na kuwa na usalama wa miliki, kupunguza migogoro baina ya watumiaji ardhi, kutumika kama dhamana katika taasisi za fedha na vyombo vya kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia Machi, 2018 jumla ya hatimiliki za kimila 56,506 zimeandaliwa katika maeneo mbalimbali nchini. Wananchi katika maeneo hayo wamenufaika kiuchumi kutokana na mikopo waliyoipata katika taasisi za kifedha kwa kutumia hati za hatimiliki za kimila kama dhamana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia Juni, 2017 kiasi cha shilingi bilioni 59.2 zimekopeshwa kwa wananchi kwa kutumia hati za hakimiliki za kimila kama dhamana kutoka mabenki na taasisi za kifedha. Miongoni mwa taasisi hizo ni pamoja NMB PLC, CRDB PLC, Stanbic Bank, SIDO, PSPF, Agriculture Trust Fund, Meru Community na Mfuko wa Pembejeo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa wananchi wote kutoa ushirikiano katika miradi ya utoaji hati za hakimiliki za kimila inayoendelezwa katika maeneo yao ili ziweze kuwanufaisha kwa ustawi wa kiuchumi na kijamii.