Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Mahakama ya Mkoa licha ya Mkoa huo kuanzishwa zaidi ya miaka mitano iliyopita. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya ngazi ya Mkoa?

Supplementary Question 1

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Serikali kuwa mepesi kabisa, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Machi, 2012 Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda aliutangaza Mkoa wa Simiyu kuwa mkoa mpya, lakini mpaka ninavyoongea hivi ni takriban miaka sita mkoa huu hauna Mahakama ya Mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jengo linalotumika kuendeshea Mahakama ya Mkoa na Wilaya ya Bariadi ni jengo ambalo ni la Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ambaye ndio ameipangisha Mahakama.
MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, kwa kitendo cha kumpangisha Mwenyekiti wa Halmashauri ni jambo ambalo linaleta mkanganyiko na hofu kwa wananchi kwamba kwa kuchelewesha kujenga jengo la Mahakama ya Mkoa ni moja ya maslahi kati ya Mwenyekiti wa Halmashauri na Serikali. (Makofi)
Je, ni lini Serikali italeta mkakati wa haraka ili kuweza kujenga Mahakama hiyo ya Mkoa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mkoa wa Simiyu tuna changamoto ya Mahakimu. Mkoa wa Simiyu una Hakimu mmoja ambaye anahudumia Wilaya sita, lakini pia Hakimu wa Mahakama ya Wilaya anahudumia Wilaya nne; Wilaya ya Busega, Wilaya ya Itilima, Wilaya ya…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nini mkakati wa Serikali wa kuharakisha kujenga Mahakama hizi katika Mkoa wa Simiyu? (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, tayari ujenzi wa Mahakama ya Mkoa katika Mkoa wa Simiyu imeshaanza kujengwa, msingi umeshakamilika na hatua nyingine za ujenzi zinafuata. Kwa sababu tunatumia ujenzi wa aina ya moladi tuna hakika kabisa jengo hilo litakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Mahakama ya Mkoa, pia Mkoa wa Simiyu utajengewa Mahakama Kuu katika mpango huu unaoendelea. Kuhusu idadi ya Mahakimu, ni kweli kumekuwa na upungufu wa Mahakimu siyo tu kwa Mkoa wa Simiyu, bali nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mahakama iko katika utaratibu wa kuajiri Mahakimu zaidi baada ya kuwa imepata ikama kupitia Tume ya Ajira ya Mahakama na hao wakipatikana, miongoni mwa mikoa ambayo itakumbukwa na kupangiwa Mahakimu ni Simiyu.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Mahakama ya Mkoa licha ya Mkoa huo kuanzishwa zaidi ya miaka mitano iliyopita. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya ngazi ya Mkoa?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona niulize swali dogo la nyongeza. Swali lililoulizwa namba 167 linafanana kabisa na Wilaya ya Ngara. Wilaya ya Ngara haina jengo la Mahakama, inatumia jengo la DC.
Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Ngara? (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Ngara imepangiwa kujengewa Mahakama ya Wilaya katika mwaka wa 2019/2020 na pia Mahakama ya Mwanzo Lulenge mwaka 2019/2020. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Mahakama ya Mkoa licha ya Mkoa huo kuanzishwa zaidi ya miaka mitano iliyopita. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya ngazi ya Mkoa?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mahakama ya Mwanzo ya Bukindo, Bukonyo na Ukara zina hali mbaya sana kimiundombinu, achilia mbali upungufu wa watumishi. Nataka kujua Serikali ina mkakati gani wa kuboresha mazingira haya ili haki ya wananchi wa Visiwa vya Ukerewe iweze kupatikana kwa haraka?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Wilaya ya Ukerewe, imepangiwa kujengewa Mahakama ya Mwanzo katika eneo la Ilangala katika mwaka wa fedha unaoanza sasa wa 2018/2019.