Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 20 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 167 2018-05-02

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:-
Mkoa wa Simiyu hauna Mahakama ya Mkoa licha ya Mkoa huo kuanzishwa zaidi ya miaka mitano iliyopita. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya ngazi ya Mkoa?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gimbi Dotto Masaba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi katika mikoa yote Tanzania Bara. Mkoa wa Simiyu kama ilivyo mikoa mingine unayo Mahakama ya Hakimu Mkazi ambayo kwa sasa inatumia jengo la kupangisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nia ya Serikali ni kuwa na jengo la Mahakama kwa kila ngazi kwa kadiri itakavyowezekana. Tayari tunao mpango wa kujenga majengo katika kila ngazi ya Mahakama kwa awamu katika mwaka wa fedha 2017/2018. Simiyu ni moja ya mikoa mitano ambayo ujenzi wake wa Mahakama umeanza ambapo kwa sasa msingi umekamilika na hatua nyingine za ujenzi zinaendelea.