Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Katika nchi yetu suala la usawa na haki kwa wananchi wetu ni jambo linalozingatiwa sana na utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano; taarifa ya hali ya umaskini nchini imebainisha kwamba ipo mikoa minne ambayo kiwango cha umaskini kipo juu sana na mojawapo ya mikoa hiyo ni Kigoma. Je, ni hatua zipi za makusudi (kibajeti) zinazochukuliwa ili Mkoa wa Kigoma ujinasue na hali ya umaskini ambayo kwa kiasi cha asilimia 80 umesababishwa na madhila ya kihistoria (historical injustices) na Serikali kuacha au kushindwa kujenga miundombinu ya maendeleo kama barabara, vituo vya afya na kadhalika?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa maelezo ya Mheshimiwa Waziri ingawa maelezo yenyewe yanajikanganya sana. Msingi wa swali ni hatua za makusudi za kibajeti, kwa sababu Mkoa wa Kigoma kama ilivyo mikoa mingine unapata bajeti kwa mujibu wa ceiling. Sasa nina maswali mawili madogo tu ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizo barabara anazozizungumza, zimesimama kujengwa. Zimeanza kujengwa tangu mwaka 2006. Barabara hizo hazijengwi tena na Wizara ya Fedha nyie ndiyo mnatoa fedha. Ni lini sasa kwa makusudi mtatoa fedha ili barabara hizi ziweze kukamilika baada ya kukaa kwa miaka 12 hazijakamilika? Hilo swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni dhahiri kabisa kukamilika kwa majengo ya NSSF na National Housing hakuwezi kuondoa umaskini wa watu wa Kigoma. Hoja ya msingi ni kwamba tunataka kuwe na special strategy ya mikoa hii minne ambayo iko nyuma, ndiyo hoja ya msingi iko hapo. Majengo haya yapo tu! Kwa hiyo, msingi wa hoja yangu ni kwamba Mheshimiwa Waziri atueleze ni mkakati upi wa kuiondoa mikoa hii minne katika lindi la umasikini kuweka katika mikoa ambayo ni bora zaidi kama ilivyo mikoa mingine? Hiyo ndiyo hoja ya msingi. (Makofi)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimeonesha dhahiri miradi inayotekelezwa ili kuweza kuwaondoa wananchi wa Kigoma kutoka kwenye lindi la umaskini. Huwezi kuwaondoa wananchi katika lindi la umaskini bila kuwa na miundombinu ambayo nimeionesha. Ndiyo msingi wa jibu langu la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara zilizosimama, Wizara tupo katika majadiliano, tulimaliza uhakiki na sasa tunaelekea kulipa na barabara hizi zitaendelea kujengwa kama ilivyopangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anauliza kuhusu special strategy, napenda kuliambia Bunge lako tukufu kwamba special strategy ipo na tumeanza kuitekeleza kwa mikoa yote. Kwa Mkoa wa Kigoma aliouliza, mfano wa special strategy ni upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma ambapo ndege kubwa zilikuwa hazitui na sasa ndege kubwa zinatua, watalii wanafika kwa wakati, wawekezaji wanafika kwa wakati, wafanyabiashara wanafika kwa wakati na tunafungua uchumi wa Kigoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekamilisha kwa asilimia 100 ujenzi wa magati mawili; Gati la Kagunga limekamilika kwa asilimia 100, Gati la Kibwesa limekamilika kwa asilimia 80. Hii ni kuufanya Mkoa wa Kigoma uwe ni hub ya biashara kwa landlocked countries zinazotutegemea sisi Tanzania ili tuweze kufungua uchumi wa watu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie Mheshimiwa Mbunge pamoja na ndugu zangu wote wa Kigoma, Serikali yao ipo makini. Tunaelewa kulikuwa na shida ya bottleneck inflation na sasa tunafungua kwa kukamilisha miradi hii, ndio maana reli yetu ya kuwa kiwango cha kisasa tunakwenda kuikamilisha kufungua mikoa yetu hii. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Katika nchi yetu suala la usawa na haki kwa wananchi wetu ni jambo linalozingatiwa sana na utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano; taarifa ya hali ya umaskini nchini imebainisha kwamba ipo mikoa minne ambayo kiwango cha umaskini kipo juu sana na mojawapo ya mikoa hiyo ni Kigoma. Je, ni hatua zipi za makusudi (kibajeti) zinazochukuliwa ili Mkoa wa Kigoma ujinasue na hali ya umaskini ambayo kwa kiasi cha asilimia 80 umesababishwa na madhila ya kihistoria (historical injustices) na Serikali kuacha au kushindwa kujenga miundombinu ya maendeleo kama barabara, vituo vya afya na kadhalika?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi na mikoa mingine ambayo imekuwa inapokea wakimbizi ni mikoa ambayo iliathirika sana kiuchumi kwa sababu nguvu yao kubwa sana ilipelekea kubeba mzigo wa wakimbizi kutoka nchi jirani na kupelekea kuwa na umasikini kwenye maeneo hayo.
Je, Serikali imejipanga vipi kusaidia maeneo ambayo yalitoa nguvu zao kubwa sana kusaidia ndugu zetu wa nchi za jirani na hali ya maisha sasa ya wananchi ambao walifanya kazi ya kuwapokea ndugu zetu wamekuwa na mazingira ya maisha duni?
Tunaomba Serikali itupe majibu, inatusaidia vipi katika mikoa hiyo?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwa Mkoa wa Kigoma na Mkoa wa Katavi nao ni hivyo hivyo. Tumeweka vipaumbele hasa kuhakikisha tunafungua mikoa hii kwa miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini Mheshimiwa Mbunge ni shahidi kwamba miundombinu inafunguka ili wakulima wetu waweze kusafirisha mazao yao kwa haraka na nguvu zote kama Serikali tunaelekeza kwenye mikoa hii iliyoonyeshwa kwenye utafiti ule kwamba ni ya mwisho katika hali ya umasikini ndani ya Taifa letu.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Katika nchi yetu suala la usawa na haki kwa wananchi wetu ni jambo linalozingatiwa sana na utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano; taarifa ya hali ya umaskini nchini imebainisha kwamba ipo mikoa minne ambayo kiwango cha umaskini kipo juu sana na mojawapo ya mikoa hiyo ni Kigoma. Je, ni hatua zipi za makusudi (kibajeti) zinazochukuliwa ili Mkoa wa Kigoma ujinasue na hali ya umaskini ambayo kwa kiasi cha asilimia 80 umesababishwa na madhila ya kihistoria (historical injustices) na Serikali kuacha au kushindwa kujenga miundombinu ya maendeleo kama barabara, vituo vya afya na kadhalika?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Ripoti mbalimbali ikiwemo Ripoti ya MVS na REPOA inaoneesha kwamba hali ya njaa na umasikini nchini imeongezeka kwa mwaka 2018 ukilinganisha na miaka iliyopita. Je, Serikali ina kauli gani juu ya hili? Ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napata taabu sana kusema kwamba hali ya njaa imeongezeka ndani ya mwaka 2018. Katika bidhaa zinazochangia mfumuko wa bei au inflation rate kuongezeka ni upatikanaji wa chakula. Inflation kwa mwezi wa Tatu ilikuwa asilimia 3.9. Hii ni indicator kwamba hali ya njaa kwa Tanzania haipo na mvua zimenyesha za kutosha, wananchi wetu wako katika amani kabisa ya upatikanaji wa chakula ndani ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namwomba tu Mheshimiwa Mbunge, yawezekana taarifa anazozisoma ni za mwaka 2016/2017 kulikokuwa na shida hiyo, siyo kwa mwaka 2018.