Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza:- Ubora wa elimu wanayopata watoto wa jamii ya kifugaji wanaosoma shule za kutwa vijijini unaathiriwa sana na umbali mrefu wanaotembea wanafunzi kutoka makazi yao (maboma) hadi shuleni. (a) Je, ni kwa nini Serikali isijenge mabweni katika baadhi ya shule zilizo kwenye vijiji vyenye mtawanyiko mkubwa wa maboma? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wa Longido kujenga vyumba 177 vya madarasa, nyumba 291 za walimu na matundu 561 ya vyoo? (c) Je, Serikali imepanga lini kuziba upungufu wa walimu 234; Waratibu Elimu Kata 18 na maafisa ngazi ya Wilaya 12 katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri aliyonipa Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijauliza, nichukue fursa hii kuishukuru Serikali kwa sababu ya kazi kubwa na nzuri wanayoifanya kuinua hali ya elimu katika Wilaya ya Longido. Historia ya Wilaya ya Longido…
Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa. Swali ni kwamba kwa upande wa ubora wa elimu ukizingatia kwamba ubora wa elimu unategemea uboreshaji wa shule kuanzia ngazi ya chekechea; na kwa kwa sababu vitongoji vya Wilaya ya Longido viko mbali na shule za msingi zenye elimu za chekechea (shule za awali).
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mpango gani katika kuhimiza wananchi wajenge shule na Serikali ipeleke walimu waliosomea?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kwa kuwa tatizo la shule za msingi la miundombinu halina tofauti na Shule zetu za Sekondari katika Wilaya ya Longido; je, Serikali imejipangaje kutusaidia kuziba mapengo yaliyopo katika madarasa yapatayo 58, maabara 27, mabweni 73, nyumba za walimu
252, maktaba nane...
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuna uhaba wa walimu wa sayansi wapatao 27? Ahsante sana.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS - TAWALAZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Kiruswa, katika muda mfupi tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge amefanya mengi, ofisini kwangu ameshakuja zaidi ya mara tatu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi zake nazipokea kwa niaba ya Serikali, naomba sana nimhakikishie kwamba wananchi waendelee na juhudi wanazozifanya. Tunatambua juhudi zao. Pale ambapo atakamilisha darasa lolote la awali, tuwasiliane ili tuweze kupeleka walimu wa madarasa ya awali ambao wamesomeshwa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kuhusu kumalizia maboma ambayo wananchi wameanzisha na yamefika kwenye lenta, naomba nimhakikishie kwamba katika fedha za ruzuku ya maendeleo ambazo tutazipeleka kuanzia mwezi wa Saba tumewapa kipaumbele Wakurugenzi wazingatie sana kumalizia maboma ambayo yameanzishwa na wananchi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza:- Ubora wa elimu wanayopata watoto wa jamii ya kifugaji wanaosoma shule za kutwa vijijini unaathiriwa sana na umbali mrefu wanaotembea wanafunzi kutoka makazi yao (maboma) hadi shuleni. (a) Je, ni kwa nini Serikali isijenge mabweni katika baadhi ya shule zilizo kwenye vijiji vyenye mtawanyiko mkubwa wa maboma? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wa Longido kujenga vyumba 177 vya madarasa, nyumba 291 za walimu na matundu 561 ya vyoo? (c) Je, Serikali imepanga lini kuziba upungufu wa walimu 234; Waratibu Elimu Kata 18 na maafisa ngazi ya Wilaya 12 katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa ukosefu wa mabweni ni tatizo la nchi nzima na hasa katika shule za sekondari za kata, hivyo kufanya baadhi ya wanafunzi kupanga katika nyumba za watu binafsi; je, Serikali haioni umefikia wakati kuhamasisha wadau mbalimbali wa elimu kujenga hostel karibu na shule ili kuepuka kadhia hii?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalitambua sana tatizo la mabweni katika shule za sekondari za kata. Lengo la kujenga shule za sekondari za kata ilikuwa ni kuwawezesha watoto ambao wako ndani ya kata waweze kusoma, lakini tatizo ni kwamba kuna baadhi ya vijiji kweli viko mbali sana na Makao Makuu ya Kata au mbali sana na eneo ambalo ipo shule. Kwa hiyo, kuna tatizo kwamba wanafunzi wengi wamekuwa wakipanga nyumba kwa sababu hawawezi kutembea kilometa labda 15,20 kutoka nyumbani kwao kwenda katika shule kusoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo tatizo tunalielewa na ninaungana naye na tutaendelea kuhimiza wadau wajenge mabweni na hostel karibu na shule hizi ili kusudi ziweze kutoa huduma nzuri kwa watoto na hasa watoto wa kike waweze kuepuka matatizo mengine ambayo yanawapata kupanga katika nyumba za watu.

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza:- Ubora wa elimu wanayopata watoto wa jamii ya kifugaji wanaosoma shule za kutwa vijijini unaathiriwa sana na umbali mrefu wanaotembea wanafunzi kutoka makazi yao (maboma) hadi shuleni. (a) Je, ni kwa nini Serikali isijenge mabweni katika baadhi ya shule zilizo kwenye vijiji vyenye mtawanyiko mkubwa wa maboma? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wa Longido kujenga vyumba 177 vya madarasa, nyumba 291 za walimu na matundu 561 ya vyoo? (c) Je, Serikali imepanga lini kuziba upungufu wa walimu 234; Waratibu Elimu Kata 18 na maafisa ngazi ya Wilaya 12 katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido?

Supplementary Question 3

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa kuuliza swali la nyongeza. Matatizo yaliyopo katika Jimbo la Longido ni sawa kabisa na matatizo ambayo yapo katika Jimbo la Ludewa. Jimbo la Ludewa kwa sasa lina upungufu wa walimu 500 wa shule za msingi. Je, Serikali ina mpango gani kutuletea walimu wa shule ya msingi katika Jimbo la Ludewa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Deo Ngalawa kwa kunirejesha vizuri katika kumbukumbu zangu kwamba tunaendelea na mchakato chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi Baraza la Mitihani linaendelea kuchakata na kuvikagua vyeti vya walimu 1,0140 ambao tunategemea waajiriwe kwa ajili ya shule za msingi ifikapo tarehe 30 Juni, 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Ngalawa tuendelee kuwasiliana ili tutakapofika wakati wa kuwapangia maeneo ya kwenda, basi tuwe na mawasiliano ya karibu. Ahsante.