Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Goodluck Asaph Mlinga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ulanga
Primary Question
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Wilaya ya Ulanga ina ongezeko la mifugo; ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe lakini hakuna huduma za mifugo kama vile majosho:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majosho?
Supplementary Question 1
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri machachari na kijana, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mifugo kuongezeka kwa wingi Ulanga limeanza tangu miaka ya 90 na tumepiga kelele lakini Serikali kwenye ujenzi wa majosho wako nyuma lakini kwenye kupiga chapa kwa sababu inawaingizia mapato wamekuwa wako mbele. Naomba commitment ya Serikali iseme kuwa mwaka huu 2018/2019 tutajenga majosho. Hilo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kwa kuwa kumekuwa na tatizo la masoko ya mifugo, masoko yaliyoko ni minada ya kienyeji ambapo wafugaji wanauza mifugo kwa bei nafuu. Je, lini Serikali itaweka utaratibu maalum wa masoko ili wafugaji wauze mifugo yao kwa bei ya faida? (Makofi)
Name
Luhaga Joelson Mpina
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisesa
Answer
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Goodluck Mlinga, Mbunge wa Ulanga kwamba tutajenga josho katika jimbo lake mwaka huu ujao wa fedha pamoja na kisima, siyo josho tu ni pamoja na kisima cha kunyweshea mifugo maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunajua kuna tatizo la uanzishaji wa masoko ambapo watu wengine wanaanzisha masoko bila utaratibu na wengine wanakosa mwongozo. Kwa hiyo, hili tunalisimamia vizuri na katika mwaka huu wa fedha tutayamaliza yote haya. Tutahakikisha kwamba miongozo ipo ya kutosha kuhakikisha kwamba masoko mahali popote yanapoanzishwa yanazingatia miundombinu mahsusi inayotakiwa na eneo mahali linapohitajika.
Name
Dr. Haji Hussein Mponda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Malinyi
Primary Question
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Wilaya ya Ulanga ina ongezeko la mifugo; ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe lakini hakuna huduma za mifugo kama vile majosho:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majosho?
Supplementary Question 2
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Ulanga na Malinyi ni walewale. Suala hili la miundombinu la mifugo tumelipigia kelele muda mrefu na tumeielekeza na kuishauri Serikali watumie Mfuko wa Maendeleo ya Mifugo (Livestock Development Fund) ambayo inakusanywa kutokana na minada waweke percentage ili kuwa na uhakika wa kuhudumia miundombinu hiyo pamoja na malambo na majosho. Ni lini Serikali watatekeleza maagizo haya ambayo mara nyingi tumetoa hapa Bungeni?
Name
Luhaga Joelson Mpina
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisesa
Answer
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ni muda mfupi sana sasa hivi Waziri wa Mifugo na Mvuvi atawasilisha hotuba yake, masuala yote yamesheheni humo ataona mipango yetu madhubuti kabisa ambapo sasa mifugo nchi hii haiwezi kufa tena kwa kukosa malisho na maji. (Makofi)
Name
Vedasto Edgar Ngombale Mwiru
Sex
Male
Party
CUF
Constituent
Kilwa Kaskazini
Primary Question
MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Wilaya ya Ulanga ina ongezeko la mifugo; ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe lakini hakuna huduma za mifugo kama vile majosho:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa majosho?
Supplementary Question 3
MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi. Kilwa ni miongoni mwa eneo ambalo mifugo inakuja kwa wingi na Serikali haijaandaa kabisa miundombinu. Serikali ina mpango gani kutujengea malambo Kilwa ile mifugo iliyopo pale iweze kupata afya inayostahili? (Makofi)
Name
Luhaga Joelson Mpina
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisesa
Answer
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaanza na kisima kimoja mwaka huu ujao wa fedha kwa Mheshimiwa Mbunge.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved