Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mwaka 1974 Tanzania iliridhia Mkataba wa Kuzuia Uchafuzi wa Bahari na Usalama wa Bahari ambao lengo mojawapo ni kuzuia uvuvi haramu wa kutumia mabomu na kutoa misaada ya vifaa vya kuzuia uchafuzi wa bahari:- (a) Je, Serikali imeweka mikakati gani ya kuzuia uvuvi haramu wa kutumia mabomu ambao bado unaendelea? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wavuvi ili waachane na uvuvi haramu wa kutumia mabomu?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu haya yenye kuleta matumaini kwa wavuvi wetu, lakini yametuelekeza namna ambavyo Serikali inaendelea kulinda mazingira ya bahari na kuendelea kulinda viumbe vilivyopo ndani ya bahari na kuendelea kuleta tija kwa wavuvi wetu. Sasa napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo ya Lindi Manispaa, Lindi Vijijini maeneo ya Kilwa, vijana sasa wameamua kujitengenezea ajira kupitia shughuli za uvuvi na tayari wamejiunga katika vikundi mbalimbali. Napenda kujua ni lini sasa Serikali itakuja kuwawezesha angalau kuwapa fiber boat na injini za boti ili vijana wale waendelee kuwa na uvuvi wa tija na kuongeza vipato vyao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, napenda sasa Serikali ituambie italeta lini mwongozo ambao utatuelekeza ni nyavu zipi zitatumika katika maziwa, mito na bahari. Unaposema kutumia nyavu ya nchi mbili, samaki wa baharini ni tofauti na samaki hao wa maziwa. Kwa mfano baharini kuna chuchungi…
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna dagaa, lakini unaposema tutumie nyavu ya nchi mbili maana yake samaki wale huwezi kuwapata. Napenda Serikali iseme ni lini itatuletea mwongozo wa namna nyavu zitakavyotumika zile za bahari, maziwa pamoja na mito?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hayo ahsante sana. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza nampongeza sana kwa ufuatiliaji wake wa karibu wa masuala yanayohusua wananchi na hasa wavuvi wa kule Lindi. Anauliza lini Serikali itawawezesha vijana, nataka nimhakikishie tu kwamba Serikali iko tayari, tunapokea maombi hasa yanayohusu vifaa kwa maana ya injini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari wiki iliyopita tumeshapokea maombi kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge wa Lindi anayeitwa Mheshimiwa Hamidu Bobali akiomba mashine kwa vikundi viwili. Kwa hivyo, nafahamu Mheshimiwa Hamida ni Mbunge makini na yeye namkaribisha ofisini kutuletea hayo maombi na mashine zipo kwa ajili ya kuweza kuwasaidia vijana na vikundi vya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni lini Serikali itaweka mwongozo wa matumizi ya nyavu katika maeneo mbalimbali. Tunafikiria mwaka huu kuleta maboresho ya sheria lakini kwa maelezo zaidi na kwa uelewa mpana zaidi wa sekta hii ya uvuvi Wizara yetu imeandaa semina kwa Wabunge wote ambayo itakwenda kujibu masuala yanayohusu tasnia nzima ya uvuvi siku ya Jumapili na tunawakaribisha Waheshimiwa Wabunge muweze kushiriki kikamilifu katika semina hii. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mwaka 1974 Tanzania iliridhia Mkataba wa Kuzuia Uchafuzi wa Bahari na Usalama wa Bahari ambao lengo mojawapo ni kuzuia uvuvi haramu wa kutumia mabomu na kutoa misaada ya vifaa vya kuzuia uchafuzi wa bahari:- (a) Je, Serikali imeweka mikakati gani ya kuzuia uvuvi haramu wa kutumia mabomu ambao bado unaendelea? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wavuvi ili waachane na uvuvi haramu wa kutumia mabomu?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa zoezi hili la kuzuia uvuvi haramu linatumiwa sasa na vikosi vya doria kunyanyasa, kudhalilisha na kupora wananchi hasa wavuvi kwenye Visiwa vya Ukerewe kwa kuwadai pesa na malipo mbalimbali yasiyo halali. Nataka kujua Serikali iko tayari kutoa kauli kuzuia unyanyasaji huo lakini na Mheshimiwa Waziri kufika Ukerewe kukaa na wavuvi na kupata ushahidi wa haya yaliyotokea ili Serikali iweze kuchukua hatua kwa wahusika? Nashukuru. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa swali la Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe. Naomba kusema kwamba kama kuna changamoto yoyote ambapo watendaji wetu kwa namna ile wameenda kinyume na misingi na taratibu tulizowapa, watendaji wetu wote wanapoenda doria wanapewa mwongozo wa makosa gani ambayo yanatakiwa kuchukuliwa hatua na kwa kiasi gani. Mheshimiwa Mbunge kama anayo hiyo orodha ya watu ambao anasema kwamba hawakutendewa haki atuletee sisi tutalishughulikia mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mimi kwenda Ukerewe…

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mwaka 1974 Tanzania iliridhia Mkataba wa Kuzuia Uchafuzi wa Bahari na Usalama wa Bahari ambao lengo mojawapo ni kuzuia uvuvi haramu wa kutumia mabomu na kutoa misaada ya vifaa vya kuzuia uchafuzi wa bahari:- (a) Je, Serikali imeweka mikakati gani ya kuzuia uvuvi haramu wa kutumia mabomu ambao bado unaendelea? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wavuvi ili waachane na uvuvi haramu wa kutumia mabomu?

Supplementary Question 3

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ya uvuvi haramu katika maeneo ya Lindi yanafanana sana na matatizo ya uvuvi haramu katika Kisiwa cha Mafia. Taasisi iliyopewa mamlaka ya kushughulika na uvuvi haramu Mafia imejitwika majukumu mengi zaidi ya uhifadhi kwa maana ya wanauza maeneo ya vivutio na kukusanya mapato. Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba Taasisi ya Hifadhi ya Bahari ya Mafia wanabaki na kazi ya uhifadhi peke yake badala ya kujishughulisha na kukusanya mapato? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Hifadhi ya Bahari kwa Kiingereza tunaiita kwa kifupi MPRU ipo kwa mujibu wa sheria za nchi. Miongozo ya kuanzishwa kwake MPRU kwa maana ya hifadhi ya bahari inawaelekeza kufanya kazi kadha wa kadha.
Moja ya kazi hizo ni uhifadhi lakini mbili ni kusimamia masuala yanayohusu wanaokuja katika maeneo yale ya hifadhi ikiwa ni pamoja na kuwatoza ushuru ambao kwa pamoja unarudishwa katika vijiji na Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa mfumo wa asilimia 30. Asilimia 10 inakwenda katika halmashauri ya wilaya na asilimia 20 inakwenda moja kwa moja katika vijiji vinavyohusika na uhifadhi ule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la Mheshimiwa Mbunge ni lini sasa MPRU itajielekeza katika kusimamia uhifadhi tu badala ya kukusanya ushuru. Masuala haya ni ya kisheria na kikanuni tunamkaribisha Mheshimiwa Dau kwa hoja hiyo mahsusi kabisa ya kutaka kwamba MPRU ijielekeze na uhifadhi tu badala ya kufanya shughuli zingine ikiwemo hiyo ya kukusanya mapato. Ahsante sana. (Makofi)