Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani juu ya urithi wa Dunia wa Kisiwa cha Kilwa Kisiwani?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. La kwanza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, atakumbuka mnamo mwaka 1981 Serikali ilikitangaza Kisiwa hiki cha Kilwa Kisiwani kuwa Urithi wa Dunia. Hadi kufikia mwaka jana Serikali ilipokea bilioni saba kutoka kwa wafadhili kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu iliyopo Kilwa Kisiwani ili kuvutia watalii wengi zaidi.
Mheshimiwa Spika, nitapenda kupata majibu ya Serikali ni kwa nini sasa ujenzi wa miundombinu hii haujafanyika ilhali wameshapokea bilioni saba kutoka kwa wafadhali na pengine Serikali ingeweza kuongeza fedha ili huu ukarabati wa magofu unaoendelea uweze kwenda sambamba na ukarabati wa miundombinu?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana na mimi, watalii wengi zaidi kutoka nchi mbalimbali duniani wangependa kutembelea urithi huu wa dunia, lakini hadi hivi tunavyozungumza hakuna kivuko cha kueleweka cha kuwavusha watalii kutoka Kilwa Masoko kwenda Kilwa Kisiwani, kitu ambacho kingeweza kuingizia mapato Serikali yetu. Nataka kujua sasa ni lini kivuko hicho kitajengwa kutoka Kilwa Masoko kwenda Kilwa Kisiwani ili kuinua kasi ya uchumi katika sekta hii ya utalii? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Kilwa Kisiwani tumepokea fedha zaidi ya bilioni saba kwa ajili ya ukarabati wa majenzi yaani ukarabati wa magofu yote ambayo yapo Kilwa Kisiwani. Naomba nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba Kisiwa cha Kilwa Kisiwani kina magofu mengi sana na hizo bilioni saba bado ni kidogo.
Mheshimiwa Spika, hizi tulishaanza kuzifanyia kazi tayari, tumeanza ukarabati na hao vijana ambao wameshapata mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kukarabati hayo majenzi wako kazini. Mimi mwenyewe tarehe 9 Machi, nilikuwa kule nikashuhudia jinsi kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa na wale vijana. Kwa hiyo, siyo kwamba zile fedha zimekaa, fedha zile zinaendelea tayari kufanya kazi.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusu kivuko ni kweli kabisa nimeshuhudia katika lile eneo kwamba tukipata kivuko cha kisasa, kizuri kinaweza kikasaidia sana katika kuwavutia watalii ili waweze kufika katika lile eneo. Hivi sasa Serikali inaendelea kujipanga pale hali itakaporuhusu ya kifedha basi tutaweza kupata kivuko hicho ili kiweze ku- promote utalii katika aneo hilo la Kilwa Kisiwani.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani juu ya urithi wa Dunia wa Kisiwa cha Kilwa Kisiwani?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Mkutano wa World Heritage ambao ulifanyika nchini Qatar, Pori la Akiba la Selou na lenyewe lilitangazwa kama urithi wa dunia na nchi mbalimbali zilikubaliana kuisaidia Tanzania takribani dola milioni mbili kwa ajili ya kupambana na ujangili wa tembo. Nataka kujua status ya hali ya ujangili wa tembo katika Pori la Akiba la Selous?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa kweli kwa sasa hivi hali kidogo ni nzuri, hakuna tena ujangili kama ambavyo umekuwepo na ndiyo maana matukio mbalimbali yale ambayo tulikuwa tunapotelewa na tembo na maeneo mengine yamepungua kwa kiwango kikubwa sana katika hili eneo.