Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE A. TAMBWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Tabora?

Supplementary Question 1

MHE. MUNDE A. TAMBWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza kabisa nianze kwa kuishukuru Serikali kwa kutuletea pesa kwenye Wilaya ya Sikonge, Nzega na Uyui kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za wilaya, naishukuru sana Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza swali langu la kwanza la nyongeza. Ukizingatia population ya Wilaya ya Tabora Manispaa, ukizingatia Sera ya Serikali yetu kwamba mnatakiwa muanze ninyi wenyewe na Serikali iwa-support kitu ambacho wananchi wa Tabora Manispaa wameshakifanya. Kinachotushangaza zaidi ni pale Wilaya mpya zilizoanza mwaka jana zinavyopelekewa pesa ya kujenga Hospitali ya Wilaya na kuacha kupeleka katika Wilaya za zamani…
MHE. MUNDE A. TAMBWE: zenye watu wengi na…
MHE. MUNDE A. TAMBWE: ...kuacha kupeleka kwenye Wilaya ya Tabora Manispaa. Je, Serikali inanipa commitment gani sasa ya kuleta pesa kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Tabora Manispaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Jimbo la Igalula halina hata zahanati moja wala kituo cha afya kimoja; hii inasababisha wananchi wote wa Jimbo hilo kwenda kwenye hospitali kubwa ya Mkoa wa Tabora ambayo ni Kitete na kuongeza msongamano mkubwa. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha inaleta pesa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya na kumalizia zahanati ambazo zilianzishwa na wananchi wa Jimbo la Igalula pamoja na Mbunge wao na mimi Mbunge wao wa Viti Maalum? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika tangu nimeingia Bunge hili na Mheshimiwa Munde akiwa ndani ya Bunge hili amekuwa ni mpiganaji kuhusiana na suala zima la afya kwa Mkoa wake wa Tabora, nampongeza sana kwa jitihada zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maswali yake mawili, swali la kwanza anauliza commitment ya Serikali katika kuhakikisha kwamba tunakamilisha ujenzi wa hospitali ya Manispaa ya Tabora kwa maana ya hospitali ya wilaya. Katika jibu langu la msingi nimemweleza commitment ya Serikali kwamba katika awamu ya pili, fedha zitakazopatikana kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za wilaya hatutaisahau Manispaa ya Tabora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anaongelea kuhusiana na Igalula ambayo hawana kituo cha afya na Hospitali ya Wilaya. Kwanza naomba niwaase na niwaombe wananchi wa Igalula, wao waanzishe ujenzi kama ambavyo Manispaa ya Tabora wamefanya na pesa ikipatikana awamu itakayofuata na sisi kama Serikali tutahakikisha kwamba tunaunga mkono juhudi za wananchi. (Makofi)

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE A. TAMBWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Tabora?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Miongoni wa vitu vya afya ambavyo vilipangiwa kupatiwa pesa Mkoani Ruvuma ni pamoja na Kituo cha Afya Namtumbo na Mkasali. Naishukuru Serikali vituo hivyo vimepata pesa. Hata hivyo, kipo Kituo cha Afya cha Matemanga ambacho kilipangiwa kupatiwa pesa kwa ajili ya ukarabati, lakini pesa ile mpaka sasa haijaenda. Ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na hiyo pesa ya ukarabati wa vituo vya afya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yale ya awali. Naomba kumpa comfort kwanza mtani wangu Mnyamwezi. Mheshimiwa Ntimizi wiki iliyopita alikuja ofisini kwetu pale kwa ajili ya vituo vya afya vitano vilivyoanzishwa katika mchakato wa ujenzi wa na tumewapa commitment kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itahakikisha kwamba ina- support ndani ya mwaka huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kuhusu suala la Matemanga, tayari naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ndani ya wiki hii tu-cross-check accounts zetu kule katika halmashauri yetu, tutakuwa tumeshaingiza hizo fedha tayari kwa ajili ya kuhakikisha kituo kile kinakamilika. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. MUNDE A. TAMBWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Tabora?

Supplementary Question 3

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kambi ya Simba Wilayani Karatu umekamilika kwa ufanisi mkubwa na kituo hicho sasa kiko tayari kuanza kutoa huduma. Hata hivyo, kituo hicho hakina gari la wagonjwa na ukizingatia Wilaya ya Karatu haina hospitali ya wilaya, je, ni lini Serikali italeta gari kwa ajili ya huduma ya wagonjwa kwenye kituo hicho?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunashukuru kwa kazi nzuri ambayo mwenyewe ana-recognise kwamba kituo cha afya kimekamilika na kiko kwenye hali nzuri. Hatua inayofuata anaomba upatikanaji wa gari la ambulance ili kuweza kusaidia huduma ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba uhitaji wa gari kwa ajili ya wagonjwa ni mkubwa sana. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kadri nafasi zitakavyopatikana, tulipata magari 50 na tumeweza kuyagawa, tukipata gari nyingine naamini na wao watakuwa miongoni mwa maeneo ambayo yatapata fursa ya kupata magari.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE A. TAMBWE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Tabora?

Supplementary Question 4

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pia nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali yetu ya Wilaya iliyopo katika Manispaa ya Iringa ilifunguliwa ili kupunguza msongamano mkubwa uliyopo katika hospitali ya mkoa, lakini hospitali ile mpaka sasa hivi haina jengo la vipimo, haina wodi za wagonjwa wengine ina wodi za wazazi na hospitali ile imekuwa ikisaidia wagonjwa wanaotoka katika Wilaya ya Kilolo, Iringa DC na kwingineko; na Mheshimiwa Jafo tunamshukuru alifika; je, Serikali sasa inasaidiaje pamoja na kuwa imetoa pesa kwa ajili ya kujenga hospitali za wilaya nyingine wakati bado hazijajengwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba ukienda Manispaa ya Iringa na kwa kuanzia hospitali ya mkoa ina wagonjwa wengi sana, ndiyo maana Serikali katika kuhakikisha kwamba tunapunguza mlundikano wa wananchi kwenda kutibiwa katika hospitali ya mkoa, ikawa ni wajibu kuhakikisha kwamba inajengwa hospitali ya wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama anavyotoa maelezo kwamba ile hospitali ya wilaya haijakamilika kwa kiwango ambacho kilitarajiwa, naomba nimhakikishie, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba hospitali zote za wilaya ambazo zinajengwa zinakuwa katika kiwango ambacho tunakitarajia ili mwananchi akipata rufaa kutoka kituo cha afya akienda kutibiwa kwenye hospitali ya wilaya apate matumaini kwamba nimefika katika hospitali ambayo hakika kwa majengo na huduma ataweza kupona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie, kwa kadri bajeti itakavyokuwa imeruhusu tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba suala la afya ni kipaumbele kama Serikali ilivyoelekeza.