Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 96 2018-04-18

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE A. TAMBWE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Tabora?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Munde Abdallah Tambwe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Manispaa ya Tabora hupata huduma za afya kupitia kwenye zahanati 22 zilizopo kwenye Wilaya hii. Kwa kuwa zahanati inatoa huduma za magonjwa madogo (minor illness), wananchi wa Manispaa ya Tabora hupata huduma kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete. Hata hivyo, Hospitali ya Mkoa kwa sasa imeelemewa na wagonjwa wengi, hivyo manispaa imeona ni vyema ianzishe ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ulianza mnamo tarehe 19/10/2015 kwa kuanza na jengo la OPD kwa gharama ya shilingi milioni 150 chini ya mkandarasi HERU Construction Company Limited ambapo hadi sasa sehemu ya msingi, nguzo, ngazi na slabu vimekamilika kwa asilimia 100, mkandarasi ameshalipwa jumla ya shilingi milioni 145.7 kwa fedha za ruzuku ya miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2018/2019, Manispaa ya Tabora imetenga shilingi milioni sabini kwa ajili ya ujenzi wa jengo la OPD katika hospitali hiyo. Vilevile Ofisi ya Rais, TAMISEMI itahakikisha inatoa kipaumbele kwa Manispaa ya Tabora katika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya mara fedha za awamu ya pili zitakapo patikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inasisitiza kuhakikisha fedha za miradi zinazopatikana zilenge katika ukamilishaji wa miradi iliyopo badala ya kuibua miradi mipya; kwa mfano fedha za Local Government Capital Development Grand (LG- CDG) milioni 483.5 kwa mwaka 2017/2018 ambazo zilitolewa maelekezo kwamba zitumike katika kukamilisha miradi iliyokwishaanzishwa.