Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Je, Serikali imefanya tathmini juu ya ubora na changamoto zilizopo katika shule za sekondari za kata nchini?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba sasa niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, shule za kata tangu zimeanzishwa sasa takribani ni muongo mmoja; na kwa bahati mimi nilikuwa ni miongoni mwa walimu walioanzisha shule za kata. Matatizo na changamoto yaliyokuwepo mwaka 2006/2007 wakati shule za kata zinaanzishwa kama vile madarasa, ukosefu wa maabara, ukosefu wa walimu wa sayansi na hisabati, bado mpaka leo changamoto zile zipo.
Naomba sasa kujua ni lini Serikali itatuhakikishia kwamba changamoto za walimu wa sayansi, hisabati na madarasa katika shule zetu zitakwisha? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, hivi karibuni Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati anazindua Mbio za Mwenge kule Geita, aliorodhesha mikoa inayoongoza kwa utoro na Mkoa wa Lindi siyo miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa utoro; bahati mbaya ni miongoni mwa mikoa inayofanya vibaya sana katika matokeo ya kidato cha nne na matokeo ya darasa la saba. Moja ya mkakati wa Mkoa ni kuhakikisha tunatoa chakula mashuleni.
Naomba sasa leo Serikali iji-commit hapa; je, iko tayari sasa kutuhakikishia kwamba sisi wa Mkoa wa Lindi tuendelee na programu ya kuwashirikisha wazazi ili waendelee kuchangia chakula ili matokeo yaweze kuboreka katika shule zetu? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa kuanzia mwezi Oktoba, 2017 hadi sasa tumeajiri walimu 200 wa masomo ya sayansi na hisabati. Mpango uliopo hadi tarehe 30 Juni tutaajiri walimu 6,000 na lengo tunataka kuondoa kabisa tatizo la walimu wa sayansi na hisabati katika shule za sekondari ifikapo mwaka 2020, maana yake inakwenda polepole.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la miundombinu pamoja na chakula, nimhakikishie Mheshimiwa Hamidu Bobali na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba Serikali haijakataza michango ya wananchi kuchangia miundombinu ya shule zikiwemo maabara. Kilichokatazwa ni kumpa adhabu mwanafunzi ya kukosa masomo kwa sababu tu mzazi wake hajatoa mchango. Kwa hiyo, hiyo ndiyo iliyokatazwa, lakini kupitia Serikali za Vijiji, mnaruhusiwa kuendelea kuhamasisha wananchi ili wachangie maendeleo ya shule zao ikiwemo miundombinu pamoja na chakula. (Makofi)

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Je, Serikali imefanya tathmini juu ya ubora na changamoto zilizopo katika shule za sekondari za kata nchini?

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, wamesema wanaajiri walimu wa sayansi, hisabati na kadhalika, lakini bado tatizo la walimu hao ni kubwa. Nataka kujua tu, wamefanya sensa, ni walimu wangapi wa sayansi ambao kila siku wanaacha kazi kwa sababu ya maslahi duni katika Serikali?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili ni gumu sana, kwa sababu hatuna takwimu za kila mwaka kwamba ni walimu wangapi wa sayansi na hisabati wanaacha kazi.
Lakini comfort niliyonayo na ambayo nataka niwape Waheshimiwa Wabunge ni kwamba malalamiko tuliyonayo ni ya walimu kutaka kuhama haraka katika shule wanazopelekwa, yaani mwalimu anaweza akapelekwa kwenye shule fulani, akikaa baada ya wiki mbili anataka ahame. Hiyo ndiyo changamoto kubwa tuliyonayo ambayo tunaishughulikia.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuacha kazi, hilo naomba sana tutoe majibu baadae.

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Je, Serikali imefanya tathmini juu ya ubora na changamoto zilizopo katika shule za sekondari za kata nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelezo yake Mheshimiwa Waziri amekiri kabisa kuwa kuna upungufu mkubwa wa walimu wa sayansi. Pamoja na mikakati mizuri ambayo Wizara mnaifanya, mtambue kabisa kwamba walimu wetu wa sayansi wana work load kubwa sana uki- compare na walimu wengine. Tuna shule moja Wilaya ya Kilolo inaitwa Shule ya Lukosi ina mwalimu mmoja wa sayansi kati ya watoto 700.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu kwa Mheshimiwa Waziri; ni incentives gani kama Wizara imejipanga kuhakikisha inawapa motisha hata hawa walimu wachache waliopo ili wawe chachu kwa watoto wetu waweze kufanya vizuri? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri ambalo ameonesha concern kubwa kuhusu walimu wa sayansi, namna ambavyo tunaweza tukawafanya wajisikie kwamba Serikali inawajali.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ambalo tumefanya kama Serikali, ni kuhakikisha kwamba tumeweka package ambayo ni nzuri zaidi kwa walimu wa sayansi hata wanapoanza kazi kuliko hata walimu wa sanaa. Kwa hiyo, hiyo ni sehemu ya motisha kwao.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunasisitiza sana kwamba wanapofika katika shule, Walimu Wakuu na Maafisa Elimu wawapokee vizuri, wawape counseling ili wakubali kuishi katika maeneo wanayopelekwa, hilo ndiyo jambo la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mengine tutaendelea kuboresha kwa sababu mengine hatuwezi kuweka motisha kubwa sana, kwa sababu nao ni watumishi sawasawa na watumishi wengine. Sasa kama utabagua, una watumishi ambao ni walimu halafu unabagua; huyu lazima apewe nyumba, huyu kwa sababu una uhasama naye, asipewe nyumba. Hicho nadhani itakuwa ni kitu ambacho siyo kizuri sana katika Taifa letu.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Je, Serikali imefanya tathmini juu ya ubora na changamoto zilizopo katika shule za sekondari za kata nchini?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la nyongeza ni kama ifuatavyo; mwaka 2016 tulipata tatizo kule Lindi kwenye shule ya sekondari ambayo ni shule kongwe. Wananchi wamejitahidi kadri walivyoweza lakini bajeti yake ni shilingi bilioni mbili. Serikali itatusaidiaje juu ya ujenzi wa shule hiyo ambayo iliungua moto mwaka 2016? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Salma Kikwete kwa sababu amekuwa akijitolea sana kuhusu kuinua elimu katika Mkoa wa Lindi, na hasa hii shule ya sekondari ya Lindi, ameichukua imekuwa kipaumbele kikubwa sana kwake. Kwa kweli namshukuru sana, ameongoza harambee nyingi, hata juzi tulikuwa kwenye harambee pale Dar es Salaam kwa ajili ya kuichangia hii shule na tukapata karibu shilingi milioni 282; na mwaka 2018 ilifanyika harambee zikapatikana shilingi milioni 550. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Salma Kikwete na Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi na wananchi wa Lindi kwa ujumla kwamba shule hii ambayo iliungua madarasa tisa na ofisi tatu za Walimu mwaka 2016, mwaka ujao wa fedha tutahakikisha kwamba madarasa 27 na ofisi tisa za walimu ambazo wamepanga kujenga yatakamilika. (Makofi)