Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Kwa juhudi zake Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale ameanzisha ujenzi wa baadhi ya majengo ya zahanati kubwa na za kisasa katika Vijiji vya Nyamikonze na Inyenze. (a) Je, Serikali ipo tayari kusaidia kukamilisha ujenzi huo? (b) Je, Serikali ipo tayari kuifungua zahanati iliyojengwa na Mbunge katika Kijiji cha Mwamakilinga ambayo imekamilika tangu Novemba, 2014?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo ya nyongeza, lakini naomba nitumie nafasi hii kuwapa pole wananchi wangu wa Jimbo la Nyang’hwale kwa mauaji ya kikatili ambayo yamefanyika wiki iliyopita, akina mama wanne wamenyongwa kwa kutumia kanga zao na wawili wakiwa wajawazito na mauaji hayo yanaendelea kwa Wilaya za jirani.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali dogo la nyongeza ni kama ifuatavyo; je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha kuisaidia Halmashauri ya Nyang’hwale ili kukamilisha ujenzi wa zahanati iliyopo Iyenze na Mwamakiliga? Serikali ina mpango gani kuisaidia Halmashauri?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naishukuru AMREF kwa kukamilisha majengo matatu yaliyopo pale Kituo cha Afya Kharumwa. Serikali ina mpango gani baada ya kukamilishwa majengo hayo kuendeleza kwa kutusaidia kuongeza vifaatiba pamoja na wauguzi? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kwa dhati kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa jitihada zake za kuhakikisha wananchi wanapata huduma iliyo bora ya afya. Yeye hakika ni mfano bora wa kuigwa kwa Waheshimiwa Wabunge wengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza, anauliza Serikali kusaidia Halmashauri kumalizia zahanati, ni nia ya dhati kabisa ya Serikali kuhakikisha kwamba tunasaidia, lakini kinachogomba ni uwezo. Kwa hiyo, kadri bajeti itakavyokuwa imeboreka, hakika hatuwezi tukawaacha wananchi ambao Mheshimiwa Mbunge ameonesha jitihada tukaacha kumalizia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili baada ya kazi nzuri iliyofanywa na AMREF, suala la zima la kupeleka vifaa pamoja na wataalam, ili kazi iliyotarajiwa iweze kuwa nzuri, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vituo vya afya na zahanati zetu zote zinafanya kazi. Muda siyo mrefu, wakati tunahitimisha, Mheshimiwa Waziri wa Utawala atakuja kusema neno kuhusiana na suala zima la kuajiri watumishi wa Serikali. (Makofi)

Name

Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Kwa juhudi zake Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale ameanzisha ujenzi wa baadhi ya majengo ya zahanati kubwa na za kisasa katika Vijiji vya Nyamikonze na Inyenze. (a) Je, Serikali ipo tayari kusaidia kukamilisha ujenzi huo? (b) Je, Serikali ipo tayari kuifungua zahanati iliyojengwa na Mbunge katika Kijiji cha Mwamakilinga ambayo imekamilika tangu Novemba, 2014?

Supplementary Question 2

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Mtikila kilijenga zahanati ambayo ilikamilika mwaka 2015, lakini mpaka leo haijafunguliwa kwa sababu ya tatizo la vifaa na wataalam. Namuomba Naibu Waziri aniambie, ni lini watafungua zahanati hii ili kutokudhoofisha nguvu za wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tulipokea katika michango ya Mheshimiwa Bobali na nikayarudia katika moja ya maswali ambayo nilikuwa najibu hapa, kwamba ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba zahanati ambazo zimekamilika huduma itatolewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimetangulia kusema muda siyo mrefu kwamba ni siku ya leo ambapo Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya Utawala atakuja kuhitimisha na atasema neno kuhusiana na suala zima la kupatikana wahudumu wa afya na waganga, maana na sisi tunategemea kupata kibali cha ajira kutoka kwake.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Kwa juhudi zake Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale ameanzisha ujenzi wa baadhi ya majengo ya zahanati kubwa na za kisasa katika Vijiji vya Nyamikonze na Inyenze. (a) Je, Serikali ipo tayari kusaidia kukamilisha ujenzi huo? (b) Je, Serikali ipo tayari kuifungua zahanati iliyojengwa na Mbunge katika Kijiji cha Mwamakilinga ambayo imekamilika tangu Novemba, 2014?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira yaliyopo Jimbo la Nyang’hwale yanafanana kabisa na mazingira yaliyopo kwenye Jimbo la Ndanda na hasa kwenye Kata ya Chiwata ambapo kuna Shule ya Sekondari ya Chidya. Wananchi wa Chidya waliamua wenyewe kutumia nguvu zao kujenga jengo pale kwa ajili ya kuweza kupata zahanati. Kwa bahati mbaya kabisa, maelekezo niliyokuwa nawaambia, watakapokuwa wamefanikiwa kukamilisha boma, wawe wameendelea juu wameweka mpaka bati, Serikali itakuja kumalizia kuwaletea vifaa pamoja na kufungua.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri ya kututaka tusubiri, lakini napenda watu wale wasikie, Chidya ni sehemu ya mkakati wa hiyo mikakati yenu ya Wizara kukamilisha maboma hayo na lini hiyo kazi itafanyika? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali na pia ni azma ya CCM; ukisoma katika Ilani ya CCM ukurasa wa 81 Ibara ya 50 tumetaja kabisa kwamba kila sehemu ambayo ipo kijiji tutahakikisha kwamba inajengwa zahanati, kila Kata itakuwepo na Kituo cha Afya na kila Wilaya itakuwa na Hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, ni azma thabiti na ndiyo maana imeandikwa. Naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge avute subira.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba wananchi wake kama ilivyo Nyang’hwale wamejitolea, lakini sina uhakika kama naye Mheshimiwa Mbunge amefanya kazi nzuri kama Mbunge wa Nyang’hwale. Na yeye tumtake ashirikiane na Serikali, kwani wanaotibiwa ni wananchi wetu. Kwa hiyo, ni vizuri wote tukashiriki katika suala zima la kuhakikisha kwamba afya inakuwa bora. (Makofi)

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Kwa juhudi zake Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale ameanzisha ujenzi wa baadhi ya majengo ya zahanati kubwa na za kisasa katika Vijiji vya Nyamikonze na Inyenze. (a) Je, Serikali ipo tayari kusaidia kukamilisha ujenzi huo? (b) Je, Serikali ipo tayari kuifungua zahanati iliyojengwa na Mbunge katika Kijiji cha Mwamakilinga ambayo imekamilika tangu Novemba, 2014?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwanza nipongeze kazi nzuri ya kuboresha mazingira ya kutolea afya katika maeneo yetu kwa nchi nzima. Kutokana na shida kubwa ya afya iliyopo katika maeneo yetu tuliyokuwa nayo, Serikali ije na mpango mahususi wa kuhakikisha kwamba zile nguvu za wananchi katika maeneo yote waliyojenga maboma ya zahanati na nyumba za wauguzi, inawasaidia kumaliza maboma hayo. Je, Serikali lini itafanya hilo ili kumaliza shida ya afya katika maeneo yetu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, mpango mahususi wa Serikali upo na ndiyo maana katika bajeti hii ambayo tunakwenda kumaliza, jumla ya vituo 208 vinaenda kujengwa, lakini pia katika bajeti ambayo ndiyo tunaomba Waheshimiwa Wabunge leo wapitishe, nina uhakika kwamba ikipitishwa jumla ya shilingi bilioni 100.5 inaenda kutumika kwa ajili ya kujenga Hospitali za Wilaya 67 katika Halmashauri zetu. Hiyo yote inaonesha dhamira ya Serikali kwamba ina nia ya kuhakikisha kwamba tatizo la afya linaondolewa.