Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Msalala hususan wakazi wa Bulyanhulu wamefanyiwa dhuluma nyingi sana na Mgodi wa ACACIA, Bulyanhulu ikiwemo kuondolewa kwenye maeneo yao bila fidia mwaka 1996 na kwa wale wanaopata kazi mgodini kufukuzwa kazi bila kufuata utaratibu, kupata madhara makubwa ya kiafya na hata kusababishiwa vifo; na Serikali ya Awamu ya Tano imesimama kidete kutetea wananchi na kuwaepushia dhuluma hizi. Je, ni hatua gani imefikiwa katika mazungumzo kati ya ACACIA na Serikali kuhusu ulipaji fidia kutokana na dhuluma hizo?

Supplementary Question 1

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kabla sijauliza maswali ya nyongeza naomba nioneshe tu masikitiko yangu kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri kimsingi hajaenda kwenye thrust ya swali langu.
Swali langu nimeuliza je, ni hatua gani imefikiwa katika mazungumzo kati ya ACACIA na Serikali kuhusu ulipaji wa fidia na athari nyingine ambazo wananchi wa msalala wamezipata?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika majibu yake pia, amesema kwamba hakuna fidia inayodaiwa, jambo ambalo si kweli kwa sababu kwa miaka 22 Serikali inafahamu kwamba watu walioondolewa mwaka 1996 Bulyanhulu, hakuna shilingi moja iliyolipwa. Mbaya zaidi kwa hawa wagonjwa Serikali imesema wamepatikana wagonjwa 78, lakini haijasema hatua gani zinachukuliwa kuhakikisha wanatibiwa, kwa sababu tayari kuna watu 49 wameshafariki na hawajalipwa fidia yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niulize maswali mawili yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa sababu uharibifu au wizi uliofanywa na ACACIA kwa Tanzania haujafanywa kwa Tanzania peke yake, umefanywa hasa kwa wananchi wa Bulyanhulu pia; na kwenye ripoti ya Profesa Ossoro ilionesha mabilioni mengi ambayo Tanzania ilipaswa kupata na mimi nilishasema kwamba wananchi wa Msalala wanastahili kulipwa shilingi bilioni 973 kama service levy.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilitaka kujua kwa sababu ACACIA walisha-concede hivyo na tayari walishatoa kishika uchumba kwa Serikali, kile cha dola milioni 300. Nilitaka kujua kwa wananchi wa Msalala wanaodai bilioni 973, je, Serikali inaweza ikawasaidia sasa ili angalau katika hii mitambo inayotaka kuuzwa na ACACIA ikabidhiwe kwa Halmashauri kama sehemu ya fidia ya service levy ambayo haijalipwa kwa miaka yote? Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili,...
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Swali la pili, katika uwasilishwaji wa taarifa ya mazungumzo Mheshimiwa Rais aliagiza kwamba uchunguzi ufanyike kwenye migodi mingine kuhusu utoroshwaji wa madini, ukiacha makinikia peke yake, utoroshwaji wa vitofali vya dhahabu na Wizara iliagizwa kwamba ifanye uchunguzi kwenye migodi mingine. Nilitaka kujua uchunguzi kwenye hilo eneo umefikia hatua gani?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la msingi imeonesha kabisa Mheshimiwa Mbunge ameuliza kuhusiana na masuala ya fidia. Kwa taarifa tulizonazo katika Wizara yetu ni kwamba Mgodi ule wa Bulyanhulu ulivyokuwa unaanzishwa na kuanza kufanya kazi zake mwaka 2000 hakukuwa na madeni yoyote ambayo mgodi unadaiwa. Isipokuwa kama Mbunge ana hao watu ambao anawafahamu wanadai fidia katika yale maeneo kwa sababu yale maeneo ya Mgodi wa Bulyanhulu waliyapata kutoka Serikalini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli kuna watu ambao wanadai fidia zao, basi tunamuomba Mheshimiwa Mbunge awalete hao watu na madai yao, sisi kama Wizara tuko tayari kuwasimamia na kuhakikisha kwamba hakuna mwananchi yeyote anayedhulumiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile ni kwamba ile taarifa ya ACACIA ambayo waliji-committ kutoa kishika uchumba, Serikali inaendelea na mazungumzo na uchunguzi ambao uliweza kutolewa, kama vile yalivyoweza kutolewa yale maoni na zile kamati mbili teule za Mheshimiwa; Rais ni kwamba yale mashauriano au ushauri uliotolewa wa uchunguzi, uchunguzi unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama itaonekana katika vile vitofali kuna wizi wa dhahabu ulitokea kwa sababu, kulikuwa kuna under declaration. Kama kweli ilitokea ni kwamba wale wa ACACIA wako tayari kuweza kutoa au kulipa fidia zote ambazo wameji-committ na walitoa kishika uchumba cha dola milioni 300, kwa maana ya kwamba waliji-committ kwamba kama kutakuwa na pesa nyingine za kutoa basi wataendelea kufidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ni kwamba maongezi yanaendelea na uchunguzi unaendelea na kama kuna upungufu wowote au kama kuna fedha yoyote ambayo inatakiwa ilipwe katika Halmashauri, kama service levy, na wewe mwenyewe umetaja kwamba kuna bilioni 973 kama kweli ni haki ya Halmashauri haki hiyo italetwa katika halmashauri hiyo. Uchunguzi unaendelea na maongezi yanaendelea. Nashukuru sana.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Msalala hususan wakazi wa Bulyanhulu wamefanyiwa dhuluma nyingi sana na Mgodi wa ACACIA, Bulyanhulu ikiwemo kuondolewa kwenye maeneo yao bila fidia mwaka 1996 na kwa wale wanaopata kazi mgodini kufukuzwa kazi bila kufuata utaratibu, kupata madhara makubwa ya kiafya na hata kusababishiwa vifo; na Serikali ya Awamu ya Tano imesimama kidete kutetea wananchi na kuwaepushia dhuluma hizi. Je, ni hatua gani imefikiwa katika mazungumzo kati ya ACACIA na Serikali kuhusu ulipaji fidia kutokana na dhuluma hizo?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza swali dogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili sekta hii ya madini kwa wachimbaji wadogo wakiwemo wachimbaji wa Jimbo la Mbulu Mjini, ni kwamba wanakosa mitaji, lakini pia uchimbaji wao ni wa kubahatisha. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia fursa za uwezeshaji, lakini pia na vifaa vya kubaini madini yako wapi na njia rahisi ya uchimbaji?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, kwamba, wachimbaji wadogo wanakumbana na tatizo kubwa la kuwa na mitaji midogo. Sisi kama Serikali tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba, wachimbaji wadogo tunakwenda kuwasaidia, ili waweze kupata mitaji ya kuweza kuchimba na waweze kuchimba kwa kupata faida, na sisi kama Serikali tuweze kupata maduhuli na kodi kutokana na uchimbaji huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wachimbaji wadogo wengi wanachimba kwa kubahatisha. Sisi kama Wizara kwa kushirikiana na Geological Survey of Tanzania taasisi ambayo chini ya Wizara ya Madini, tuna mkakati kabambe wa kuhakikisha tunafanya tafiti mbalimbali. Tafiti ambazo zitaonesha ni wapi kuna madini ya kutosha na kuweza kuwapa ushauri wachimbaji wadogo kuchimba maeneo ambayo yana madini ili kuepukana na tatizo la kuchimba kwa kubahatisha. Wanatumia fedha zao za mfukoni, wengine wanauza hadi mali zao, ili waende wakachimbe maeneo ambayo hayajafanyiwa utafiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara tumejipanga vizuri, tunafanya tafiti za kutosha na tutaendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo, ili waweze kuchimba maeneo ambayo yana madini na waweze kuchimba kwa teknolojia nzuri ya kisasa na nyepesi, ili waweze kupata tija na waweze kuendesha maisha yao vizuri zaidi, ahsante.

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Msalala hususan wakazi wa Bulyanhulu wamefanyiwa dhuluma nyingi sana na Mgodi wa ACACIA, Bulyanhulu ikiwemo kuondolewa kwenye maeneo yao bila fidia mwaka 1996 na kwa wale wanaopata kazi mgodini kufukuzwa kazi bila kufuata utaratibu, kupata madhara makubwa ya kiafya na hata kusababishiwa vifo; na Serikali ya Awamu ya Tano imesimama kidete kutetea wananchi na kuwaepushia dhuluma hizi. Je, ni hatua gani imefikiwa katika mazungumzo kati ya ACACIA na Serikali kuhusu ulipaji fidia kutokana na dhuluma hizo?

Supplementary Question 3

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kutokana na swali la kwanza la msingi mazingira hayo pia yanafanana na kule kwetu Geita ambako wananchi wa Geita wamekuwa wakiathirika kwa kiasi kikubwa na shughuli za Mgodi wa Geita Gold. Serikali kipindi cha Waziri Muhongo na Naibu Waziri Kalemani waliunda tume kwenda kuchunguza matatizo hayo kule Geita na kubaini nyumba ambazo zimeathirika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa suala hili litaisha? Kwa sababu, wananchi wanaishi katika maeneo yenye mitetemo, wanaathirika na vumbi, wanapata hata madhara ya kiafya. Ni lini sasa Serikali itasimamia huo Mgodi wa Geita Gold Mine kuhakikisha ya kwamba, inawaondoa wananchi katika maeneo ya Compound na maeneo ya Katoma ili kupisha shughuli za mgodi? Ahsante sana.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, kuna watu ambao wanaishi ndani ya maeneo ambayo ni square kilometer 290,000 ambazo zinamilikiwa na GGM. Kwa mujibu wa sheria ilivyo ni kwamba kuna watu ambao bado wanamiliki zile surface area, yaani kwa maana ya eneo la juu la ardhi, na maeneo ambayo ni ya chini yanamilikiwa na mgodi wa GGM, kwa hiyo, kuna wananchi ambao bado wanaishi maeneo ambayo yako ndani ya leseni ya GGM.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwahi kufika pale mwezi wa pili na nilitoa tamko kwamba kuna Kamati ziliundwa na Waheshimiwa Mawaziri waliotangulia na ilionesha kabisa kwamba kuna watu ambao wameathirika katika maeneo yale. Nikatoa tamko kwamba wale ambao wako ndani ya maeneo ya GGM, GGM kama kampuni ikae nao iwalipe fidia iwaondoe yale maeneo ambayo wale wananchi wanaathirika na mgodi huo.
Vilevile kuna watu ambao wako maeneo ya Katoma, wameathirika na matetemeko kutokana na milipuko inayofanywa na GGM. Kulikuwa kuna taarifa mbili ambazo zilikuwa zimetolewa moja ikiwa ya GST kuangalia ni namna gani yale matetemeko yalikuwa yanaathiri zile nyumba. Majibu yaliyokuwa yanatoka yalikuwa yanakizanzana kwamba kuna wengine walisema milipuko ilisababisha nyufa katika nyumba zile na kuna taarifa nyingine inasema kwamba ile mitetemeko haikusababisha zile nyufa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tumeamua kwa pamoja kwamba wakae waangalie tena upya na vile vile wafanye tathmini ya kutosha kwenye zile nyumba zilizoathirika wawalipe wale wananchi. Ikiwezekana wale wananchi walimo ndani ya hiyo leseni ya GGM waondolewe, wawalipe fidia, ikiwemo na watu wa Nyakabare, walipwe fidia waondoke yale maeneo ya uchimbaji. Kwa hiyo, hiyo tumeshawapa GGM na tunaendelea na maongezi na tunaendele na mikakati kuangalia namna gani ya kuweza kuwalipa fidia wananchi hawa. Ahsante sana.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Msalala hususan wakazi wa Bulyanhulu wamefanyiwa dhuluma nyingi sana na Mgodi wa ACACIA, Bulyanhulu ikiwemo kuondolewa kwenye maeneo yao bila fidia mwaka 1996 na kwa wale wanaopata kazi mgodini kufukuzwa kazi bila kufuata utaratibu, kupata madhara makubwa ya kiafya na hata kusababishiwa vifo; na Serikali ya Awamu ya Tano imesimama kidete kutetea wananchi na kuwaepushia dhuluma hizi. Je, ni hatua gani imefikiwa katika mazungumzo kati ya ACACIA na Serikali kuhusu ulipaji fidia kutokana na dhuluma hizo?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa Halmashauri ya Geita inaudai mgodi wa GGM zaidi ya dola milioni 12; tumekaa tukakubaliana watulipe kwa awamu. Awamu ya kwanza ilikuwa itekelezwe mwezi wa pili, lakini utekelezaji huo haujafanyika na Halmashauri haina nguvu tena ya kuudai Mgodi wa GGM. Je, Wizara inaisaidiaje Halmashauri ya Geita ili tuweze kulipwa pesa hizo?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Halmashauri ya Geita inaudai GGM service levy. Tulitoa ushauri kama Wizara kwamba wakae kwa pamoja na waangalie ni namna gani Kampuni ya GGM inaweza ikawalipa wale Halmashauri ya Geita, yaani wakae kwa pamoja waelewane ili wangalie namna bora ya kuweza kulipa kidogo kidogo deni hilo na wameshakaa na nilipokwenda mara ya mwisho mwezi wa pili walisema kwamba wanakwenda kukaa na Halmashauri, ili waweze kusaini memorandum of understanding, namna ya kuweza kulipa deni hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama hawajalipwa mpaka sasahivi, naomba nishirikiane na Mbunge kwamba nifuatilie. Sisi kama Wizara tuko pamoja tutahakikisha kwamba haki ya Halmashauri ya Geita italipwa kama inavyostahili. Ahsante sana.