Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi pamoja na majibu ya kukatisha tamaa ya Mheshimiwa Waziri naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza. (Kicheko)
Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba barabara hii ni muhimu sana katika eneo hili na ametueleza kwamba katika bajeti ya mwaka 2018/2019 wametenga kujenga kilometa tano tu katika barabara ambayo anasema ina urefu wa zaidi ya kilometa tisini na kitu.
Je, Mheshimiwa Waziri atakubaliana nami kwamba kuendelea kutenga kilometa tano zitawafanya wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini na Mkoa wa Singida na Manyara kusubiri ujenzi huu kwa zaidi ya miaka 19 ijayo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii imekuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na imetusumbua sana wakati wa uchaguzi kila mara.
Je, Serikali sasa ipo tayari kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kilometa 15 zilizosalia katika kufika katika mji wa Ilongero ili kusudi kuwaondolea walau kuwapunguzia wananchi adha hii wanayoipata kwa sasa? Ahsante sana.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara au ujenzi wowote ule unahitaji kupata pesa ya kutosha. Ninamwomba tu Mheshimiwa Mbunge aelewe kwamba nchi yetu ni kubwa na kila sehemu inahitaji ipate huduma kutokana na mfuko na kipato cha Serikali kilichopo na sio kwamba tuna-concentrate na barabara moja tu. Tunakiri kwamba kweli barabara ile ni muhimu lakini Tanzania ni kubwa na yote inahitaji pesa kutoka Wizara hiyo hiyo moja.
Kwa hiyo, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kupata kilometa tano ni mwanzo, lakini pesa itakapopatikana tunaweza tukajenga hata kilometa nyingi lakini angalau hizo tano zilizopatikana ni muhimu azipokee na ashukuru kwamba tunafanya jitihada kama Serikali ya Chama cha Mapinduzi kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto za barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ni kweli barabara hii ipo kwenye ahadi na hata kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi barabara hii inasomeka, lakini siyo hiyo tu peke yake ni barabara ambayo inatoka kuanzia Karatu ambayo ipo Arusha, inapitia Mbulu inakuja mpaka hapo tunapopazungumza Haydom inakwenda mpaka Simiyu. Pesa zitakapopatikana na tukumbuke kwamba tuna ahadi mpaka mwaka 2020, pesa itakapopatikana hizi barabara zote zitajengwa kwa kiwango cha lami. Tuna nia nzuri kama Serikali kuhakikisha kwamba Wananchi wanapata huduma nzuri za barabara.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 2

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante, wananchi wa Busekelo kwa kushirikiana na mimi nikiwa Mbunge wao tumeamua kulima barabara inayounganisha Mkoa wa Njombe na Mkoa Mbeya kwa kutumia zana za jembe la mkono.
Je, ni lini Serikali itatupa support ili tuweze kukamilisha barabara hii ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Busekelo na Makete na ukizingatia kwamba…

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana kwa jinsi anavyopigania wananchi wa jimbo la Busokelo katika kuhakikisha kwamba wanapata huduma nzuri za barabara. Ni kweli nakiri kwamba nilimwona juzi kwenye vyombo vya habari akihamasisha na kufanya kazi sambamba na wananchi kuhakikisha kwamba barabara inapitika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii imo kwenye Ilani, Serikali inalitambua na tumeona jitihada za Mbunge na kwenye bajeti yetu ya mwaka huu imesomeka kwenye hatua za upembuzi yakinifu na details design. Kwa hiyo, tutalishughulia.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa. Na mimi nilitaka niulize kuhusu barabara ya kutoka Mtwara – Pachani - Mkongo – Gulioni – Ligera - Lusewa inaenda Magazine - Likusenguse hadi Tunduru ambayo ina urefu wa kilometa 300 iliyoahidiwa na Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Awamu ya Nne, ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kipande hicho cha barabara kimekuwa kikisumbua kwa muda mrefu na kwa kweli tumekuwa tukipata mawasiliano mazuri sana na Mbunge akiwa anatetea kipande hicho cha barabara. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo suala tunalo na tunalifanyia kazi; tunawasiliana mara kwa mara na Meneja wa TANROADS wa Mkoa kuhakikisha kwamba inaingizwa kwenye utaratibu ambapo tutaanza kuifanyia matengenezo makubwa. Ahsante.

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 4

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nichukue nafasi hii kumwuliza swali dogo Mheshimiwa Naibu Waziri; ni nini kauli ya Serikali juu ya kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Masasi - Nachingwea - Nanganga?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli ya Serikali ni kwamba pesa inatafutwa, kwa sababu hatua za awali za ujenzi wa kipande hicho cha barabara zilishaandaliwa na zinatekelezwa. Pesa itakapopatikana, barabara hiyo itaingizwa kwenye mpango ianze kutengenezwa kwa kiwango cha lami.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 5

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa kwa mujibu wa taarifa ya Serikali ya mwezi Desemba, 2017 kuhusu barabara ya Nyakahura - Murugarama ilieleza kwamba iko kwenye hatua ya mchakato wa manunuzi, ni lini sasa mchakato huo wa manunuzi utakamilika ili barabara hii yenye urefu wa kilometa 85 iweze kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, mara baada ya kumpata mkandarasi shughuli za ujenzi wa kipande hicho cha barabara zitaanza mara moja.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 6

MHE. DANIEL N. NSWAZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo tu; barabara ya Kidahwe – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi, ni barabara ya muda mrefu sana; na kipande cha Kidahwe – Kasulu kina mkandarasi, lakini mkandarasi huyo amekuwa kazini kwa miaka kumi akijenga kilometa 50. Swali langu kwa Waziri ni kwamba ni kwa nini mkandarasi huyu halipwi madeni yake ili barabara hiyo ikamilike? Kwa nini barabara ya kilometa 50/0 aijenge kwa miaka 10 wakati hana fedha? Barabara hii mkandarasi yupo kwenye site.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kipande cha kutoka Kidahwe kuja mpaka Kasulu kina mkandarasi. Nimhakikishie Mheshimiwa Nsanzugwanko kwamba mkandarasi huyo ameshalipwa malipo yake, lakini sasa hivi kuna mvua nyingi sana zinaendelea pale Mkoani Kigoma, tena mkoa mzima na hivyo kusababisha ucheleweshaji kidogo wa kumalizia. Kuna hatua za awali ambazo zimeshaendelea na yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge anajua, kipande cha kilometa karibu 20 kitawekwa lami mara mvua zitakapopungua. Kwa sababu mambo mengine ni ya kitaalam, huwezi kuweka lami wakati kuna mvua inanyesha kila siku. Mvua za Mkoa wa Kigoma bahati nzuri anazifahamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kipande cha kutoka Kibondo mpaka Nyakanazi kupitia Kakonko na kutoka Kasulu, tender itatangazwa hivi punde. Ahsante sana.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Barabara ya Singida - Ilongero - Mintiko hadi Haydom inayounganisha Mikoa ya Singida na Manyara ni kiungo muhimu katika kusafirisha mazao ya wakulima na bidhaa za wafanyabiashara na inapita katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom ambayo wananchi hufuata huduma kwa kukosa Hospitali ya Serikali katika Halmashauri. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kunusuru maisha ya wananchi wa Singida Kaskazini?

Supplementary Question 7

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Mbozi na Wilaya ya Songwe hazijaunganishwa kwa barabara licha ya kwamba Wilaya ya Mbozi ni Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe, lakini wananchi wa kutoka Wilaya ya Songwe kwenda Makao Makuu ya Mkoa ambayo yako Mbozi wanalazimika kupita mkoa mwingine ambao ni Mkoa wa Mbeya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize sasa, ni lini barabara ya kutoka Kata ya Magamba ambayo inapitia Kata ya Magamba Wilaya ya Mbozi; na hili niliweke vizuri, Magamba hiyo inapatikana Songwe, lakini Magamba nyingine pia inapatikana Mbozi. Kuna uwezekano wa kutengeneza njia kwenda Makao Makuu ya Mkoa kutoka Songwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini barabara hii itatengenezwa licha ya kwamba Naibu Waziri wa Ujenzi alisema kwamba angeweza kuja Mbozi kuangalia uwezekano na hadi sasa amewadanganya wananchi wa Mbozi, hajafika. Naomba sasa jibu la Serikali.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaunga mkono kabisa mambo ambayo yanaendelea hapa Bungeni, kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge katika kuuliza maswali. Nadhani wakati mwingine ni vizuri tuwe tunawasiliana kimkoa kwanza kujua status ya mambo ambayo tunakuja kuyauliza huku Bungeni. Siyo kitu kibaya wananchi wakifahamu kwamba umekuja kuuliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba kuna taratibu za ujenzi wa barabara ambazo zinaendelea kupitia TANROADS Mkoa wa Songwe. Ninaamini kama Mbunge angewasiliana na Meneja wa TANROADS Mkoa, asingekuja kuuliza swali kama alilouliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Haonga kwamba detailed design tayari, sasa hivi tunafanya utaratibu baada ya kupitia hizo details kuanza kutafuta Mkandarasi wa kujenga hicho kipande cha barabara kutoka Mbozi kwenda Songwe. (Makofi)