Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENAN aliuliza:- Mara kwa mara Serikali imekuwa ikishindwa kesi mbalimbali Mahakamani:- Je, Serikali imefanya uchunguzi na kujua sababu za kushindwa kesi mara kwa mara?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa, Halmashauri nyingi nchini zinapopelekwa Mahakamani zinashindwa kesi, hali inayoonyesha ni jinsi gani Wanasheria wetu wa Halmashauri wanashindwa kuwashauri vizuri Wakuu wa Idara na kusababisha hasara kwenye Halmashauri zetu. Serikali ina utaratibu gani wa kufuatilia weledi wa Wanasheria wetu kwenye Halmashauri ili kuepusha hasara zinazotokea kwenye Halmashauri zetu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; katika kesi za usuluhishi nje ya nchi napenda kufahamu, ni kesi ngapi tumeshinda kama Serikali na zipi tumeshindwa ikiwepo ya DOWANS, IPTL na nyinginezo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anauliza namna ambavyo Serikali inaweza kufuatilia weledi wa Mawakili katika Halmashauri ambao wamekuwa wakisababisha hasara kwa Halmashauri kushindwa kesi nyingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ya kwamba Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, imekuwa ikiingilia katika baadhi ya mambo ambayo maslahi ya Serikali yanakuwa yako hatarini na pia katika ushauri ambao tumeuweka hapa tumeshauri taasisi hizi zikiwa zina kesi kubwa ambazo zinahitaji intervention ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa-consult mapema, ili wapate ushauri ambao unaweza kusaidia kulinda maslahi ya Serikali. Katika swali aliloliuliza sasa, nitoe tu rai kwa Wanasheria wote, hasa wale Mawakili katika Taasisi za Serikali katika kila Halmashauri kuendelea kufanya kazi hizi kwa weledi mkubwa na ufanisi, ili kulinda maslahi ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itaendelea kuwajengea uwezo Mawakili mbalimbali na pia Halmashauri zitenge fedha kwa ajili ya kuwajengea uwezo Wanasheria wao, ili pindi wanapokwenda kulinda maslahi ya Serikali, basi wafanye kazi hiyo katika weledi na ufanisi mkubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la kesi ngapi tumeshinda za usuluhishi; Mheshimiwa Mbunge aniruhusu tu nikachukue takwimu na nikishazipata nitampatia ili na yeye aone ni kwa kiwango gani Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imefanya kazi hii ya kulinda maslahi ya nchi yetu. (Makofi)