Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Kutokana na wananchi wa vijijini kuwa na uelewa mdogo wa masuala ya sheria na haki zao, Watendaji wa Vijiji na wa Kata wakishirikiana na Mahakama za Mwanzo na Mabaraza ya Ardhi huwaonea na kuwadhulumu kwa kuwabambikizia kesi na kuwanyang’anya ardhi:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kukomesha tabia hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imekiri kwamba kuna dhuluma sana miongoni mwa wananchi wetu, ni lini sasa Serikali itachukua hatua kwa sababu kuna matukio mengi sana ambayo siwezi kuyaorodhesha hapa, yako kule kwenye Jimbo la Igunga ambapo wananchi wengi sana wamedhulumiwa. Ni lini sasa Serikali itachukua hatua hizo badala ya kutoa onyo tu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kwenye Kijiji cha Lugubu, kijiji kiliamua kutenga eneo moja kuwa eneo la hifadhi, lakini kwa bahati mbaya baadhi ya watendaji waliwaruhusu wananchi wawili waingie kwenye hilo eneo na kukazuka mgogoro mkubwa sana wa ardhi ambao Mahakama ya Ardhi na Mahakama ya Mwanzo wameshindwa kuurekebisha huo mgogoro. Je, ni lini sasa Serikali itatusaidia jambo hili ili tuweze kutenga eneo katika Kijiji hicho cha Lugubu? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba lini tutaanza kuchukua hatua naomba nikuhakikishie kwanza naomba ikiwezekana atupe orodha sasa hivi, kama kuna watu wa aina hiyo basi tuanze kuelekeza mara moja jinsi gani watu ambao wanakwamisha haki za watu ambao wanadhulumu kwa makusudi na wao wamepewa dhamana tuweze kuwachukulia hatua. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nimsihi kama ana orodha sasa hivi naomba aikabidhi kwangu tuweze kuifanyia kazi haraka iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine katika Kijiji cha Lugugu ambalo amezungumza kwamba kuna eneo la kijiji limetengwa lakini kuna watu wawili wamekabidhiwa eneo hilo, eneo ni mali ya kijiji, kwa kweli inatia huzuni. Katika hili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutalifanyia kazi. Naomba nimwelekeze Mkuu wetu wa Wilaya ya Igunga aweze kufanyia uchunguzi wa haraka katika eneo hilo kipi kinachojili ili mradi mwisho wa siku haki ya wananchi iweze kupatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hilo halitavumilika hata mara moja na kwa vile nimekubaliana na Wabunge wa Mkoa wa Tabora kwamba nitakwenda Mkoa wa Tabora lakini nitakuwa na interest ya kufika eneo hilo kwenda kujua ni ubadhirifu gani unaofanyika ambao unanyima haki za watu, lengo kubwa tuhakikishe wananchi wanapata huduma inayotakiwa. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Kutokana na wananchi wa vijijini kuwa na uelewa mdogo wa masuala ya sheria na haki zao, Watendaji wa Vijiji na wa Kata wakishirikiana na Mahakama za Mwanzo na Mabaraza ya Ardhi huwaonea na kuwadhulumu kwa kuwabambikizia kesi na kuwanyang’anya ardhi:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kukomesha tabia hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa kukosa fedha za kuendeshea shughuli za Mabaraza ya Ardhi ya Kata ni kichocheo kikubwa sana cha rushwa kinachopelekea wananchi wengi kunyimwa haki zao za msingi. Sasa Serikali haioni sababu na umuhimu sasa itoe ruzuku kwa Mabaraza haya ili yaweze kuendesha shughuli zake na kuondoa uwezekano wa kuchukua rushwa? Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa kesi kubwa nyingi sana kuja kuziangalia hata maamuzi mengine yanakuwa yanasababishwa na baadhi ya wale ambao wako katika Mabaraza ya Kata. Wakati mwingine inaonekana kwamba mtu aliyenacho ndiyo huyo ambaye haki inamwendea, hili ndiyo maana Serikali ilikuwa inafanya tathimini kwa kina sana kuangalia nini kifanyike katika suala zima katika uendeshaji wa Baraza la Kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Mbunge tunalichukua lakini kuna mchakato mpana tunaufanya kuona jinsi gani tutaboresha haya Mabaraza ya Kata yaweze kufanya kazi vizuri zaidi kulinganisha na hivi sasa kwa sababu haki nyingi za watu zinapotea kwa sababu haki haisimamiwi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wazo hili tunalichukua, lakini tunajumuisha miongoni mwa mambo ya kufanya restructuring tuifanyeje, lengo kubwa la Mabaraza hayo yaweze kufanya vizuri, kwa hiyo, ni wazo zuri tunalichukua kama Serikali kulifanyia kazi kwa mpango.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Kutokana na wananchi wa vijijini kuwa na uelewa mdogo wa masuala ya sheria na haki zao, Watendaji wa Vijiji na wa Kata wakishirikiana na Mahakama za Mwanzo na Mabaraza ya Ardhi huwaonea na kuwadhulumu kwa kuwabambikizia kesi na kuwanyang’anya ardhi:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kukomesha tabia hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kama alivyojibu mjibu swali, kwa kuwa hawa Wazee wa Mahakama wanalipwa nafikiri Sh.5,000/= au Sh.7000/=. Je, huo mchakato wanaoufanya wanajiandaa kuongeza kiwango cha hawa Wazee kwa sababu ni kazi ya hiyari? Isije kuwa wanashindwa kwenda Mahakamani ndiyo maana haki inachelewa kupatikana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema hapa Mheshimiwa Bulembo kwamba tunachokifanya ni kufanya tathmini ya kina jinsi gani tutafanya kuhakikisha wananchi wanapata haki. Siwezi kusema kwamba kiwango hiki kitaongezeka kwa sababu kuna mambo mengi ndani yake yanaendelea hapa, isipokuwa kwamba tuamini Serikali inafanya kazi na mwisho wa siku ni kwamba miongoni mwa kuondoa kero nyingi za wananchi ni kushughulikia Mabaraza ya Kata, ili kulinda haki za watu kwa kuyashughulikia na kuyaunda vizuri Mabaraza ya Kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali inafanya kazi hii hatima yake itakapofika, basi tutapata mwelekeo maalum wa Serikali wa jinsi gani jambo hili tunaenda kuli- handle vizuri kwa maslahi mapana ya wananchi.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Kutokana na wananchi wa vijijini kuwa na uelewa mdogo wa masuala ya sheria na haki zao, Watendaji wa Vijiji na wa Kata wakishirikiana na Mahakama za Mwanzo na Mabaraza ya Ardhi huwaonea na kuwadhulumu kwa kuwabambikizia kesi na kuwanyang’anya ardhi:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kukomesha tabia hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa, sababu mojawapo ya utendaji mbovu wa Mabaraza ya Ardhi ni kwa sababu hawana weledi na mafunzo ya kutosha; na kwa kuwa pia Halmashauri ndiyo yenye jukumu la kuwapa mafunzo Wajumbe wa Mabaraza ya Ardhi na Halmashauri hizi hazina pesa, Serikali inaonaje kupiga marufuku Mabaraza ya Ardhi ambayo hayajapata mafunzo ya kutosha kufanya kazi yake mpaka hapo yanapokuwa yamepata mafunzo ya kutosha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kupiga marufuku kwamba Mabaraza yasifanye kazi jambo hilo naomba niseme kwamba hatuwezi kupiga marufuku hapa, isipokuwa tunachotaka kufanya ni kwamba niwasihi hasa Wakurugenzi wa Halmashauri zetu zote 185 ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pale inapobainika kwamba kuna Mabaraza ya Kata ambayo uelewa wao ni mdogo katika utaratibu tunaokwenda nao katika kuyaboresha kipindi hiki cha mpito, lazima wahakikishe wanatumia ile staffing yao iliyokuwa katika Halmashauri kuona watafanyaje kuhusu capacity building kwa watu hawa, lengo kubwa waweze kutoa haki stahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni hoja ya msingi, kwa hiyo, hatuwezi kusitisha hivi sasa, lakini tutaendelea kuwasihi Wakurugenzi wetu wa Halmashauri zetu wafanye capacity building kwa kushirikiana na Wanasheria tuliokuwa nao, lengo kubwa likiwa, Mabaraza haya yaweze kufanya kazi kwa mujibu wa sheria.