Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 55 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 453 2017-06-28

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:-
Kutokana na wananchi wa vijijini kuwa na uelewa mdogo wa masuala ya sheria na haki zao, Watendaji wa Vijiji na wa Kata wakishirikiana na Mahakama za Mwanzo na Mabaraza ya Ardhi huwaonea na kuwadhulumu kwa kuwabambikizia kesi na kuwanyang’anya ardhi:-
Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kukomesha tabia hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Dalaly Peter Kafumu, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba yapo malalamiko dhidi ya baadhi ya Watendaji wa Kata na Vijiji ambao wamekuwa wakilalamikiwa na viongozi na wananchi kuwabambikizia kesi na kushirikiana na Mahakama za Mwanzo na Mabaraza ya Ardhi kuwaonea na kuwadhulumu ardhi wananchi hao kwa kuwanyang’anya ardhi yao. Serikali inakemea vikali tabia ya baadhi ya watumishi wa umma wasio waaminifu na ambao wanakiuka maadili ya utumishi wa umma.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukomesha tabia hii, Serikali inaelekeza kwa viongozi na watendaji mambo yafuatayo ya kuzingatia:-
• Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wahakikishe wanasimamia uzingatiaji wa maadili ya watendaji walio chini yao.
• Watendaji wote katika ngazi zote za mamlaka za Serikali za Mitaa wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu, miiko na maadili katika utekelezaji wa majukumu yao.
• Serikali haitasita kumchukulia hatua Mtendaji yeyote atakayekiuka sheria, kanuni, taratibu na maadili ya kazi yake, ikiwemo kujihusisha na tabia ya ubambikiziaji kesi wananchi na kuwanyang’anya ardhi;
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuhakikisha inasimamia kikamilifu maadili ya watumishi wa umma ili kuongeza nidhamu katika utumishi wa umma na haitasita kuchukua hatua mara moja dhidi ya Mtendaji yeyote wa Kata au Kijiji atakayethibitika kutumia vibaya madaraka yake ikiwemo kubambikia kesi wananchi kwa lengo la kuwanyang’anya ardhi. Nitoe wito kwa viongozi na wananchi wote nchini kuhakikisha wanafichua utendaji na watumishi wa umma wenye tabia kama hii ili waweze uchukuliwa hatua stahiki.