Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:- (a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu? (b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, siridhiki kabisa na majibu aliyotoa Mheshimiwa Naibu Waziri, na huu ndio mzaha ambao hatupendi Wabunge. Milioni 20 mimi ninazo mfukoni hapa, si ningetengeza bwawa hilo? Halitengelezeki kwa milioni 20 bwawa hilo, Bwawa kubwa na limepasuka. Nataka kujua na alisema kwamba itatokana na ruzuku, nani anatoa ruzuku, hatujui; lakini hela zinakwenda kwa nani, hatujui; mkandarasi nani atafanya hiyo kazi hatujui, jibu hili si sahihi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki tena kuomba mwongozo baadaye lakini ningependa Waziri anijibu vizuri, kwamba hizo hela zitatoka wapi na hela hizo hazitoshi, lakini je, lini hela zitapatikana? Hiloni swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tangu mwaka 2014/2015, 2016/2017, leo miaka mingapi? Barabara imejaa miti iliyoota, nani atatengeneza hiyo barabara ya kwenda kwenye bwawa kwa sababu haipitiki? Nataka kujua pia je, barabara ile itatengenezwa na nani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu milioni ishirini; mara nyingi kila mtu ana taaluma yake. Maana yake ma-engineer kama wamefanya assessment; kwa sababu ni ile sehemu iliyobomoka tu. Kama Mbunge anahisi kama shilingi milioni ishirini haitoshi; katika hili naomba niseme kwamba; kwa sababu bwawa limevunjika katika spillways; ngoja tupeleke hizo fedha halafu tuone nini kitaendea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapofanya assessment; kama mtaalam wa maji, mabwawa, engineer amefanya assessment na amesema ni milioni ishirini, lakini Mheshimiwa Mbunge anasema haitoshi, aah, tutaangalia maana huyo mtu inawezekana qualifications zake hazimtoshi kukaa katika nafasi hiyo, ndiyo maana ameleta assessment ya milioni ishirini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili maana yake si kwa sababu yuko Jafo hapa; kwa sababu kuna mtu alifanya designing na assessment ya bwawa lilivyopasuka na amesema milioni ishirini. Isipotosha maana yake watu hawa ndio watakaokuwa wanakwamisha shughuli za maendeleo katika maeneo yetu, hatutaweza kuvumilia. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwa sababu nina safari ya kwenda Kaliua na Urambo nitapita kwenda kutembelea bwawa hilo na kuangalia hali halisi ikoje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini fedha hizi zitatoka katika Local Government Capital Development Grant kutoka TAMISEMI, naomba asihofu fedha hizo zitakwenda. Kuhusu suala la barabara kufika katika eneo lile naomba niseme kwamba hiki ni kipaumbele cha Halmashauri yenyewe kadri inavyosema kwamba bajeti yake inajenga barabara katika eneo gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu naamini kwamba tutafika site tutakwenda kuiona hiyo barabara, basi waweke kipaumbele kama barabara hiyo ambayo haipo katika mpango lazima iwekwe katika mpango ili wananchi waweze kufika katika eneo hilo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:- (a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu? (b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo tu la nyongeza. Matatizo yaliyoko huko Uyui yapo pia katika Jimbo la Manyoni Magharibi. Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kuna mabwawa madogo yale malambo madogo ambayo yamepasuka na mengine yamefukiwa na maji likiwemo la Kaskasi stesheni, Mkalamani Itigi Majengo, pamoja na la Muhanga. Je, Serikali iko tayari na sisi kutusaidia fedha kidogo katika Mfuko huo ili na sisi kama halmashauri tuweze kurekebisha mabwawa haya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge ame-pose hilo swali hapa sasa hivi na hatujui kwamba mabwawa hayo assessment imefanyika na inahitaji gharama kiasi gani na hatujui kama Halmashauri imeweka kipaumbele gani katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu kwamba kwa sababu suala la mabwawa hayo ni jambo la msingi; naomba tuwaagize wenzetu wa Halmashauri ya Itigi, kwamba sasa wataalam wa maji waweze kwenda katika eneo hilo wafanye tathmini ya mabwawa hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwa sababu mabwawa haya yakijengwa yataisaidia jamiii katika eneo letu; tujue kwamba kama Serikali tunajipanga vipi kurekebisha mabwawa hayo mara baada ya kupata bajeti halisi na tuweze kuliweka katika mipango ya maendeleo ya bajeti katika Halmashauri ya Itigi.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:- (a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu? (b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Matatizo yaliyopo Uyui kwenye miradi inayosimamiwa na TASAF na TAMISEMI yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika Jimbo la Ndanda hasa kwenye Kata ya Mwena.
Mheshimiwa Mwenyekit, kwenye hii TAMISEMI phase III ambayo imekuwa ikishirikisha wananchi. Kuna miradi pale ya mabomba ambayo Mheshimiwa Diwani kwa kushirikiana na watendaji wamekuwa hawatekelezi wajibu wao; kwa maana ya thamani ya pesa haionekani kwenye miradi. Sasa Mheshimiwa Waziri tunaomba atuleze badala ya kusubiri mpaka haya mambo yaharibike kabisa ndipo Wizara yake ikachukue hatua, je, hawaoni kuna haja ya kufuatilia utoaji na matumizi ya pesa ya TASAF katika maeneo mbalimbali kadiri siku zinavyokwenda?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme wazi kwamba jambo la kusimamia fedha (value for money) katika maeneo yetu naomba tulipe kipaumbele sana. Mheshimiwa Cecil nakumbuka tumetembelea mpaka kwenye bwawa lake pale chini. Kama fedha lakini usimamizi si mzuri na kama fedha imekwenda wengine wanatengeneza caucus kule kwa ajili ya kula ile fedha, jambo hilo halikubaliki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wao ni Wajumbe wa Kamati ya Fedha, wasikubali kupitisha mradi wa aina yoyote katika site na Majimbo yao ambayo wanaona katika njia moja au nyingine, mradi huu baadhi ya watu wanahujumu kwa makusudi. Tukifanya hivi ndipo tutalinda fedha hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Masasi, kwamba aangalie kwanza nini kilichotokea katika mradi huo ambao tunasema kwamba lengo ni kuweza kuwasaidia wananchi halafu tupate taarifa. Nitaenda kufanya follow up ya haraka ili fedha zinapokwenda kule site lazima fedha zile ziweze kuleta matunda makubwa sana kwa manufaa ya wananchi.

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:- (a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu? (b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba niulize swali la nyongeza. Kutokana na mvua zilizonyesha, barabara yetu ya kutoka Mbwela kwenda Muholo imeharibika zaidi. Je, Wizara yake ina mkakati gani wa kutukarabatia barabara hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mheshimiwa Ungando amehamisha goli lakini ngoja nimjibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, anachosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, ile barabara kwanza ni korofi na Mheshimiwa Mbunge anakumbuka siku ile tulikuwa delta mpaka usiku saa mbili ndipo tulirudi kwa kuwa barabara iliharibika sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tumepitisha fedha za barabara za vikwazo na barabara hiyo tumeiweka basi nimhakikishie Mheshimiwa Ungando kwamba kwa sababu bajeti tumeipitisha jana na yeye amepiga kura ya ndiyo, bajeti hii sasa itakapoanza kufanya kazi katika eneo lake lile tutalipa kipaumbele ili barabara ile tuirekebishe sambamba na ujenzi wa yale madaraja ambayo yanakwamisha sana kuwapitisha wananchi wa Kibiti.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:- (a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu? (b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Supplementary Question 5

MHE. WILLY Q. QAMBALO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Tatizo la mabwawa kupasuka lililopo Tabora Kaskazini linafanana kabisa na matatizo tuliyonayo kule Karatu. Bwawa la Bashay lililopo nje kidogo ya Mji wa Karatu lilikuwa chanzo muhimu sana cha maji kwa wakazi wa Kata ya Qurus hadi pale lilipopasuka wakati wa zile mvua za el- nino. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati bwawa hilo ili wananchi wa Gongali, Bashay na Qurus waweze kupata huduma hiyo muhimu ya maji?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS – TAMISEMI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema Mipango yote ya Serikali lazima ianze katika Halmashauri zetu, tufanye needs assessment, tubainishe na tuweke katika mipango ya Serikali. Hata hivyo, imeonekana kwamba katika maeneo mengi mabwawa haya mengi sana yanapasuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwasihi hasa Waheshimiwa Wabunge tunaposimama katika maeneo yetu, japo kuwa si wataalam sana katika maeneo hayo lakini tuna haki ile miradi wakati inajengwa tuisimamie kwa karibu kwa sababu wakati mwingine wakandarasi wanapojenga ile embarkment haishindiliwi vizuri na hatimaye lile tuta linapasuka au spillway ya kupitisha utoro wa maji haiwi vizuri na mwisho wa siku maji yanafurika na bwawa linapasuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa ndugu yangu Mbunge wa Karatu jambo hili tumesema kwamba kama Serikali tumelisikia, lakini naomba nielekeze kama nilivyotoa maelekezo katika maeneo mengine, kule Halmashauri ya Karatu tuweke kipaumbele cha kufanya ukarabati wa bwawa hili ambalo linasaidia wananchi ili hatimaye tutenge fedha katika bajeti ile ili tuweze kurekebisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, naomba niseme kwamba tumelisikia, tumelipokea na kama Serikali tunajua kuna wananchi wetu huko wanapata shida kwa sababu bwawa limepasuka.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:- (a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu? (b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Supplementary Question 6

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa mabwawa yameendelea kupasuka katika nchi hii na kwa kuwa katika Wilaya ya Monduli, Kata ya Esilalei, bwawa la Josho na Oltukai, tulishaleta mpaka kwa Waziri Mkuu kuomba Serikali iweze kukarabati mabwawa yaliyopasuka mwaka 2015. Je, ni lini Serikali itakuja kukarabati mabwawa haya ambayo Serikali ilishahaidi kuyakarabati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ukiangalia kila mtu anazungumza kuhusu bwawa lililopasuka na nimetoa maangalizo, kwamba mabwawa haya yanapasuka huenda kandarasi haikusimamiwa vizuri, ile spillway (utoro wa maji) haukuwa vizuri au ile embarkment haikushindiliwa vizuri au utaalam wenyewe uliotumika huenda haukutumika sawasawa; kwa hiyo hapa inawezekana kila mtu atazungumza bwawa lake limepasuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri zote wafanye tathmini ya mabwawa yote yaliyopasuka ili Serikali tuone kwamba tuna tatizo kiasi gani tuweze kulipangia mpango na tulirekebishe na hatimaye mabwawa haya yawasaidie wananchi katika mifugo, maji ya kunywa na matumizi mengine. (Makofi)