Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 427 2017-06-21

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-
Katika Kijiji cha Majengo, Kata ya Ikongolo, TASAF ilijenga bwawa kubwa la kukinga maji ya mvua kwa madhumuni ya umwagiliaji na matumizi ya vijiji vyote vinne vya Kata ya Ikongolo, lakini bwawa hili lilivuna maji kwa mwaka mmoja tu na kisha kwa masikitiko makubwa bwawa hilo lilipasuka kingo yake moja na maji yote yakatoka:-
(a) Je, wataalam wa Serikali wamegundua ni kwa nini bwawa hilo limepasuka kingo yake kuu?
(b) Kwa vile bwawa hilo lilileta shughuli nyingi za kiuchumi kwa wananchi kwa kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini Serikali itaanza harakati za kuziba mpasuko uliotokea katika kingo za bwawa ili wananchi waendeleze shughuli zilizosimama?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora kaskazini lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, kubomoka kwa tuta (Embarkment) la Bwawa karibu na sehemu ya kupumulia (spillways) katika Kijiji cha Majengo kulitokana na athari za mvua nyingi zilizonyesha msimu wa mwaka 2013/2014.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu wa bwawa hilo, Serikali imeidhinisha shilingi milioni ishirini kwa ajili ya ukarabati wa bwawa hilo ambao utahusisha ujenzi wa njia ya kuchepusha maji (spillways). Fedha hizo zitatokana na ruzuku ya maendeleo kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa.