Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Mkomazi Game Reserve (sasa Hifadhi ya Taifa Mkomazi) ilianzishwa kabla ya Uhuru wakati tukiwa na idadi ndogo ya watu na mifugo. Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kusogeza mipaka ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi ili wananchi wa Kata za Visiwani, Mji Mdogo wa Same na Vumari wapate maeneo ya kuishi, kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niulize maswali mawwili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi wangu wa Kata za Kisiwani, Vumari na Mji Mdogo wa Same wamebanwa sana na Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi; na kwa kuwa Mwenyezi Mungu wakati anaumba dunia alimuumba binadamu akamwambia atawale viumbe vyote viishivyo kwenye maji na kwenye nchi kavu; na kwa kuwa wakati wa uhuru tulikuwa na idadi ya watu milioni 10.3 na sasa hivi tuko takribani milioni 50, tulikuwa na ng’ombe milioni nane sasa hivi milioni 28; tulikuwa na mbuzi milioni 4.4 sasa hivi ni milioni 16.6; tulikuwa na kondoo milioni tatu na sasa hivi ni milioni tano, tulikuwa na nguruwe 22,000 sasa hivi ni milioni mbili, astaghfilillah nimetaja nguruwe wakati ni mwezi wa Ramadhani, mnisamehe sana. (Kicheko)

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza je, Wizara ya Maliasili na Utalii iko tayari kushirikiana na Wizara ya Kilimo, TAMISEMI pamoja Ardhi ili waweze kutathmini eneo na idadi ya watu pamoja na mifugo wanayofuga ili kusudi kama kuna uwezekano maeneo ya hifadhi za misitu pamoja na Hifadhi za Wanyamapori zipunguzwe ili binadamu waweze kupata maeneo ya makazi pamoja na mifugo na kilimo?
Swali la pili, kwa kuwa Botswana, Afrika ya Kusini na Namibia wameweza kuzuia wanyamapori kutoka kwenye mapori kwenda kwa binadamu ama kwenye wanyama wanaofugwa, je, Serikali iko tayari sasa kuandaa mpango rasmi wa kuweka fence ili wanyamapori wasiweze kwenda kwenye makazi ya watu kuwasumbua na kuwaletea madhara ikiwa ni pamoja na vifo? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza Mheshimiwa Mbunge anazungumzia upungufu wa ardhi kwa ajili ya matumizi ya kibinadamu hasa kwa ajili ya faida ya kiuchumi na kijamii, akihusisha na uhaba au upungufu wa rasilimali ardhi kwa ajili ya shughuli hizo zinazotokana na ongezeko la binadamu na wanyama kama ambavyo amewataja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi Serikali inatambua na kwa kweli ni dhamira ya Serikali kuwafanya wananchi waweze kufanya kazi za kuzalisha mali kwa sababu ni kwa kufanya hivyo tu peke yake ndiyo hata madhumuni makubwa kabisa ya Serikali ya kuiondoa nchi kutoka katika uchumi wa chini kwenda uchumi wa kati yatafanikiwa, ni kwa kufanya kazi tu peke yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili wananchi waweze kufanya kazi lazima waweze kuwa na ardhi au wawe na maeneo ya kufanyia kazi. Kabla hatujaanza kusema kwamba maeneo tunayoyatumia hayatoshi ni lazima kwanza tuone maeneo hayao yanatumikaje hivi sasa, kwa hiyo, hapa ndipo ambapo tunazungumzia juu ya suala la mpango wa matumizi bora ya ardhi.
Kuhusu swali lake tutashirikiana vipi na Wizara nne zile alizozitaja ukweli ni kwamba Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba tayari tunayo Kamati ya Kitaifa ya Wizara alizozitaja ambayo iko kazini inashughulikia suala hilo na baada ya utafiti wa kitaalam, baada ya kujiridhisha kitaalam tutapitia upya sheria na kuona katika kila eneo kama kweli suluhisho pekee la kuweza kuwafanya wananchi kupata eneo la kufanya shughuli za kibinadamu kama suluhisho pekee ni kugawa maeneo ambayo yamehifadhiwa kwa faida ambazo tunazifahamu ziko lukuki, basi Serikali itazingatia mwelekeo huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kutajitokeza ukweli kwamba bado maeneo tuliyonayo tunaweza kuyatumia vizuri zaidi bila kuathiri maeneo yaliyohifadhiwa basi hatutakuwa na haja ya kupunguza maeneo ya hifadhi isipokuwa tutajiimarisha zaidi katika kutumia vizuri zaidi maeneo ambayo hayajahifadhiwa kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili juu ya kuweka fence, kuweka uzio kwa ajili ya kuzuia wanyamapori kwenda kwenye maeneo ambayo ni ya binadamu, kwa ajili ya maeneo ya makazi ya binadamu na maeneo ambayo binadamu wanafanya shughuli za kibinadamu za kiuchumi na kijamii; napenda tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba huko ambako anazungumzia kwamba udhibiti umefanikiwa njia iliyotumika siyo hii tu peke yake ya kuweka fence, njia ya kuweka fence ni njia mojawapo na inatumika tu pale ambapo ni lazima kuweka fence kwa sababu njia hii ni ya gharama kubwa na si rafiki pia kwa mazingira hata kwa wanyama wenyewe na hata kwa binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoweza kwa sasa hivi ni kwamba Serikali inalichukua suala hili na kwa kweli tumekuwa tukilifanyia kazi muda mrefu kuweza kuona ni namna gani tunaweza kudhibiti kiwango na kasi ya Wanyamapori kutoka kwenye maeneo yao na kwenda kwenye maeneo ambayo ni ya binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la msingi hapa vilevile na binadamu na wenyewe tusiendelee na utaratibu ule wa kwenda kukaa kwenye maeneo ambayo aidha ni njia za wanyapori au ni maeneo ya mtawanyiko ya wanyamapori.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Mkomazi Game Reserve (sasa Hifadhi ya Taifa Mkomazi) ilianzishwa kabla ya Uhuru wakati tukiwa na idadi ndogo ya watu na mifugo. Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kusogeza mipaka ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi ili wananchi wa Kata za Visiwani, Mji Mdogo wa Same na Vumari wapate maeneo ya kuishi, kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la hifadhi ya Mlima Kilimanjaro una eneo la Half Mile au 0.8 ya kilometa, huduma za jamii kwa mfano uvunaji wa majani, uvunaji wa kuni kusafisha vyanzo vya asili vya maji, kwa mfano mifereji, inahusu vijiji 42 vya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi. Wakati huu hakuna mahusiano mazuri kati ya wananchi wa vijiji hivi 42 pamoja na Hifadhi chini ya KINAPA hasa wale askari. Serikali haioni ni vema pande zote zinazohusika yaani wawakilishi wa vijiji pamoja na KINAPA ikisimamiwa na Serikali kuweka taratibu na kanuni endelevu zinazoaminika za mazingira ya kisasa ili mahusiano mema kati vijiji 42 na Hifadhi ya Mlima Kilimajora viweze vikawa vya mazingira ya kisasa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi kabisa Serikali inazingatia ukweli kwamba ili uhifadhi uwe endelevu ni sharti wananchi wanaozunguka maeneo ya hifadhi husika, wanaopakana nazo waweze kuona kwamba wao ni sehemu ya huo uhifadhi kwenye hayo maeneo yanayohusika.
Kwa hiyo, njia zote zinazotumika katika kukamilisha malengo ya uhifadhi ni lazima ziwe rafiki kwa wananchi ambao wanazunguka kwenye maeneo hayo. Kwa sasa Serikali inachokifanya ni kuanzisha taratibu za kuwasogelea wananchi kwa ukaribu kabisa na kuwashirikisha, kuwapa elimu kwanza ya manufaa ya uhifadhi wenyewe, pia kuona namna gani wanaweza kushiriki kwenye jitihada za Serikali za kuhifadhi, muhimu zaidi mwishoni kabisa ni kuona namna ambavyo wananchi hawa wanaweza wakanufaika na uhifadhi moja kwa moja ukiacha ule utaratibu wa kunufaika na uhifadhi kwa njia na taratibu za kawaida za Kiserikali.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Mkomazi Game Reserve (sasa Hifadhi ya Taifa Mkomazi) ilianzishwa kabla ya Uhuru wakati tukiwa na idadi ndogo ya watu na mifugo. Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kusogeza mipaka ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi ili wananchi wa Kata za Visiwani, Mji Mdogo wa Same na Vumari wapate maeneo ya kuishi, kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wakati anajibu suala la Mbuga ya Mkomazi na Mbuga ya Mkomazi kwa Mkoa wa Tanga kuna Wilaya ya Lushoto, Korogwe na Mkinga. Tatizo la mipaka hata kule linatuathiri na kuna timu sasa inapita kutathmini hilo tatizo, nataka nitambue, je, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili imeshirikiana na hawa watalaamu ambao wanapita kutathmini ile mipaka, hasa katika eneo la Mwakijembe Wilaya ya Mkinga?

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mbuga ya Mkomazi kwa Mkoa wa Tanga iko katika Wilaya za Lushoto, Korogwe na Mkinga na hili tatizo la mipaka sasa hivi kuna timu ya ambayo iko chini ya RAS kwa kule Tanga inafuatilia haya maeneo yenye migogoro ambayo wananchi na mbuga wanakinzana hasa eneo la Mwakijembe katika Halmashauri ya Mkinga, je, Wizara ya Maliasili na Utalii inatambua uwepo wa hii timu ambayo inakagua mipaka?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa timu hiyo inayokagua mipaka.
Lakini Mheshimiwa Mbatia nafikiri wakati nikiwa namjibu swali alikuwa anasisitiza lini nilimuona wakati anataoka alikuwa anaendelea kuongea anauliza lini, sasa Mheshimiwa Mbatia tukimaliza kikao hiki cha Bunge (Kamati ya Fedha hivi) mimi na wewe tuambatane tukaangalie uhalisia ulivyo halafu tuweke ratiba ya kushughulikia suala hilo.