Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 51 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 422 2017-06-20

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-
Mkomazi Game Reserve (sasa Hifadhi ya Taifa Mkomazi) ilianzishwa kabla ya Uhuru wakati tukiwa na idadi ndogo ya watu na mifugo.
Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kusogeza mipaka ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi ili wananchi wa Kata za Visiwani, Mji Mdogo wa Same na Vumari wapate maeneo ya kuishi, kilimo na ufugaji?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa Mkomazi imetokana na kupandishwa hadhi kwa Pori la Akiba la Mkomazi – Umba kupitia Tangazo la Serikali Namba 27 la mwaka 2008. Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ilirithi mipaka ya lililokuwa Pori la Akiba la Mkomazi – Umba mipaka ambayo ilitambulika kisheria kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 275 la mwaka 1974.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ni sehemu muhimu ya mfumo wa kiikolojia na toshelezi kwa idadi ya wanyamapori waliopo hifadhini kujipatia mahitaji yao ikiwemo malisho, maji na maeneo ya mazalia hivyo kufanya hatua za kupunguzwa kwa eneo kusababisha athari hasi ikiwemo baadhi ya wanyamapori kutoka nje ya hifadhi kwa ajili ya kujitafutia mahitaji yao muhimu na hatimaye kusababaisha kuongezeka kwa migogoro kati ya binadamu na wanyama pori.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009 hairuhusu kufanyika kwa shughuli za kibinadamu ndani ya hifadhi ikiwepo kilimo, ufugaji na uchimbaji madini. Hivyo, kutokana na sababu hizi za msingi za kiuhifadhi, kwa sasa Serikali haioni haja ya kusogeza mipaka ya hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, isipokuwa kwamba Serikali itaendelea kupokea kutoka kwa wananchi na wadau wengine maoni yatakayozingatia matakwa ya sheria na taaluma ya uhifadhi. (Makofi)