Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TBC Radio kwenye maeneo ya Tarafa ya Amani Muheza ni hafifu. • Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mawasiliano ya redio na televisheni ya Kituo cha Taifa cha TBC? • Je, ni lini Serikali itaboresha mawasiliano kwenye maeneo hayo ya milima ya Amani ya Vituo vya Taifa Redio na TBC ili wananchi waweze kunufaika na vipindi hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Tarafa ya Amani tunaitegemea sana pale Muheza kwa mambo ya uchumi, kukosekana kusikilizwa kwa redio kwenye maeneo hayo pamoja na televisheni hususan kwenye Kata za Mbomole, Zirai, Misarai, Amani kwenyewe na Kwezitu kunawafanya wananchi hao kukosa uzoefu ili kuweza kujifunza sehemu nyingine. Swali langu la kwanza ni kama ifuatavyo:-
Kufuatana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwamba katika mwaka huu wa fedha 2017/2018 zimetengwa bilioni tatu, nataka uwahakikishie wananchi wa Amani kwamba nao wako kwenye mpango huu ili waweze kupata uzoefu wa kuona televisheni yao na redio yao ya Taifa?
Swali langu la pili; utaratibu wa TBC wanapoweka minara kwenye vijiji kuwalipa fidia wananchi wa vijiji hivyo vya karibu ili kuimarisha ulinzi na pia kuhakikisha kwamba usalama wa minara hiyo inakuwepo. Kata yangu moja ya Potwe ina mnara wa TBC, lakini hawajapata fidia na ninaomba kama kwenye mpango huu wa sasa hivi, kwenye hii Tarafa ya Amani patakuwepo na mipango ya kuongeza usikivu, basi wananchi hao waweze kulipwa fidia.
Naomba uwahakikishie wananchi hao mambo hayo, nakushukuru. (Makofi

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ametaka kujua hizo shilingi bilioni tatu kama wao nao wako kwenye mpango huu wa kuimarisha usikivu. Labda tu nitoe maelezo kama tulivyosema nadhani sote tulisikia hotuba ya Mheshimiwa Waziri akisoma katika bajeti yetu ni kwamba ziko Wilaya nyingi sana ambazo hazina usikivu. Ziko Wilaya takribani 84 usikivu wake ni hafifu sana. Tulipoanza kujaribu kuboresha usikivu katika Wilaya zetu tano tulianzia kwanza kwa mwaka huu wa fedha katika Wilaya ya Geita na tulipoweka mitambo ile ya FM katika Mkoa wa Geita tumegundua kwamba katika utafiti wetu ni kwamba masafa yale usikivu uko katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Geita na maeneo mengine.
Kwa mfano; usikivu umekwenda mpaka Geita Mjini, umekwenda Bukombe, umekwenda Chato, umekwenda Kahama, kwa hiyo, ni imani yangu kwamba tunapoboresha meneo ya Longido na maeneo ya Rombo pengine usikivu unaweza ukaboreka katika maeneo mengine. Kwa hiyo, siyo rahisi sasa hivi kuamua kwamba hizi shilingi bilioni tatu tunaweza kuzipeleka wapi, tunatarajia tuone kwamba effect inaweza au usikivu huu katika maeneo haya tutakayoboresha yanaweza yakaenda mpaka maeneo gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuna mpango mwingine wa kufufua ile mitambo ya zamani, mitambo ya AM ambayo yenyewe inakwenda mbali zaidi. Mwanzoni tulikuwa na mitambo minne tu ambapo mmoja ulikuwa Dodoma, mwingine Mwanza, mwingine Dare es Salaam na mmoja ulikuwepo Nachingwea, ambapo yote hii ilikuwa inapelekea usikivu katika nchi nzima. Kwa hiyo, tumeshakubaliana na wadau wa maendeleo kwamba watatusaidia kufufua mitambo hii, ili kusudi tuweze kuboresha usikivu katika nchi nzima. Ahsante.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TBC Radio kwenye maeneo ya Tarafa ya Amani Muheza ni hafifu. • Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mawasiliano ya redio na televisheni ya Kituo cha Taifa cha TBC? • Je, ni lini Serikali itaboresha mawasiliano kwenye maeneo hayo ya milima ya Amani ya Vituo vya Taifa Redio na TBC ili wananchi waweze kunufaika na vipindi hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa kama alivyosema muuliza swali wa kwanza TBC wameweza kupata shilingi bilioni tatu, naomba kumuuliza Mheshimiwa mjibu swali.
Ni lini Serikali itaweza kununua vifaa vidogo TVU au AVIWEST vifaa vile tukio linapotokea wanaweka pale pale tunakwenda kwenye breaking news, lakini TBC leo kwenye breaking news wanakodi vifaa, kifaa kimoja kinanunuliwa kama shilingi milioni 50 au shilingi milioni 60, hii ni aibu katika Serikali yetu.
Serikali waniambie ni lini wataweza kununua vifaa hivyo na kuvisambaza Tanzania kwa sababu masafa marefu hayasikiki. (Makofi)

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, kama nimempata vizuri Mheshimiwa Mbunge hii TVU ni kwa upande wa televisheni na ambapo tayari TBC imeshanunua vifaa hivi, ahsante.(Makofi)

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TBC Radio kwenye maeneo ya Tarafa ya Amani Muheza ni hafifu. • Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mawasiliano ya redio na televisheni ya Kituo cha Taifa cha TBC? • Je, ni lini Serikali itaboresha mawasiliano kwenye maeneo hayo ya milima ya Amani ya Vituo vya Taifa Redio na TBC ili wananchi waweze kunufaika na vipindi hivyo?

Supplementary Question 3

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu TBC 1 na TBC Redio ni visemeo vya Taifa, ndiyo spika ya Serikali. Je, kwa sababu matatizo ni mengi, usikivu karibu nchi nzima hawasikii vizuri, Je, Mheshimiwa Waziri hivi unatambua kwamba TBC1 na Redio TBC 1, televisheni ni kisemeo cha Taifa. Kwa nini sasa Serikali isiwekeze ili kuondoa kutokusikia vizuri katika maeneo mbalimbali?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Seneta Ndassa kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa TBC katika nchi hii na ndiyo maana umeona uwekezaji ukiongezeka kila mwaka. Sasa hivi tupo katika kuboresha usikivu katika Wilaya tano kwa pesa tuliyoongezewa tuna uwezo kuongeza usikivu katika Wilaya zingine 15. Kwa hiyo, tunapoongeza hizo Wilaya 15 tunaenda kuangalia sehemu ipi ambayo ina hali mbaya zaidi tutaendelea kuboresha hii bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa na matatizo ya kifedha, sasa hivi tumeanza kuangalia pia mifumo yetu ya ndani ambayo imekuwa ikitunyima kupata kipato zaidi. Tuna mikataba ambayo mmekuwa mkiipigia kelele hapa kama StarTimes, tumeanza kuchunguza, ninakuhakikishia kwamba katika zoezi tunalolifanya sasa hivi kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais tutafika mahali pazuri. Kwa taarifa tu kwa Bunge hili lako Tukufu Mheshimiwa Rais wa StarTimes Group kutoka China imebidi naye afunge safari kama mwenzetu wa makinikia kuja kutuona kwa ajili ya suala hilo.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TBC Radio kwenye maeneo ya Tarafa ya Amani Muheza ni hafifu. • Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mawasiliano ya redio na televisheni ya Kituo cha Taifa cha TBC? • Je, ni lini Serikali itaboresha mawasiliano kwenye maeneo hayo ya milima ya Amani ya Vituo vya Taifa Redio na TBC ili wananchi waweze kunufaika na vipindi hivyo?

Supplementary Question 4

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii nyeti. Wilaya ya Kakonko ni miongoni mwa Wilaya zenye matatizo ya usikivu wa TBC. Kule tunasikiliza Redio Burundi, ndugu yangu Mheshimiwa Mwamoto ni shahidi amekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibondo kule. Maeneo ya Kibondo na Kokonko hakuna usikivu wa TBC. Katika swali la msingi imetajwa Wilaya ya Kakonko. Naomba kujua na nipewe time frame na Serikali ni lini, ni tarehe ngapi TBC itaanza kusikika Kakonko?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli kwamba Kakonko ni moja ya zile Wilaya tano za mipakani ambazo zimetengewa fedha katika bajeti ya mwaka huu 2016/2017, ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwamba amekuwa akipambania usikivu katika Wilaya yake na ni kweli kwamba matangazo mengi wanayapata kutoka nchi jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu ambao tumeanza, tulianza na kufanya tathmini kwamba ni wapi minara iwekwe tayari tulishaomba masafa kutoka TCRA na tumepata, tayari mzabuni ameshapata zabuni ya kufanya kazi hii, lakini time frame tuliyopanga ni mwisho wa mwaka huu wa fedha usikivu utakuwa umeimarika katika Wilaya ya Kakonko na maeneo mengine ambayo ameyataja. Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TBC Radio kwenye maeneo ya Tarafa ya Amani Muheza ni hafifu. • Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mawasiliano ya redio na televisheni ya Kituo cha Taifa cha TBC? • Je, ni lini Serikali itaboresha mawasiliano kwenye maeneo hayo ya milima ya Amani ya Vituo vya Taifa Redio na TBC ili wananchi waweze kunufaika na vipindi hivyo?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na matatizo ya usikivu pia TBC kuna matatizo ya weledi kwa watangazaji. Mfano, kuna watangazaji wa TBC walitangaza uongo kwamba Donald Trump alimpongeza President Magufuli, upambe uliopitiliza mpaka tajiri anashtuka. Sasa wale watu walisimamishwa lakini hivi karibuni nimeanza kuwaona kwenye tv. Walipewa adhabu gani ili wasirudie tena upambe? (Kicheko)

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tulichukua hatua za kinidhamu kwa kosa ambalo ni la kiufundi tu ambalo mtu yeyote duniani hapa anaweza kulifanya. Yametokea matatizo kama hayo hayo Kenya yalifanyika na watangazaji wamerudi, tulichokifanya ni kuchukua tu hatua ya muda mfupi. Wazungu wanasema it’s a deterrent kwamba uwe muangalifu zaidi. Ni kitu kinafanyika kila siku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii nikikuletea, tuchukulie tu mfano wa magazeti yote yanayochapishwa kila siku, ninakuhakikishia asilimia 60 utakuta kuna matatizo/makosa ndani, ni kitu cha ubinadamu. Ahsante. (Makofi)

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TBC Radio kwenye maeneo ya Tarafa ya Amani Muheza ni hafifu. • Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mawasiliano ya redio na televisheni ya Kituo cha Taifa cha TBC? • Je, ni lini Serikali itaboresha mawasiliano kwenye maeneo hayo ya milima ya Amani ya Vituo vya Taifa Redio na TBC ili wananchi waweze kunufaika na vipindi hivyo?

Supplementary Question 6

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Nkasi usikivu kwa ujumla hasa mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika Tarafa ya Wampembe, Kata ya Kala, Wampembe, Kizumbi pamoja na Ninde hazina kabisa usikivu wa Redio Tanzania, bahati mbaya sana maeneo haya hayana mawasiliano ya barabara ya uhakika. Viongozi ni mara chache wanatembelea maeneo haya ukiacha DC, Mkuu wa Mkoa na viongozi wengine wa Chama. Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha usikivu katika eneo hili ili wananchi wa Ziwa Tanganyika mpakani kule wawe na usikivu wa kutosha kusikiliza matangazo mbalimbali ya nchi yao? (Makofi)

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Kama nilivyotangulia kusema mwanzoni, tuna mpango wa kufanya suluhisho la kudumu ambalo tunaweza kukarabati ile mitambo michache ambayo inaweza ikafika eneo la nchi nzima. Kwa mfano, mtambo ule wa Mwanza unaweza ukaenda mpaka maeneo hayo na tayari tumeshaandika andiko kupeleka kwa mbia wetu wa maendeleo ambaye tayari amekubali kufanya ukarabati wa mitambo hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini kabisa, kuliko kusubiri hizi fedha kidogo kidogo za kila mwaka ni bora tukaifufua ile mitambo ya AM ambayo haina matatizo kabisa na sifa zake ni kwamba inakwenda mbali sana na haipati pingamizi la milima.
Kwa hiyo, nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge awe na subira ili kusudi tuweze kupata majibu kutoka kwa mbia wetu wa maendeleo na kuweza kufufua mitambo yetu ambapo maeneo hayo aliyoyataja yatapata usikivu pamoja na nchi nzima.