Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Selemani Kaunje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Sokoine Mkoani Lindi inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji na ubovu wa vyoo katika wodi zake, pia watumishi wa hospitali hiyo wamekuwa na lugha na huduma duni zinazokera wateja. Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto zinazoikabili hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza Serikali ya Awamu ya Nne ilitoa ahadi ya kujenga kituo cha Afya katika kata ya Mnazi Mmoja. Ahadi hii ilikuwa ina inataka kutekelezwa na Serikali Kuu, mpaka tunapozungumza hakuna chochote kinachoendelea ikiwa ni mwaka wa saba sasa. Nini kauli ya Serikali kuhusu jambo hilo?
Swali la pili, wananchi wa Lindi tuliwahamasisha waanze kujenga vituo vya afya katika kata zao. Wamepata maelekezo kutoka TAMISEMI ya kwamba vituo hivyo visimame kujengwa kwa muda mrefu mpaka sasa. Nini kauli za Wizara dhidi ya watu wale ambao wameamua kujitolea kuweza kujenga vituo vile vya afya? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya Serikali kama zilivyo ahadi zingine na nikifahamu sehemu ya Mnazi Mmoja ni juction ya population kubwa na imetolewa ahadi hii takriban miaka saba, nikijua kwamba kuna juhudi zimeshaanza pale. Naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali naomba ihamasishe Halmashauri yako muanze kuibua jambo hili vizuri halafu na sisi tutaliratibu vizuri. Naomba nikuambie Serikali itakupa ushirikiano wa kutosha lengo letu ni kwamba commitment ya Serikali ya ahadi zote zilizotolewa na viongozi wetu wa Kitaifa tunaenda kuzitekeleza.
Kwa hiyo, naomba nikusihi Mheshimiwa Mbunge katika mchakato huu bajeti utakao kuja sasa tuliweke hili vizuri ili na sisi tutalipa nguvu, lengo kubwa kituo cha afya tuweze kukitengeneza katika eneo lile. Jambo la hivi vituo vya afya vingine ambavyo wananchi wameanza ujenzi nikijua kwamba commitment ya Serikali ni kuwahamazisha wananchi katika suala zima la ujenzi wa afya. Kama vituo hivyo ni vipya vinaendelea basi naomba niseme kwamba tutaendeleza kuvihakikisha tunavipa nguvu. Lakini nikijua kwamba kuna utaratibu ambao wakati mwingine umejitokeza kuna utaratibu wa kubadilisha zahanati kuwa kituo cha afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana Ofisi yetu sasa ilitoa maelekezo kama hizi zahanati tuziache ziwe zahanati lakini tujenge vituo vipya viwe vya afya. Lakini kwa sababu Bwana Kaunje jambo hili umelileta hapa naomba nikuhakikishie kwamba ofisi yetu itakupa ushirikiano wakutosha kuangalia scenario ipi iliyoko kwenye Manispaa ya Lindi tuweze kusaidiana kwamba wananchi waweze kupata huduma kutokana na hali halisi ilivyo pale kwako Lindi.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Sokoine Mkoani Lindi inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji na ubovu wa vyoo katika wodi zake, pia watumishi wa hospitali hiyo wamekuwa na lugha na huduma duni zinazokera wateja. Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto zinazoikabili hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa katika jitihada za kupunguza mzigo mkubwa unaobebwa na Hospitali ya Lindi, Serikali iliingia makubaliano na hospitali za mission kwa mfano Hospitali ya Nyangao pale Jimbo la Mtama kwa ajili ya kusaidiana nao katika kutoa huduma za afya ili tupunguze mzigo mkubwa katika Hospitali ya Lindi. Lakini utekelezaji wa makubaliano hasa upelekaji wa fedha na watumishi kwa ajili ya kufanya kazi katika hospitali hizi ambazo mmekubaliana nazo hautelekezeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali sasa itaanza kupeleka pesa kama walivyokubaliana pamoja na watumishi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Nape, naomba tulichukue hilo kwa sababu kuna hizi ahadi najua kwamba katika hospitali mbalimbali zinatekelezeka na nikijua kwamba kweli kuna shida kubwa na ndiyo maana kutokana na kesi ile ya kwako tumeona kwamba pale Kituo cha Nyangarapa ambao kituo cha afya kwenda kukiboresha zaidi kama tulivyokubali pale mwanzo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tutaenda kukiboresha kituo hiki lakini suala zima la commitment za hizi taasisi ambazo za dini au vituo mbalimbali vya dini au vituo mbalimbali binafsi ambao Serikali imeingilia nazo, kama kuna scenario ambayo kwa Wakilindi iko tofauti kidogo upelekaji wa fedha hauko vizuri tunakwenda kuufuatilia kuangalia jinsi gani tuuboreshe wananchi waweze kupata huduma vizuri.