Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 50 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 409 2017-06-19

Name

Hassan Selemani Kaunje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Hospitali ya Rufaa ya Sokoine Mkoani Lindi inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji na ubovu wa vyoo katika wodi zake, pia watumishi wa hospitali hiyo wamekuwa na lugha na huduma duni zinazokera wateja.
Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto zinazoikabili hospitali hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS,TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Kaunje Mbunge wa Lindi Mjini kama kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutatua changamoto zinazokabili Haspitali ya Mkoa wa Lindi zikiwemo uchakavu wa miundombinu, katika mwaka wa fedha 2016/2017 iliidhinishiwa kiasi cha shilingi miioni 344 kwa ajili ya kazi ya ukarabati wa miundombinu ambapo fedha zote zimepelekwa.
Vilevile Mkoa umepanga kutumia shilingi milioni 185 kwa ajili ya kujenga kichomea taka (incinerator) ya kisasa na ukarabati wa hospitali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kazi zinazoendelea hivi sasa ni ukarabati wa wodi ya wazazi, wodi ya upasuaji wa wanaume na aidha, katika kutatua tatizo la maji Serikali inakamilisha mradi mkubwa wa maji katika eneo la Ng’apa, Manispaa ya Lindi unaotarajiwa kumaliza kabisa tatizo la maji katika Manispaa ya Lindi. Wodi ya daraja la I. Aidha, mkandarasi atakayejenga kichomea taka ameshapatikana ili kuanza kazi hiyo. Vilevile Serikali ipo katika hatua za mwisho ya kupata mkandarasi kwa ajili ya ukarabati wa wodi ya watoto, jengo la upasuaji (theatre) jengo la huduma ya afya ya kinywa na meno na jengo la huduma ya macho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imepanga kukarabati wodi ya wagonjwa ya akinamama, chumba cha mionzi na jengo la utawala. Ukarabati wa miundombinu utafanyika sambamba na uboreshaji wa mfumo wa maji safi na maji taka.