Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI (K.n.y MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- Serikali ilitoa mafunzo kwa walimu ambao walihitumu mwaka 2015 lakini walimu hao hawajaweza kuajiriwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaajiri walimu hao walioachwa ingawa kiuhalisi bado kuna uhaba mkubwa wa walimu katika shule za sekondari hasa vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Issa Mangungu na wananchi wa Mbagala nitakuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Serikali katika mwaka unaokuja 2017/2018 wamepanga kutoa ajira za walimu. Je, ni walimu kiasi gani ambao wamepangwa kwenda kuajiriwa katika Wilaya ya Temeke hususan katika jimbo la Mbagala, katika shule za sekondari za Kingugi, Mbande, Charambe, Toangoma na Mbagala Kuu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali katika mwaka huu imeajiri walimu wengi wapya, je, ni lini sasa Serikali itawapatia stahiki zao walimu hawa wapya na pia kuwapatia makazi ili kuwawesha kufanya kazi yao kwa ufanisi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema pale awali kwamba tuna mpango wa kuajiri walimu, lakini katika hili sasa hivi tunafaya vile vile na tathmini ya idadi ya walimu ambao wametoka katika system ya kiserikali mara baada ya vyeti fake. Kwa hiyo, tutaleta taarifa rasmi hapa baadaye kwamba idadi ya walimu ambao wamekutana na vyeti fake ambapo hivi sasa kuna deficit ambayo itakuwepo, lakini na idadi ya walimu wapya. Kwa hiyo, tutaleta taarifa rasmi ya idadi ya walimu. Hata hivyo naomba nikuhakikishe Mheshimiwa Jamal kwamba kwa Mkoa wa Dar es salaam maeneo ya Temeke na mimi nafahamu sana Temeke ilivyogawanyika mpaka kwenda kule ndani maeneo ya Toangoma tutaangalia ni jinsi gani tutafanya ili maeneo hayo kama ambavyo umeainisha tuweze kuwapeleka walimu wa kutosha ili vijana wetu wanaokwenda kujiunga, waweze kupata elimu hiyo inayokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika upande wa pili wa swali lako nadhani Mheshimiwa Jamal, nimesahau kidogo kipengele cha pili.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI (K.n.y MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- Serikali ilitoa mafunzo kwa walimu ambao walihitumu mwaka 2015 lakini walimu hao hawajaweza kuajiriwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaajiri walimu hao walioachwa ingawa kiuhalisi bado kuna uhaba mkubwa wa walimu katika shule za sekondari hasa vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na swali la msingi kwa kuwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi imesema watoto wote wasome bure, katika jimbo la Kaliua shule ya msingi Ushokola walimu wanafundishia nje na walimu hawatoshi. Ni lini Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi itaona hili tatizo la Kaliua kuongezea walimu wa shule za msingi? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Bulembo, Senior MP, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la bwana Bulembo bahati nzuri siku nne zilizopita nilikuwa na viongozi kutoka katika Wilaya ya Kaliua, walifika ofisini kwangu pale lakini ili kujadili ajenda za kimaendeleo. Ninasema Senior MP kwa sababu mwanzo alikuwepo na hivi sasa mnajua kazi zake kubwa anazozifanya katika nchi hii na juzi alikuwepo kule Mkoa wa Tabora nadhani ndio maana ameweza kufanya verfication ya tatizo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa zaidi nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge; nilikubaliana na viongozi waliotoka Kaliua kwamba nitafika Kaliua. Naomba nikuhakikishie kwamba nitatembelea shule ile ili kubaini mahitaji halisi. Hata hivyo Serikali tutaweka mpango, namna ya kufanya ili tuweze kujenga miundombinu na kuwapatia walimu ili vile vile wananchi wa eneo lile wapate fursa ya kusema tulitembelewa na mjumbe wa Kamati Kuu ambaye anasimamia suala zima la utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. (Vicheko/Makofi)

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI (K.n.y MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- Serikali ilitoa mafunzo kwa walimu ambao walihitumu mwaka 2015 lakini walimu hao hawajaweza kuajiriwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaajiri walimu hao walioachwa ingawa kiuhalisi bado kuna uhaba mkubwa wa walimu katika shule za sekondari hasa vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa vile swali langu ni sawa sawa na hali halisi iliyoko Mbagala, ningependa nimuulize Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwamba jimbo la Same Mashariki limekuwa na shida sana ya walimu, tuna kata moja ya Bwambo, shule ya Changuruwe imekuwa na walimu wawili tangu darasa la kwanza mpaka la saba kwa muda mrefu sana na kilio hiki hakijaweza kusikilizwa na kufanyiwa kazi. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kunisaidia ni lini atanipa walimu tuongezee hii shule ambayo wanabidii sana lakini kwa walimu wawili hata ungefanya nini hawawezi kutosheleza kusaidia wanafunzi? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge nikupe pole katika hilo. Nilivyofika katika Mkoa wa Kilimanjaro, miongoni mwa Mikoa ambayo ina walimu wengi ni Mkoa wa Kilimanjaro. Kwa hiyo, nitumie fursa hii sasa kumuagiza Afisa Elimu wa Mkoa, haiwezekani walimu wote wakajazana Moshi Mjini, wakati wananchi wa Same hawana walimu. Nimuagize Afisa Elimu wa Mkoa wa Kilimanjaro, shule zinapofunguliwa ahakikishe shule ambayo Mheshimiwa Mbunge ameianisha katika Halmashauri ya Same amepeleka walimu wa kutosha, la sivyo tutamuona kwamba hatoshi kusimamia eneo hilo la elimu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI (K.n.y MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- Serikali ilitoa mafunzo kwa walimu ambao walihitumu mwaka 2015 lakini walimu hao hawajaweza kuajiriwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaajiri walimu hao walioachwa ingawa kiuhalisi bado kuna uhaba mkubwa wa walimu katika shule za sekondari hasa vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kupata fursa hii. Kama ilivyoshida ya walimu katika jimbo la ndugu zangu wa Mbagala na sisi watu wa Mkuranga tunashida kubwa ya upungufu wa walimu. Serikali inanipa ahadi gani ya kuhakikisha kwamba upungufu ule wa walimu unapungua? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Ulega, kama alivyokuwa makini kusimamia shughuli za maendeleo katika jimbo lake, naomba nimuhakikishie kwamba katika mchakato huu wa sasa wa kuelekea kuajiri walimu Mkuranga tutaipa kipaumbele, na nikijua kwamba jimbo lako lile limetawanyika sana, tutakupa kipaumbele ili elimu kwa wananchi wa Mkuranga iweze kupanda na hatimaye waweze kupata mafanikio mazuri ya Serikali yao.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri napenda niongezee sehemu kidogo tu. Waheshimiwa Wabunge ni karibu maeneo mengi yana upungufu wa walimu na hasa kwenye shule zetu za msingi. Pamoja na jitihada za Serikali kuwapeleka walimu ambao wanaonekana wamezidi katika baadhi ya maeneo lakini baadhi ya shule bado walimu hao ni wachache, kwa sababu ya changamoto za miundombinu zilizopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapopokea mipango ya Halmashauri na vipaumbele vyao inasikitisha kuona wakati mwingine mipango hiyo, na kwa sababu utawala wa nchi hii unatoka chini kwenda juu na si juu kwenda chini na ndio maana bajeti inaanza kupangwa kutoka chini baadaye juu tunakuja kumalizia, tungelitegemea vipaumbele viwe nyumba za walimu na miundombinu kama hiyo inayotegemea kujenga mazingira bora ya watumishi hawa kwenda kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokizungumza Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza swali la msingi inaonekana ni mazingira magumu ya kule milimani ya kule Same ndiyo maana walimu hawakai, hivyo ukijiuliza hakuna nyumba na hata walimu hawa wakifika uongozi tu wenyewe kuwapokeana kujenga mazingira mazuri ni vigumu sana, hawashughuliki nao, na ndiyo maana kuna upungufu.
Kwa hiyo niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, sisi ndio tunaoshiriki kwenye vikao vya maamuzi makubwa, sisi tunashiriki kwenye vikao ambavyo vinapanga mipango na bajeti. Tupange mipango hiyo inayotatua kero za nyumba za walimu ndipo tutakapoweza kuwa-retain walimu hawa katika shule zetu.