Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 401 2017-06-16

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI (K.n.y MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:-
Serikali ilitoa mafunzo kwa walimu ambao walihitumu mwaka 2015 lakini walimu hao hawajaweza kuajiriwa.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaajiri walimu hao walioachwa ingawa kiuhalisi bado kuna uhaba mkubwa wa walimu katika shule za sekondari hasa vijijini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2017 Serikali imeajiri walimu 3,081 wa masomo ya sayansi na hisabati ambao wameshapangwa na kuripoti katika shule walizopangiwa nchi nzima. Ajira hizo zimetolewa kwa walimu waliohitimu mafunzo mwaka 2015 na mwaka 2016. Mpango wa Serikali ulikuwa ni kuajiri walimu 4,129. Hata hivyo, walimu 1,048 wa masomo hayo ya sayansi na hisabati hawakupatikana katika soko wakati wa uhakiki wa vyeti uliofanywa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imepanga kuajiri watumishi wa kada mbalimbali wakiwemo walimu katika mwaka wa fedha 2017/2018.