Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa wana majukumu mengi ikiwemo kuhakikisha amani na usalama katika maeneo yao:- Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho ya mwezi ya Wenyeviti hawa ili kutoa motisha kwa kazi yao?

Supplementary Question 1

MHE.ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 20 ni fedha ndogo sana inayopelekwa kijijini na kama wataamua kumlipa Mwenyekiti wa Kijiji, Serikali ya Kijiji haitafanya kitu chochote kingine. Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka wa kubeba jukumu hili la kuwalipa Wenyeviti wa Vijiji?
Swali langu la pili, kutokana na umuhimu sasa wa kundi hili na malalamiko yaliyopo kila kona nchini Serikali sasa haioni ni muda muafaka wa kutoa waraka maalum ambao utatoa maelekezo kwa mamlaka ya Serikali za Mitaa kuhusu malipo ya Wenyeviti hawa na kuweka kiwango cha chini cha posho hiyo, badala ya kila Halmashauri kutekeleza jinsi wanavyoona wao inafaa.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia kwa tathmini, maeneo mbalimbali posho hizi huwa hazilipwi na hoja ya Mbunge ni kwamba asilimia 20 ni ndogo. Ina maana ukiirejesha Kijijini, ikimlipa Mwenyekiti wa Kijiji mwisho wa siku ni kwamba fedha ile haitatosheleza hata kufanya kazi zingine za vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu Serikali za Mitaa safari hii ndiyo maana tumeweka Specification katika bajeti ya mwaka huu. kila Halmashauri wakati ikipitia mchakato wa bajeti tuione inakidhi jinsi gani itahakikisha mapato yake ya ndani kwa kupitia vyanzo mbalimbali ili mwisho wa siku iweze kuhakikisha kwamba inapeleka fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana tumesisitiza kuanzia Julai Mosi lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba hili jambo tunalolifanya, jinsi gani kila Halmashauri iweze kukusanya pesa za kutosha. Lengo ni kwamba Wenyeviti wa Vijiji waweze kupata posho, hali kadhalika pesa nyingine iende katika shughuli zingine za Maendeleo ya Kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili juu ya kupanga kiwango maalum, ni kweli. Sehemu zingine wanalipa sh. 20,000, sehemu nyingine wanalipa sh. 10,000, tutaangalia lakini, tutafanya utafiti wa kutosha kuona jinsi gani hii hali iende sawasawa. Kwa sababu tunajua wazi kwamba kila mtu hapa katika Bunge hili anategemea kazi ya Mwenyekiti wa Kijiji au Mwenyekiti wa Mtaa katika kufanikisha shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwa ni sambamba na mikutano yetu ambayo tunaenda kuifanya katika Jumuiya hizo.