Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:- Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?

Supplementary Question 1

MHE. LIVINGSONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Naibu Waziri kwa majibu, hata hivyo napenda kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; urefu wa barabara alizotaja na milioni 350 kweli hapo kuna matengenezo ya barabara kwa kiwango cha changarawe au ni kwa kiwango cha tope?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa mvua za mwaka huu Mungu ametupa neema zimekuwa nyingi na zimetusaidia sana kwa upande wa kilimo, vilevile zimeleta uharibifu mkubwa sana wa barabara na madaraja, Mheshimiwa Waziri anatuambiaje juu ya matengenezo mazuri na yenye maana kwa ajili ya wananchi kuweza kupitisha mazao yao ambayo wanategemea kuyavuna ili waweze kujiletea maendeleo? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, anaulizia juu ya idadi ya kilometa ambazo nimezitaja na kiasi cha fedha ambacho kimetumika je, tumetengeneza kwa ubora uliotarajiwa au tumeyatengeneza kwa kutumia tope.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza hatujatumia tope kwa sababu yeye mwenyewe ni shuhuda kwamba tumehama kutoka katika matengenezo yaliyokuwa yanafanywa na Halmashauri pale ambapo kila Mheshimiwa Diwani alikuwa akiomba angalau apate hata kilometa moja au kalivati moja katika aeneo lake, mwisho wake inakuja inafikia kwamba hata ile thamani ya pesa ambayo imetumika haikuweza kuonekana na hivyo tukawa tunarudia kila mwaka katika matengenezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Lusinde na bahati nzuri na yeye ni shuhuda amekuwa akifanya kazi nzuri ya kupita kwenye Jimbo lake hebu akalinganishe kazi ambayo imefanywa na chombo hiki cha TARURA linganishe na jinsi ambavyo kazi zilikuwa zinafanyika hapo awali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili ameongelea neema ya mvua ambayo tumepata na sisi sote tukiwa ndani ya Mkoa wa Dodoma ni mashuhuda, tumepata mvua ya kutosha, mvua ni neema, lakini kila neema nayo inakuja na dhahama yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba nimhakikishie chini ya TARURA na ndiyo maana kuna maeneo ambayo kumekuwa na mataengenezo na maombi maalum ili kuhakikisha kwamba barabara hizi zinapitika vipindi vyote na kiasi cha pesa ambacho chombo hiki kimeombewa kama Bunge lako Tukufu itaidhinisha chini ya usimamizi madhubuti hakika barabara zitatengenezwa kwa kiwango kizuri na kitakachoweza kupita katika vipindi vyote.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:- Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwanza napongeza TARURA kwamba wameanza kazi vizuri hususani katika Mji wangu wa Korogwe, lakini napenda kujua je, Wizara ina mpango gani sasa wa kuwawezesha hawa TARURA hususani kwenye hizi Halmashauri za Miji pamoja na kwamba wanawapa fedha za kujenga barabara zile kwa kiwango cha changarawe, sasa wapewe fedha za kutengeneza ile mifereji kwa kiwango cha kutumia mawe ili kusudi wasiweze kurudia mara kwa mara kutengeneza zile barabara? Wana mpango gani wa kuwatengea fedha ili Miji hii iweze kuwa na barabara zilizo imara kwa kupitia kuweka mawe misingi yao? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri yote ya msingi ya mwanzo yaliyoweza kutolewa. Naomba nimpongeze mama Mary Chatanda ni miongoni mwa Wabunge ambao tulipambana sana katika ujenzi wa barabara na stendi yake ya pale Korogwe Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa utengenezaji katika Halmashauri za Mji kwanza tunatumia mradi wa UGLSP ambao tunagusa takribani Manispaa na Halmashauri zote za Mji. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie Wabunge wote ambao wako katika Halmashauri za Miji na Manispaa mpango wetu mkakati ni kuhakikisha maeneo haya tunayabadilisha kwa ajili ya ujenzi katika maeneo haya kwa tabaka la lami. Huu ndiyo mpango wa Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, katika ile Miji Mikuu Saba ambayo nimezungumza tutaaendelea kuboresha suala la mifereji, suala la barabara kwa kiwango ambacho tunajua kwamba barabara zetu tunataka guarantee ya miaka 20 ndiyo tuweze kuzifanyia service, ndiyo maana hatuko katika supervision ya hali ya juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba nikiri kwamba TARURA tuna mtandao wa barabara takribani kilometa 108,000 ambao ni matandao mkubwa sana, lakini ukiangalia kutokana na suala la kisera la mgawanyo wa Mfuko wa Barabara ambao asilimia 30 inakuja TARURA na asilimia 70 inaenda TANROAD, eneo hili ndilo lina changamoto kubwa. Baadaye tutaangalia nini cha kufanya, lengo letu kubwa ni kwamba Halmashauri zote ziweze kupitika kwa sababu wananchi huko ndiko uchumi unapojengeka. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:- Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ninachotaka kujua TARURA ni chombo ambaco kimeundwa hivi karibuni, nataka kujua TARURA sasa kwa sababu barabara wanazoshughulikia ni zile zilikuwa zinashughulikiwa na Halmashauri chini ya Madiwani. Je, hiki chombo sasa kinasimamiwa na mamlaka gani kwa niaba ya wananchi, kwa sababu hawaingii kwenye Baraza la Madiwani?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba TARURA ni chombo ambacho kimeanzishwa hivi karibuni. Kimsingi taarifa ya kazi zinazofanyika taarifa yake inapelekwa kwenye chombo kinaitwa DCC na katika DCC Waheshimiwa Wabunge wote wanakuwemo kwenye kile chombo, lakini pia kila Mwenyekiti wa Halmashauri husika anahudhuria kwenye hicho kikao na ndiyo fursa ambayo kwa sasa hivi TARURA inatoa taarifa juu ya utekelezaji wa kazi zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama hiyo haitoshi, hata katika vipaumbele vya barabara ambazo zinaenda kutengenezwa ni wajibu wa Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani wote tunaidhinisha barabara ambazo ni vipaumbele, lakini TARURA inapelekewa kulingana na bajeti sasa wao ndio wanasema katika hizi barabara tunaenda kutengeneza barabara zipi, lakini fursa kama forum ya Waheshimiwa Madiwani bado ipo.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:- Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH S. MTULIA: Mheshimiwa Naibu Spika, Alhamdulilah. Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru sana, lakini pia nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima, nina afya njema, akili timamu na utayari wa hali ya juu ya kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Kinondoni na tunasema dua la mwewe halimpati kuku. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo letu la Kinondoni na Manispaa ya Kinondoni kwa ujumla TARURA inafanya kazi vizuri, tunawapongeza sana. Hata hivyo, Manispaa yetu ya Kinondoni ina barabara za kiwango cha lami siyo zaidi ya asilimia 10 za barabara zote katika Manispaa ya Kinondoni na tumewaambiwa wananchi tunataka kuleta Kinondoni mpya; je, TARURA ina mpango gani wa kutuongezea barabara zetu katika kiwango cha lami ili angalau kufikia asilimia 50 kama siyo asilimia mia moja?(Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) - MHE. JOSEPH S. KANDEGE:
Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi niungane na Wabunge wenzangu kumpongeza sana Mheshimiwa, welcome again uko katika nafasi iliyo sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambayo chombo chetu TARURA kinafanya kazi vizuri ni pamoja na Manispaa ya Kinondoni, nimepata fursa ya kwenda kutembelea, Halmashauri zingine zinatakiwa kwenda kuiga na kutazama kazi nzuri ambayo inafanywa na TARURA Kinondoni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala zima la kuongeza ili angalau tufike asilimia 50 ya barabara zote kuwa za lami, kati ya Miji ambayo ina fursa ya kupata maendeleo kwa maana ya miundombinu ya barabara ni pamoja ni Jiji letu la Dar es Salaam. Naamini katika mpango mzima wa kuboresha Jiji la Dar es Salaam na program zinazoendelea hakika, barabara za Kinondoni zitahama kutoka hiyo asilimia kufika asilimia 50 katika kipindi ambacho siyo kirefu sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, nataka tu niongezee katika majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba katika eneo la Kinondoni ambako Mbunge aliyeapishwa leo Mheshimiwa Mtulia anatoka ni kwamba hiyo coverage tutaifika haraka sana kwa sababu tuna combination mbili; tuna mradi wa DMDP ambao Mheshimiwa Mbunge anaufahamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu una kazi kubwa sana ya kuboresha miundombinu ya barabara za lami katika Jiji la Dar es Salaam na eneo la Kinondoni ni eneo moja wapo, lakini kuna upande mwingine upande wa TARURA, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge aondoe hofu zile ahadi alizozisema kwa wananchi wake, naamini ikifika mwaka 2020 zote zitakuwa zimetekelezwa tena kwa zaidi.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:- Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Hata hivyo, nitumie fursa hii kuwashukuru wananchi wa Siha kwa kuniamini tena na kuhakikisha hawa wanaosema muda nawapiga kipigo ambacho hawajawahi kukisikia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna barabara yetu ya kutokea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwenda kwenye Kata ya Biriri kukutana na barabara inayotokea Sanya Juu kuelekea mpaka KIA (Kilimanjaro International Airport), kwa mwaka jana ni katika barabara mbili ambazo zilikuwa zipandishwe hadhi kuingizwa TANROAD ikashindikana ikawa imepanda barabara moja ya Mwanga. Nataka kumuuliza Waziri mwaka huu basi isidunde kama zawadi ya watu wa Siha kwa uamuzi wa busara walioufanya. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) - MHE. JOSEPH S. KANDEGE:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze na kumkaribisha sana Dkt. Mollel na kumhakikishia kwamba yuko katika nafasi ambayo ni salama sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kupandisha hadhi barabara ambayo anaiongelea ili iwe chini ya TANROAD.
Mheshimiwa Naibu Spika, wewe ni shuhuda kwamba Waheshimiwa Wabunge wengi tulikuwa tunapenda barabara za Majimboni kwetu zipandishwe zichukuliwe na TANROADS, lakini ni kwa nini tulikuwa tunataka zichukuliwe na TANROADS? Ni kutokana na namna ambavyo barabara ambazo ziko chini ya TANROADS zimekuwa zikihudumiwa kwa namna nzuri. Ndiyo maana kama Bunge tukaona kwamba ni vizuri tukaanzisha chombo ambacho kitakuwa kinafanya kazi madhubuti kama ambavyo zimekuwa zikifanywa na TANROADS.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie, kwa kasi ambayo tumeanza nayo na jinsi ambavyo TARURA imeanza kufanya kazi, nimtoe mashaka, barabara ambayo anaisemea chini ya TARURA itakuwa na hadhi na ubora sawa na barabara ambazo zinatengenezwa chini ya TANROADS.