Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 02 2018-04-03

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Serikali iliunda chombo kinachosimamia barabara za Vijijini na Mijini kinachoitwa TARURA:-
Je, chombo hicho kitaanza lini kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwani barabara hizi ni mbaya sana hasa wakati wa masika?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Livingstone Joseph Lusinde, Mbunge wa Mtera, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) ilianzishwa kwa Sheria za Wakala za Serikali, Sura 445 na kutangazwa katika Gazeti la Serikali Na. 211 la tarehe 12 Mei, 2017. TARURA imeanza rasmi tarehe Mosi Julai, 2017, kwa ajili ya utekelezaji wa matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 108,946.2 katika mwaka wa fedha 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA imeidhinishiwa shilingi bilioni 230.8 kwa ajili ya matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 34,024. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 98.5 zimetolewa na kutumika kujenga barabara zenye urefu wa kilometa 4,188.31, madaraja 35, makaravati makubwa 43 na makaravati madogo 364.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018, barabara zilizojengwa katika Jimbo la Mtera zina urefu wa kilometa 93.3 kwa gharama ya Sh.356,737,115.80. Barabara hizo ni:-
Handali – Chanhumba – Igandu - Nghahalezi (kilometa nne); Nghahalezi – Miganda – Idifu - Iringa Mvumi - Mlowa barabarani (kilometa tano); na Nagulomwitikila - Huzi - Ilangali (kilometa 17) kwenda Nhinhi - Wiliko (kilometa 20); Mlowa barabarani - Makangw’a (kilometa 12); Manzase – Sasajila - Ilowelo (kilometa 21.3); Chipogolo - Loje - Igungili (kilometa 14). Wakandarasi wanaendelea kufanyakazi na wanatarajia kukamilisha kazi hiyo Mei, 2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019, TARURA imeomba kutengewa kiasi cha shilingi bilioni 243.3 kwa ajili ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilometa 23,465.05, ukarabati wa madaraja 117, mifereji ya mvua yenye urefu wa mita 67,844 na makaravati 1,881 kwa nchi nzima.