Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Primary Question

MHE. HAMAD SALIM MAALIM aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 16 inatoa uhuru wa faragha kwa raia. Je, kwa nini Jeshi la Polisi linapokwenda kupekua kwenye nyumba yenye mume na mke hutumia askari wa kiume peke yao?

Supplementary Question 1

MHE. HAMAD SALIM MAALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo hayaridhishi pia nina maswali mawili ya nyongeza.
Katika jibu la msingi Mheshimiwa Waziri amesema kwamba busara na utu wa mwanadamu huwa unazingatiwa, lakini naomba niseme kwamba siyo kweli kwamba busara na utu wa mwanadamu unazingatiwa.
Mimi binafsi nimefanyiwa tendo hili na nilipodai kwamba kwa nini hamkuja na askari wa kike wakalazimisha kutumia nguvu. Sasa naomba niulize Jeshi la Polisi, je, tabia hii mbaya itamalizika lini?
Swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuniletea orodha ya malalamiko ya matendo haya yaliyotendeka? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la kwanza kwamba inawezekana kuna tukio ambalo Mheshimiwa Mbunge anathibitisha lilimtokea binafsi la kufanyika upekuzi bila kuhusisha askari wa kike, naomba hili tulichukue ili tuelewe ni sababu gani iliyosababisha hilo litokee, halafu tuone sasa mimi na yeye Mheshimiwa Mbunge labda baadae tukae tuweze kulijua suala hili lilikuwaje ili tuone hatua gani ya kuchukua. Orodha tutampatia lakini siwezi kumpatia hapa kama Mheshimiwa Naibu Spika alivyosema.

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. HAMAD SALIM MAALIM aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 16 inatoa uhuru wa faragha kwa raia. Je, kwa nini Jeshi la Polisi linapokwenda kupekua kwenye nyumba yenye mume na mke hutumia askari wa kiume peke yao?

Supplementary Question 2

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, lakini kabla ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumpongeza aliyekuwa Kaimu Waziri Mkuu Mheshimiwa Mwakyembe kwa kazi nzuri aliyoifanya Kukaimu Kiti cha Waziri Mkuu.
Baada ya hapo nichukue fursa hii swali la msingi linahusu mwanamke na mwanaume, je, kuna sheria gani iliyopitishwa na Bunge kama mtu kafanya kosa mume akakamatwa mke kuna utaratibu gani au kuna sheria iliyopitishwa? Vilevile ninavyojua mimi utaratibu…

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Jaku anataka kujua kama kosa la mwanamke anakamatwa mwanamume. Kosa aliyefanya ndiye atakayekamatwa, kwa hiyo, haiwezekani Mheshimiwa Jaku kosa akafanya mtu mwingine ukakamatwa wewe.