Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 102 2018-02-08

Name

Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Primary Question

MHE. HAMAD SALIM MAALIM aliuliza:-
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 16 inatoa uhuru wa faragha kwa raia.
Je, kwa nini Jeshi la Polisi linapokwenda kupekua kwenye nyumba yenye mume na mke hutumia askari wa kiume peke yao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamad Salim Maalim, Mbunge wa Kojani kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la upekuzi ni jukumu ambalo sheria imelipa Jeshi la Polisi na utaratibu wake umeainishwa wazi namna ambavyo upekuzi utafanyika kwenye maeneo mbalimbali. Kifungu cha 38 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 inatoa masharti na utaratibu wa kuweza kufanya upekuzi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo nyumba, majengo na vyombo vya usafiri kama magari, boti na kadhalika endapo Afisa wa Polisi atakuwa amehisi na amejiridhisha pasipo na shaka kwamba kuna sababu ya kutosheleza kuwa kuna uwezekano wa kosa kutendeka au ushahidi kupatikana kuthibitisha kosa lililotendeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, upekuzi wa makazi ya nyumba yenye mke na mume sheria haijaweka masharti ya ni askari wa jinsia gani anatakiwa kufanya upekuzi. Hata hiyo, Jeshi la Polisi kwa kutumia Kanuni ya Kudumu za Jeshi la Polisi (PGO) pia kwa kuzingatia busara na utu wa mwanadamu huwa inazingatia utaratibu wa kupeleka askari wa kike na wa kiume pale upekuzi unapofanyika kwenye makazi ya mume na mke.