Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Songwe kwa michango yao wenyewe wamejenga jengo kubwa kwa ajili ya Kituo cha Polisi katika Kata ya Mpona tangu mwaka 2014 ili kupambana na majambazi wanaovamia wananchi hasa wakati wa mavuno ya zao la ufuta. Je, ni lini Serikali itasaidia kuamlizia jengo hilo na kupeleka askari polisi ili kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 1

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo itakuwa ni mara ya pili nipende tu kusikitika kwamba swali hili tena halijajibiwa na Bunge lililopita mwezi Novemba, swali langu nalo halikujibiwa vizuri sasa sijui nina mkosi gani. Kwa sababu swali la msingi haliendani kabisa na majibu ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na swali langu la kwanza liwe hivi. Naomba Serikali iniambie inatumia mfumo gani wa kuwajibu maswali Wabunge humu ndani, kwa sababu Wabunge wengi wamekuwa wakilalamika maswali hayo hayajibiwi vizuri?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, bado niseme namuomba Waziri tena Waziri mwenye dhamana aje Jimbo la Songwe afanye ziara aangalie jinsi ambavyo vijiji vyangu na kata vilivyo scattered ili aone umbali wa kutoka kijiji kimoja kwenda kijiji kingine, karibuni kilometa 20 hapa, ndipo wanaweza kujenga vituo vya polisi. Lakini kunijibu kwamba kipaumbele ni RPC na OCD wala haviingi akilini naomba Mheshimiwa Waziri mwenyewe anijibu.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mulugo; ni kweli anafuatilia sana masuala ya Jimbo lake na hasa haya yanayohusu askari kufuatana na aina ya Wilaya yake na aina ya Jimbo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwa sababu la msingi na ushauri alioutoa ni kufika kule, nimuahidi baada ya Bunge hili kabla ya Bunge la Bajeti nitazungukia Wilaya yake kule ili nijionee mwenyewe haya anayoyasemea ili tuweze kutengeneza utaratibu ulio mzuri wa kushughulika na jambo hilo alilolielezea.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Songwe kwa michango yao wenyewe wamejenga jengo kubwa kwa ajili ya Kituo cha Polisi katika Kata ya Mpona tangu mwaka 2014 ili kupambana na majambazi wanaovamia wananchi hasa wakati wa mavuno ya zao la ufuta. Je, ni lini Serikali itasaidia kuamlizia jengo hilo na kupeleka askari polisi ili kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 2

MHE. FAKHARIA SHOMARI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Kwa kuwa kituo cha polisi Ziwani Zanzibar kuna baadhi ya majengo yamechakaa na yanahitaji ukarabati. Je, Mheshimiwa Waziri anawajulisha nini askari hao polisi wa Ziwani kuhusu ukarabati wa majengo yao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Makao Makuu ya Polisi Ziwani kuna changamoto ya miundombinu ikiwemo uchakavu wa majengo. Serikali tunalitambua hilo na tupo katika mbalimbali za kuhakikisha kwamba tunafanya marekebisho hayo kadri ya hali ya upatikanaji fedha itakaporuhusu.

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Songwe kwa michango yao wenyewe wamejenga jengo kubwa kwa ajili ya Kituo cha Polisi katika Kata ya Mpona tangu mwaka 2014 ili kupambana na majambazi wanaovamia wananchi hasa wakati wa mavuno ya zao la ufuta. Je, ni lini Serikali itasaidia kuamlizia jengo hilo na kupeleka askari polisi ili kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 3

MHE. OMARY A BADWELI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Tarafa ya Chipanga wameitikia wito wa kujenga kituo cha polisi miaka 13 iliyopita, kituo kikubwa kizuri na cha kisasa na wakati huo kilighalimu 40,000,000. Hata hivyo tangu nikiwa diwani mpaka nimekuwa Mbunge kipindi cha miaka 13 nimehangaika na Wizara ya Mambo ya Ndani wafungue wapokee na wafungue kituo kile cha polisi hawajafanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya kumpeleka Mheshimiwa Shamsa Vuai Nahodha akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani akaagiza kifunguliwe hakikufunguliwa; nikampeleka Mheshimiwa Silima akaagiza kifunguliwe na akawahaidi wananchi wa pale ndani ya miezi sita kwamba kituo kile kitakuwa kimefunguliwa mpaka leo hakijafunguliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali langu, je, Serikali inajua kwamba miezi sita waliohaidi wananchi wa Kata ya Chipanga na Tarafa ya Chipanga kwamba imekwisha na hawajapokea kituo hicho cha polisi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kama leo sikupata majibu ya uhakika ya kwamba wanakipokea na kuja kukifungua kituo kile cha polisi nawaambia Jumamosi ijayo nakwenda kuwakabidhi wananchi kituo chao cha polisi ili wafanyie shughuli zingine ikiwemo kukaa watumishi kama nyumba ambao na wenyewe wana matatizo makubwa. Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hii si mara ya kwanza Mheshimiwa Badwel kuuliza swali hili Bungeni na binafsi nilipata fursa ya kuzungumza naye kuhusianana mchakato wa ufunguzi wa kituo hiki na nilikuwa nimemwambia kabisa niko tayari kwenda kufungua wakati wowote. Lakini Mheshimiwa Badwel tulikubaliana kwamba tuchukue hatua kwanza kuhakikisha kwamba RPC wa Mkoa wa Dodoma anakwenda kulikagua ili kuona maandalizi yote kabla ya ufunguzi yamekamilika. Makubaliano hayo baina yangu mimi na Mheshimiwa Mbunge. Kwa hiyo nashangaa sana leo Mheshimiwa Badwel hazungumzii zile hatua ambazo tumepiga mimi na yeye binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu ambacho kilikwamisha ufunguzi ni changamoto ambayo imetokana na wananchi wenyewe pamoja na Mheshimiwa Mbunge wa eneo lile. Tulichokubaliana na Mheshimiwa Badwel ni kwamba kutokana na hali ya kituo ilivyo inahitaji kiweze kuwekwa sawa vizuri. Nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa muda mrefu. Hiyo hiyo hatuwezi kuwa wezi wa fadhila tusipompongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa hali ya bajeti ilivyo mwaka huu wa fedha tumepanga takribani shilingi milioni 150 ambazo tutatoa kipaumbele katika kukamilisha vituo ambavyo vimefikia katika hatua kama ambavyo kituo hiki ambacho kiko katika Jimbo la Mheshimiwa Badwel kilipofikia.
Lakini kipindi hiki ambapo bado fedha hazijapatikana, ikiwa kuna uwezekano wa kuendelea kukamilisha yale marekebisho madogo madogo ili kiweze kufikia viwango vya kuweza kufunguliwa rasmi waweze kufanya hivyo, vinginevyo tusubiri bajeti itakapokuwa imekamilika ili tuweze kukikamilisha na kuweza kukizindua. Wakati wowote hayo yatakapofanyika nitakuwa tayari kwenda kukizindua ili wananchi waweze kukitumia.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Songwe kwa michango yao wenyewe wamejenga jengo kubwa kwa ajili ya Kituo cha Polisi katika Kata ya Mpona tangu mwaka 2014 ili kupambana na majambazi wanaovamia wananchi hasa wakati wa mavuno ya zao la ufuta. Je, ni lini Serikali itasaidia kuamlizia jengo hilo na kupeleka askari polisi ili kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru ingawa kwa kweli majibu ya Waziri, Naibu Waziri yanakatisha tamaa maana tumekuwa tukisikia siku zote kadri fedha zitakavyopatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi wa raia na mali zao ni muhimu sana katika nchi yetu. Kwenye Jimbo la Tarime Mjini katika Kata zote nane tuna kituo cha poilisi kwenye Kata ya Bomani tu, na Kata zingine ambazo za pembezoni wananchi wamejitolea kujenga vituo vya polisi. Tunataka kujua mkakati thabiti wa Serikali katika ku-support zile juhudi za wananchi hasa Kata ya Nyandoto, Kenyamanyoli, Nkende na Kitale ambazo ni mbali na mji, na kuna gari moja tu ambayo inafanya patrol.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nini mkakati wa Serikali maanake mnakusanya mapato mengi, muweze kuelekeza kwenye kumalizia vituo vya poilisi ili tuweze kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nieleze tu kwa ufupi, ni kwamba changamoto ya vituo vya polisi haipo tu katika vituo vya polisi vya ngazi ya kata na tarafa, tuna Mikoa ya kipolisi takribani 34 nchi nzima. Kati ya hiyo majengo ambayo ya makamanda wa mikoa yaliyopo nchini ni 19. Kwa hiyo takribani mikoa 15 haina Ofisi ya Makamanda wa Mikoa. Mikoa miwili Manyara na Mara ndiyo ambapo ujenzi wa Ofisi mpya za makanda unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mtaona changamoto hii ni pana sana, na ndiyo maana wakati wote tumeendelea kuwashawishi wadau werevu ikiwemo ninyi Waheshimiwa Wabunge ambao wengi wenu mmekuwa mkijitolewa na sisi tumekuwa tukichukua jitihada mbalimbali kuhamasisha wananchi kujitolea kuchangia ujenzi wa vituo hivyo vya polisi ili kabiliana na changamoto hii; wakati ambapo Serikali kila mwaka imekuwa ikitenga bajeti kwa ajili ya ujenzi pamoja na ukarabati wa vituo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi hii haiwezi kumalizika kwa wakati mmoja. Naamini wewe Mheshimiwa Mbunge ni Mbunge wa Jimbo na una fedha za Mfuko wa Jimbo. Unaweza ukatumia hizo vilevile kusaidia jitihada hizi za Serikali katika kuhakikisha kwamba ina punguza changamoto ya upungufu wa vituo vya polisi nchi nzima kuanzia ngazi ya Wilaya, Kata na Tarafa. Serikali kama ambavyo tunasema pale fedha zitakapopatikana tutapunguza tatizo hili hatua kwa hatua, hatuwezi tukamaliza kwa wakati mmoja.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Songwe kwa michango yao wenyewe wamejenga jengo kubwa kwa ajili ya Kituo cha Polisi katika Kata ya Mpona tangu mwaka 2014 ili kupambana na majambazi wanaovamia wananchi hasa wakati wa mavuno ya zao la ufuta. Je, ni lini Serikali itasaidia kuamlizia jengo hilo na kupeleka askari polisi ili kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yaliyoko Songwe yanafanana kabiasa na matatizo yaliyoko kwenye Jimbo la Geita Vijijini. Jimbo la Geita Vijijini lina wakazi kama 650,000, na tuna vituo viwili vikubwa ambavyo wasimamizi wao ni askari wenye nyota mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumelalamika muda mrefu sana kwa ngazi ya Mkoa wetu naona sasa tutafute msada huku kwa Waziri. Jimbo zima na vituo hivi vikubwa havina askari wa kike, kwa hiyo askari wa kiume wanawapekua wanawake.
Sasa pengine kwa kuwa sisi ni vijijini hakuna haki za binadamu, nilikuwa namuomba Mheshimiwa Waziri, ni lini utatuletea askari wa kike kwenye vituo vile vikubwa ili wake zetu wakapekuliwe na askari wa kike na si askari wa kiume? (Makofi).

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yake ni ya msingi tutaifanyia kazi.