Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 89 2018-02-07

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Songwe kwa michango yao wenyewe wamejenga jengo kubwa kwa ajili ya Kituo cha Polisi katika Kata ya Mpona tangu mwaka 2014 ili kupambana na majambazi wanaovamia wananchi hasa wakati wa mavuno ya zao la ufuta.
Je, ni lini Serikali itasaidia kuamlizia jengo hilo na kupeleka askari polisi ili kituo hicho kianze kutoa huduma?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Phillipo Augustino Mulugo kwa uhakika, Mbunge wa Songwe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Songwe ni kati ya mikoa mipya iliyoanzishwa hivi karibuni ambayo ina changamoto nyingi ya vituo vya polisi, ofisi pamoja na nyumba za askari kama ilivyo katika maeneo mengine ya nchini. Aidha, katika mkoa mpya wa Songwe hakuna Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa na Wakuu wa Polisi wa Wilaya mbili mpya za Momba na Songwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa jitihada alizofanya yeye na kushirikiana na wananchi wa Kata ya Mpona za kujenga Kituo cha Polisi katika eneo hilo. Aidha, kwa sasa kipaumbele ni ujenzi wa Ofisi ya Kamanda wa Mkoa pamoja na Wilaya mpya. Hata hivyo Serikali inafanya jitihada ili kukamilisha kituo hicho kulingana na upatikanaji rasilimali.