Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K.n.y. MARY P. CHATANDA) aliuliza:- Mahakimu na Watumishi wa Mahakama hawajapandishwa vyeo kwa muda mrefu na hata wanaobahatika kupandishwa hawabadilishiwi mishahara:- (a) Je, ni lini Serikali italifanyia kazi tatizo hilo? (b) Kwa kuwa Wanasheria wengine hupewa house allowance: Je, kwa nini hawa nao wasipewe kama sehemu ya motisha lakini pia wapewe extra duty allowance?

Supplementary Question 1

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Profesa mwenzangu kwa majibu mazuri na yenye msimamo. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Mahakimu wengi wa Mahakama za Mwanzo wanafanya kazi katika mazingira magumu na wanapokwenda kwenye Mahakama za vijijini huwa wanatumia usafiri wa mabasi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia usafiri kwa ajili ya usalama wao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mahakimu wengi wanakaa katika nyumba za mtaani za kupangisha. Katika nyumba hizo huwa baadhi yao kuna watuhumiwa wanaowajua sehemu walipo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Mahakimu hao wanapata nyumba maalum kwa ajili ya usalama wao? Ahsante sana.

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo wanafanya kazi katika maeneo magumu hasa maeneo ya vijijini yenye matatizo ya usafiri. Kutegemea hali ya bajeti itakavyokuwa inaboreka Serikali ina mpango wa kuwapa vyombo vya usafiri, hasa Mahakimu ambao wanahudumia maeneo makubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu nyumba za Mahakimu Serikali pia inatambua umuhimu wa Mahakimu kuwa na nyumba na kwa kuwa sasa imeanza na mpango wa ujenzi wa Mahakama mara baada ya zoezi la ujenzi wa Mahakama litakapokuwa limefikia mahali pazuri basi Serikali ina mpango pia wa kufikiria kuanza kujenga nyumba za Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo hasa katika maeneo ambayo yana matatizo makubwa. (Makofi)

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K.n.y. MARY P. CHATANDA) aliuliza:- Mahakimu na Watumishi wa Mahakama hawajapandishwa vyeo kwa muda mrefu na hata wanaobahatika kupandishwa hawabadilishiwi mishahara:- (a) Je, ni lini Serikali italifanyia kazi tatizo hilo? (b) Kwa kuwa Wanasheria wengine hupewa house allowance: Je, kwa nini hawa nao wasipewe kama sehemu ya motisha lakini pia wapewe extra duty allowance?

Supplementary Question 2

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Mahakimu wengi wamekuwa wanaenda shuleni kwa kujiendeleza kwa maana ya shule ya sheria kwa vitendo (Law School of Tanzania), lakini wengi wao wameachwa wakifanya kazi kwenye Mahakama za Mwanzo, Mahakama ambazo haziendani na taaluma zao, huku katika Mahakama zetu za Wilaya na Mahakama za Hakimu Mkazi kuna upungufu wa Mahakimu. Nataka kujua ni lini Serikali sasa ita-upgrade wanafunzi hawa ambao wamepitia elimu ya sheria kwa vitendo ili waweze kufanya kazi kulingana na taaluma yao. (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inawapongeza sana Mahakimu wote ambao wamechukua hatua ya kujiendeleza kielimu na pia kwenda katika Shule ya Sheria kwa Vitendo au Taasisi ya Sheria kwa Vitendo. Kwa kuzingatia hilo kila mwaka Mahakama imekuwa na mpango wa kupitia wale waliopata sifa ili waweze kupandishwa madaraja kulingana na elimu walioyoipata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ulivyosema ni sahihi kabisa kwamba lengo la Serikali sasa ni kuhakikisha pia kwamba Mahakimu wote wa Mahakama za mwanzo ambapo ndiko kwenye mashauri mengi wawe ni wale ambao wana Shahada za Chuo Kikuu na kwa maana hiyo baada ya miaka michache ijayo Mahakama zote za Mwanzo zitakuwa na Mahakimu ambao wana Shahada ya Kwanza ya Sheria ukizingatia kuwa huko ndiko kwenye mashauri mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo huo kuendelea ku-upgrade hao ambao wamejiendeleza na tunawapongeza na tunawatia moyo waendelee kufanya hivyo. (Makofi)