Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2000-2005 Session 12 Sitting 6 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 75 2018-02-06

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K.n.y. MARY P. CHATANDA) aliuliza:-
Mahakimu na Watumishi wa Mahakama hawajapandishwa vyeo kwa muda mrefu na hata wanaobahatika kupandishwa hawabadilishiwi mishahara:-
(a) Je, ni lini Serikali italifanyia kazi tatizo hilo?
(b) Kwa kuwa Wanasheria wengine hupewa house allowance: Je, kwa nini hawa nao wasipewe kama sehemu ya motisha lakini pia wapewe extra duty allowance?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mary Pius Chatanda, Mbunge wa Korogwe Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuwapandisha vyeo Watumishi wenye sifa stahiki ni wajibu endelevu wa Serikali. Mahakama ya Tanzania imekuwa ikichukua hatua kuwapandisha Mahakimu na Watumishi wa ngazi mbalimbali vyeo kuzingatia vigezo vilivyowekwa kisheria ikiwa ni pamoja na muda wa utumishi kazini, utendaji wa kazi, weledi na maadili pamoja na upatikanaji wa vibali kutoka Idara Kuu ya Utumishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013, jumla ya Mahakimu na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji 52 walipandishwa vyeo. Mwaka 2013/2014, jumla ya Watumishi 200 walipandishwa vyeo, mwaka 2014/2015, jumla ya Mahakimu na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji 22 na Watumishi 686 walipandishwa vyeo na mwaka 2015/2016, jumla ya Mahakimu na Wasaidizi wa Sheria 59 na Watumishi 447 walipandishwa vyeo.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kutoa posho kwa watumishi wake kama sehemu ya motisha. Mahakama imeendelea kutoa motisha ya posho mbalimbali na stahili za watumishi kwa mujibu wa sheria, kulingana na uwepo au hali ya bajeti.