Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa ya Haydom inahudumia wananchi wengi lakini inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi, madaktari wakiwemo Madaktari Bingwa pamoja na ukosefu wa maji. (a) Je, Serikali itachukua hatua gani za dharura kutatua changamoto hizo? (b) Kwa kuwa watumishi hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu, je, ni kwa nini Serikali isiondoe kodi kwenye posho zao kama vile on-call allowance, hardship allowance na food allowance?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza naomba nimpongeze sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na ya kuridhisha. Pia nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali yetu kwa kuipandisha hadhi Hospitali ya Haydom kuwa Hospitali ya Rufaa Ngazi ya Mkoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na upandishwaji hadhi huko, ni kwa nini Serikali yetu isione umuhimu wa kuhakikisha kwamba inajenga miundombinu ya hospitali hii muhimu inayohudumia mikoa zaidi ya mitatu hasa katika suala la upatikanaji wa maji, jambo ambalo ni muhimu sana? Amekiri mwenyewe kwamba source ya maji sasa hivi ni umbali wa kilometa 25 kutoka hospitali kwa kutumia jenereta ambayo inakabiliwa na uharibifu wa mara kwa mara. Suala la REA Awamu ya Tatu linachukua muda mrefu, tungeomba Serikali ifikirie kupeleka umeme katika hospitali hii muhimu kabla ya hata REA kufikia eneo hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, suala la income tax kwenye posho za watumishi wa Hospitali ya Haydom tayari ameshaonyesha kwamba kuna tabaka mbili ya watumishi katika hospitali hiyo, lakini ukweli na utafiti unaonyesha kwamba baadhi ya watumishi katika Hospitali za Wilaya na kwingineko katika nchi yetu hawakatwi kodi kwenye on-call allowances lakini hawa watumishi wa Haydom wanakatwa na hasa tukizingatia kwamba wanafanya kazi katika mazingira magumu sana. Tunaomba Serikali itoe kauli katika hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Umbulla, naomba kwa moyo wa dhati kabisa nimpongeze kwa jinsi ambavyo amekuwa akipigania wananchi wa mkoa wake lakini bila kusahau hata Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo jinsi ambavyo wamekuwa wakiipigania hospitali yao hii ya Haydom. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maswali yake ya nyongeza anasema kwamba ufanyike utaratibu wa haraka ili kuwezesha kupatikana umeme kabla ya REA.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, utaratibu wa haraka kabisa na chanzo cha uhakika ni kwa kutumia REA Awamu ya Tatu, nadhani ndiyo njia sahihi. Kwa taarifa tulizonazo Serikalini ni kwamba tayari mkandarasi yupo kule. Kwa hiyo, tuvute subira, kama mmesubiri muda wa kutosha, kipindi kilichobaki ni kifupi na tatizo hili litakuwa limeondoka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na watumishi ambao wameajiriwa na Hospitali hii ya Haydom kukatwa on-call allowance. On-call allowance inakatwa kwa sababu wao katika malipo ambayo wanafanya, wanajumuisha pamoja na mshahara wao na ukisoma ile Sheria ya Income Tax, unapotaka kukata kodi lazima utizame vyanzo vyote, ni tofauti na hawa wa Serikalini ambao allowance hizi huwa zinalipwa dirishani, hazisubiri mpaka kipindi cha kuja kulipa mshahara wa mwisho. Kwa hiyo, ni namna tu watakavyojipanga wakaji-adjust inawezekana kabisa wasikatwe hicho wanachokatwa. (Makofi)

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona na namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa majibu yake kwa maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ni vizuri tuweke rekodi sawasawa. Bunge hili kupitia Finance Act ya mwaka 2011 liliongeza misamaha kwa posho mbalimbali. Katika vitu vilivyoongezwa kwamba vitasamehewa kodi ya mapato ni allowance payable to an employee who offers intramural private services to patients in a public hospital and housing allowance, transport allowance, responsibility allowance, extra duty allowance and honoraria payable to an employee of the Government or its institution whose budget is fully or substantially paid out of Government budget subvention. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, allowances hizi ndizo zilizosamehewa kodi kwa mujibu wa sheria na TRA hiki ndicho wanachofanya. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa ya Haydom inahudumia wananchi wengi lakini inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi, madaktari wakiwemo Madaktari Bingwa pamoja na ukosefu wa maji. (a) Je, Serikali itachukua hatua gani za dharura kutatua changamoto hizo? (b) Kwa kuwa watumishi hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu, je, ni kwa nini Serikali isiondoe kodi kwenye posho zao kama vile on-call allowance, hardship allowance na food allowance?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa tunapozungumza Hospitali ya Amana imepelekwa katika Wizara ya Afya na kwa maana hiyo Manispaa ya Ilala haina Hospitali ya Wilaya. Bahati nzuri katika Jimbo la Ukonga, Kata ya Kivule kuna eneo la ekari 45, Manispaa ya Ilala imeshaanza kuweka msingi.
Je, ili kupata huduma ya afya katika Manispaa ya Ilala kwa kuwa na Hospitali ya Wilaya, nini kauli ya Serikali katika jambo hili? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Hospitali ya Amana imechukuliwa na hivyo kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge hawana hospitali. Pia ni ukweli usiopingika kwamba jana nilipata fursa ya kuteta na Mheshimiwa Mbunge akaniambia katika own source yao walikuwa wametenga shilingi bilioni moja kwa ajili la kuanza ujenzi wa hospitali yao. Kwa hiyo, ninachowaomba, zile jitihada ambazo walishazianzisha za kuanza kujenga hospitali ya kwao ya Wilaya zisisimame, ni lazima zitiwe msukumo tuhakikishe kwamba wananchi wetu wanapata maeneo mengi ya kujitibia. Nikitoka hapa nitafanya kila jitihada niwasiliane na Mkurugenzi ili nimuelekeze hicho kiasi cha pesa ambacho kimetengwa kifanye kazi iliyokusudiwa.

Name

Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa ya Haydom inahudumia wananchi wengi lakini inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi, madaktari wakiwemo Madaktari Bingwa pamoja na ukosefu wa maji. (a) Je, Serikali itachukua hatua gani za dharura kutatua changamoto hizo? (b) Kwa kuwa watumishi hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu, je, ni kwa nini Serikali isiondoe kodi kwenye posho zao kama vile on-call allowance, hardship allowance na food allowance?

Supplementary Question 3

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Kishapu lina zahanati 45 zilizokamilika na zinafanya kazi, vituo vya afya vinne vimekamilika vinafanya kazi na viwili tayari tunasubiri vianze kufanya kazi hivi karibuni na tuna hospitali kubwa ya kisasa ambayo inafanya kazi vizuri. Kwa kuwa tumekwishaleta maombi ya upungufu wa baadhi ya madaktari, wauguzi na watumishi wa kada ya afya, je, Mheshimiwa Naibu Waziri, uko tayari kukaa na mimi hata leo tupitie maombi hayo uone namna ambavyo utasaidia jitihada za watu wa Kishapu? Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla ya kujibu kama niko tayari au siko tayari, naomba niwapongeze kwa jitihada ambazo zimefanyika za kuweza kuhakikisha kwamba huduma za afya zinapatikana kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niko tayari kabisa, kabisa. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa ya Haydom inahudumia wananchi wengi lakini inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi, madaktari wakiwemo Madaktari Bingwa pamoja na ukosefu wa maji. (a) Je, Serikali itachukua hatua gani za dharura kutatua changamoto hizo? (b) Kwa kuwa watumishi hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu, je, ni kwa nini Serikali isiondoe kodi kwenye posho zao kama vile on-call allowance, hardship allowance na food allowance?

Supplementary Question 4

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali hii ya Haydom kwenye swali la msingi iko katika jimbo langu na inaihudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Mara, Singida na Shinyanga. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu alishafika na kutuahidi kwamba atatupatia watumishi zaidi na Mheshimiwa Ummy amefika kwenye hospitali hiyo. Je, lini sasa Serikali inatimiza ile ahadi yake ya kutupatia watumishi katika hospitali hii ambayo inahudumia mikoa mingi niliyoisema?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali ilishatoa ahadi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tatizo la watumishi linaweza kutatuliwa haraka iwezekanavyo.
Mheshimiwa Mbunge ni shahidi, jana alikuwepo, Mheshimiwa Waziri wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora alitoa majibu kwamba kwa zile Halmashauri na maeneo ambayo tunahitaji kuweza kuziba pengo hilo kwa haraka ni vizuri barua zikaandikwa. Pia tunakiri kabisa juu ya kujengea uwezo Hospitali ya Haydom kwa sababu inahudumia wagonjwa wengi, naomba tufuate procedures za kawaida ili jambo hili liweze kutatuliwa kwa wakati.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ngazi ya Mkoa ya Haydom inahudumia wananchi wengi lakini inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi, madaktari wakiwemo Madaktari Bingwa pamoja na ukosefu wa maji. (a) Je, Serikali itachukua hatua gani za dharura kutatua changamoto hizo? (b) Kwa kuwa watumishi hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu, je, ni kwa nini Serikali isiondoe kodi kwenye posho zao kama vile on-call allowance, hardship allowance na food allowance?

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nitoe shukrani kwa Serikali, wanasema kwamba usiposhukuru kwa kidogo basi hata kikubwa hutaweza kupata, kwa sababu nililalamika hapa sina hata kituo cha afya kimoja, lakini sasa hivi nimepewa pesa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha pili na pesa za kuboresha kile kituo cha afya cha zamani ambacho nilisema ni mfu, kwa hiyo nasema ahsanteni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bado Hospitali ya Wilaya ya Liwale ina tatizo la nursing officers na mpiga picha wa x-ray. Ni lini Serikali itaweza kutupatia watumishi hawa wa kada mbili; mpiga picha wa x-ray na nursing officers? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, ambalo kimsingi amekuwa akipigania sana wananchi wake na mimi najua na jana alikuwepo na majibu yaliyokuwa yametolewa aliyasikia. Kwa msisitizo na nimejibu katika swali kutoka kwa Mheshimiwa Kigoda kwamba ni vizuri tukaweza kutumia own source kama ambavyo wao wamefanya na katika maeneo ambayo wameajiri ni pamoja na hawa wataalam wa picha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, inawezekana, kama wenzetu wa Handeni wamefanya, Liwale tunaweza. Bahati nzuri kule sasa hivi hali ya kipato inakwenda juu kabisa. Kwa hiyo, ni namna tu ya kupanga kitu gani ni kipaumbele kwa ajili ya wananchi kupata huduma. Ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba kwa kupitia bajeti yake ikiruhusu tutaweza kuajiri na kupeleka watumishi wa kada ya afya.