Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Halmashauri zina wataalam wa kusimamia na kutekeleza mipango yao na zina uwezo kisheria kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo, elimu, afya, maji kilimo na ardhi pasipo kuingiliwa. Viongozi na Watendaji wa Serikali ngazi za Mkoa na Wilaya huambiwa watawajibishwa kufikia malengo mathalani, katika ujenzi wa maabara, madarasa na kutengeneza madawati:- Je, mipaka ipi ni ya kinadharia (theoretical) na ipi inatekeleza (practical) kiutendaji na uwajibikaji kati ya viongozi wa Serikali Kuu na Halmashauri za Majiji, Miji na Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina swali la nyongeza. Serikali iko moja nayo ni Serikali Kuu na hao wote waliotamkwa wanatekeleza kutokana na maagizo ya Serikali Kuu. Je, inakuwaje pale ambapo hela hazipelekwi za kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali inafuatilia vipi kuepusha migongano hiyo kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pale ambapo fedha za kutekeleza mradi fulani hazijapelekwa zote mawasiliano yanafahamika kati ya waliopokea na waliopeleka. Kwa hiyo hayo yanakuwa ni maelezo sahihi wakati wa tathmini kwamba hatukuweza kutekeleza vizuri mradi huu au hatukukamilisha kwa sababu fedha imekuja nusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hiyo ni mawasiliano ya ndani ya Serikali na mara nyingi imefanyika; lakini kitu kimoja kizuri kwa upande wa Serikali za Mitaa ni kwamba wanapopewa wakati mwingine fedha imezidi au imechelewa kuja imekuja mwishoni mwa mwaka wa fedha wenzetu wanaruhusiwa kubaki na fedha ile halafu mwezi wa Saba wanakaa kwenye vikao vyao rasmi wanazipitisha kwa ajili ya matumizi yaliyovuka mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la pili kwamba tunafuatiliaje mgogoro; Serikali ina macho usiku na mchana. Kule kule ziliko Serikali za Mitaa wapo waangalizi wa Serikali ambao wanakusanya taarifa kila siku asubuhi na mchana kwa masaa yote. Kwa hiyo kama kuna harufu yoyote ya mgogoro Serikali Kuu huwa inapata taarifa hizo mara moja. Ahsante sana.

Name

Maida Hamad Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Halmashauri zina wataalam wa kusimamia na kutekeleza mipango yao na zina uwezo kisheria kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo, elimu, afya, maji kilimo na ardhi pasipo kuingiliwa. Viongozi na Watendaji wa Serikali ngazi za Mkoa na Wilaya huambiwa watawajibishwa kufikia malengo mathalani, katika ujenzi wa maabara, madarasa na kutengeneza madawati:- Je, mipaka ipi ni ya kinadharia (theoretical) na ipi inatekeleza (practical) kiutendaji na uwajibikaji kati ya viongozi wa Serikali Kuu na Halmashauri za Majiji, Miji na Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. MAIDA H. ABDALLAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa miradi mingi ya maendeleo ngazi ya Halmashauri imekuwa ikisuasua na ikikwama kutokana na ucheleweshwaji wa fedha kutoka Hazina. Je, Serikali inatoa kauli gani katika ukamilishwaji wa miradi ya maendeleo iliyopitishwa na bajeti ya Serikali mwaka 2015/2016 na 2016/ 2017?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kusuasua kwa miradi; huku kunategemea na eneo na mradi na Halmashauri husika. Ziko Halmashauri ambazo tumekuwa tukizifuatilia na kuwashauri kuhusu matumizi ya fedha kwa wakati. Wakati mwingine wanakuwa na fedha kwenye akaunti lakini wakati mwingine watekelezaji kule kwenye mradi wanakuwa hawajui kama fedha zimekuja. Kwa hiyo matatizo mengine ni ya kimawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kusisitiza, Halmashauri mara zinapopata fedha kutoka Serikali Kuu, zijipange kwa haraka na kwa wakati kutumia fedha hizo kwa ajili ya wananchi, wasiziache kwenye akaunti. Pale ambapo kuna ucheleweshaji wa aina yoyote wafanye mawasiliano haraka na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kusudi tuweze kufuatilia kwa wenzetu tuweze kusuluhisha suala hilo mara moja.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Halmashauri zina wataalam wa kusimamia na kutekeleza mipango yao na zina uwezo kisheria kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo, elimu, afya, maji kilimo na ardhi pasipo kuingiliwa. Viongozi na Watendaji wa Serikali ngazi za Mkoa na Wilaya huambiwa watawajibishwa kufikia malengo mathalani, katika ujenzi wa maabara, madarasa na kutengeneza madawati:- Je, mipaka ipi ni ya kinadharia (theoretical) na ipi inatekeleza (practical) kiutendaji na uwajibikaji kati ya viongozi wa Serikali Kuu na Halmashauri za Majiji, Miji na Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa hapa nchini wamekuwa wakiwasimamisha hovyo watumishi wa Serikali za Mitaa bila kufuata taratibu na sheria zilizopo. Je, nini kauli na msimamo wa Serikali katika suala hili? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kukanusha, hakuna sehemu yoyote ambayo Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa amesimamisha watu kazi hovyo, hakuna! Nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba usimamishaji wowote wa kazi unafuata masharti ya taratibu za kazi na sheria zinazomwongoza anayetoa amri hiyo. Ahsante sana. (Makofi)