Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Kwa muda mrefu chanzo cha maji cha Ruvu Chini na Ruvu Juu kimekuwa chanzo pekee cha maji katika Mkoa wa Pwani. Lakini kimsingi chanzo hicho hakitoshelezi mahitaji na hivyo kushindwa kumaliza tatizo la maji. Je, ni lini Serikali itatumia chanzo cha maji cha Mto Rufiji kuwapatia maji safi na salama wananchi hususan wa Wilaya ya Rufiji, Kibiti, Mkuranga na Kisarawe?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Nabu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ningependa kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Waziri utakubaliana na mimi kuvunwa kwa maji ya Mto Rufiji ni pasi moja ndefu mpaka golini, na ushindi huo unanufaisha akinamama kutua ndoo kichwani. Sasa ni kwa nini Serikali inapata kigugumizi kuanza kuyavuna maji haya ili kupoza kiu ya Mheshimiwa Rais ya kuwatua akinamama ndoo kichwani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa mradi huu hauna dalili ya kuanza leo wala kesho. Na kwa kuwa, mradi wa maji ya visima uliopo haukidhi mahitaji ya Wana Rufiji. Ni nini sasa kauli ya Serikali juu ya upatikanaji wa maji safi na salama ndani ya mita 400 kama ilivyo kwenye sera? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda nimpongeze dada yangu Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, kwa namna ya kipekee anavyowapigania wananchi wake wa Mkoa a Pwani na wananchi wa Rufuji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mpango wa Serikali kuutumia Mto Rufiji, nikubalianenae, kutumia Mto Rufiji kutaweza kuondoa tatizo kabisa la maji katika mji wa Rufiji, lakini kikubwa katika lengo na nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba, inawapatia wananchi wake maji. Si maji tu, ni maji safi, salama na yenye kuwatosheleza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa lengo na mkakati wa Rais wetu ni kuwatua ndoo akinamama kichwani na kwa kuwa hii ni Serikali ya Hapa Kazi Tu, kazi ya kuhakikisha kwamba mtaalamu mshauri kwa ajili mya kufanya upembuzi yakinifu wa/ya Mto Rufiji imeshaanza katika utaratibu. Kwa hiyo, subira yavuta heri, namuomba tusubiri kuhakikisha kwamba, tunatekeleza mradi ule wa Mto Rufiji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili kuhusu suala zima la kuondoa tatizo la majni katika Mji wa Rufiji; ikumbukwe katika Bunge lako Tukufu katika Mji wa Rufiji tumetenga kiasi cha shilingi milioni 630,977,000 kwa ajili ya kuondoa tatizo la maji kwa kipindi hiki wanasubiri katika suala zima la kutumia Mto Rufiji. Ahsante sana.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Kwa muda mrefu chanzo cha maji cha Ruvu Chini na Ruvu Juu kimekuwa chanzo pekee cha maji katika Mkoa wa Pwani. Lakini kimsingi chanzo hicho hakitoshelezi mahitaji na hivyo kushindwa kumaliza tatizo la maji. Je, ni lini Serikali itatumia chanzo cha maji cha Mto Rufiji kuwapatia maji safi na salama wananchi hususan wa Wilaya ya Rufiji, Kibiti, Mkuranga na Kisarawe?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Tatizo la maji lililoko Mkoa wa Pwani linafanana kabisa na tatizo la maji lililopo Jimbo la Ngara ambapo tunapata maji kwa wiki mara moja au mara mbili. Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili la maji katika Wilaya ya Ngara?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, tayari Wizara yangu inatafuta mkandarasi mshauri ambaye ataanza kufanya design ya kutumia maji ya Mto Rubuvu kupeleka Ngara kwa sababu yale maji ni mengi kwa hiyo yatasambaa maeneo mengi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikwambie tu kwamba Serikali, Wizara yangu haijalala tayari inaangalia maeneo yote na kutumia vyanzo vilivyopo kuhakikisha kwamba, wananchi wanapata maji safi na salama.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Kwa muda mrefu chanzo cha maji cha Ruvu Chini na Ruvu Juu kimekuwa chanzo pekee cha maji katika Mkoa wa Pwani. Lakini kimsingi chanzo hicho hakitoshelezi mahitaji na hivyo kushindwa kumaliza tatizo la maji. Je, ni lini Serikali itatumia chanzo cha maji cha Mto Rufiji kuwapatia maji safi na salama wananchi hususan wa Wilaya ya Rufiji, Kibiti, Mkuranga na Kisarawe?

Supplementary Question 3

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mradi wa maji wa Kijiji cha Getamog Wilayani Karatu, uliojengwa katika ule mpango wa Benki ya Dunia ambao uligharimu takribani shilingi milioni 600 haufanyi kazi kwa sababu umejengwa chini ya kiwango. Nimshukuru Waziri wa Maji kwa kutuma wataalam wake ili kubaini tatizo hilo, ili mradi huo uweze kurekebishwa.
Je, ni lini Serikali sasa itapeleka fedha ili wananchi wa Kijiji cha Getamog waendelee kupata huduma hiyo muhimu? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilipata hiyo taarifa na nikamuagiza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Arusha, ambaye ameenda kule kuangalia uchunguzi namna gani mradi ulijengwa chini ya kiwango. Taarifa hiyo ikishapatikana, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba Serikali itafanya maandalizi ya kuweka mkandarasi wa kuboresha ule mradi na fedha itatolewa baada ya kuleta hati za malipo.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Kwa muda mrefu chanzo cha maji cha Ruvu Chini na Ruvu Juu kimekuwa chanzo pekee cha maji katika Mkoa wa Pwani. Lakini kimsingi chanzo hicho hakitoshelezi mahitaji na hivyo kushindwa kumaliza tatizo la maji. Je, ni lini Serikali itatumia chanzo cha maji cha Mto Rufiji kuwapatia maji safi na salama wananchi hususan wa Wilaya ya Rufiji, Kibiti, Mkuranga na Kisarawe?

Supplementary Question 4

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe lina vyanzo vingi sana vya maji, lakini vijiji vyake vingi havina maji. Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Ikuna, Ninga, Kichiwa, Kidegembye, Lupembe, Matembwe, Mtwango na Igongolwa? Ahsante sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kumpongeza. Waheshimiwa Wabunge katika Halmashauri ambazo zimetumia fedha vizuri kwa bajeti ya mwaka 2016/2017 ni pamoja na Halmashauri ya Lupembe, ilitumia fedha zote ambazo zilikuwa zimetengwa na tukawaongezea nyingine. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi hiyo tutahakikisha tunatenga fedha zaidi, ili vijiji vingine vyote vilivyobaki vipate maji.