Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Ukosefu wa nyumba za walimu maeneo ya vijijini husababisha walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa walimu. Aidha, Halmashauri nyingi zikiwemo za Mkoa wa Ruvuma hazina uwezo wa kujenga nyumba za walimu kwa kutumia fedha za ndani. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi vijijini ili kuweka mazingira rafiki ya kufanyia kazi kwa walimu?

Supplementary Question 1

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO:Mheshimiwa Naibu Spika,asante kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi kwamba ukosefu wa makazi bora ya walimu kunawakatisha tamaa walimu kuishi vijijini na mara kwa mara walimu wengi wamependa kuhama kutoka kwenye maeneo haya na kuhamia maeneo ya mijini ambako kuna makazi bora. Ukichukulia Halmashauri moja tu ya Tunduru mahitaji ni nyumba za walimu 1782; upungufu 1688 lakini Naibu waziri amesema ana mpango wa kujenga nyumba 30 katika mkoa mzima wa Ruvuma naona hii kasi ni ndogo nilipenda kujua Serikali ina mkakati gani katika kuhakikisha jambo hili tunalimaliza kwa haraka na ukizingitia sisi wote tumetokana na hao walimu? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu langu la msingi nimeeleza kwamba ni wajibu wetu sisi Serikali Kuu Halmashauri pamoja na wananchi kwa ujumla tukizingatia kwamba upungufu huu ni mkubwa sana haitakuwa busara tukasema tunaiachia Serikali peke yake, tuna wajibu wa kuhakikisha kwamba tunashirikishana ili tatizo hili tulimalizekwa haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, na hii naomba nirejee kwa ruhusa yako jana wakati Mheshimiwa Gekul wakati anaomba Mwongozo kwa Mheshimiwa Spika alisema kwamba kuna barua (Waraka ambao umetolewa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI) ukiwataka wananchi kwamba kuanzia sasa hivi ni wajibu kushiriki kuanzia mwanzo kwa maana ya msingi hadi kwenda kumalizia. Kabla Serikali haijaleta taarifa yake rasmi naomba niseme kwamba hakuna waraka kama huo ambao umepelekwa ni wajibu wetu sisi wananchi pamoja na Serikali kushirikiana ili kumaliza matatizo yanayohusu watumishi wa Serikali.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Ukosefu wa nyumba za walimu maeneo ya vijijini husababisha walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa walimu. Aidha, Halmashauri nyingi zikiwemo za Mkoa wa Ruvuma hazina uwezo wa kujenga nyumba za walimu kwa kutumia fedha za ndani. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi vijijini ili kuweka mazingira rafiki ya kufanyia kazi kwa walimu?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na vyumba na uhaba wa nyumba za walimu limekuwa tatizo kubwa sana na Jimbo langu ni miongoni mwa matatizo ambayo yanawakabili katika shule ya Busongola, Bulamata, Vikonge, Mchangani, Kapanga na Kafishe ambako kuna vyumba viwili tu vya madarasa lakini zipo darasa saba. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na uhaba wa nyumba za walimu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Naibu wangu Mheshimiwa Kandege kwa clarification nzuri kwa maswali yote yaliotangulia.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna changamoto kubwa sana ya vyumba vya madarasa na ndio maana kwa Serikali kipindi hiki cha sasa tulifanya tulitumia takribani shilingi bilioni 21 kuhakikisha tunaongeza vyumba vya madarasa katika shule za sekondari 85 na shule za msingi 19. Lakini hata hivyo kipindi cha muda mfupi uliopita tumetumia takribani shilingi bilioni 16 kufanya uwezeshaji mkubwa katika shule za sekondari 65 na shule za msingi 56 lakini hata hivyo naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge katika fedha tulizozitenga takribani shiling bilioni 246 kwa ajili ya kusaidia kwamba yale maboma yaliyojengwa kuhakikisha tunayakamilisha naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tushirikiane vya kutosha na wizara ya fedha, fedha ziweze kutoka ziende katika halmashauri zetu kwa lengo la kumalizia viporo na kujenga maeneo mengine lengo kubwa wanafunzi wetu wapate mahali pa zuri pa kusomea.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Ukosefu wa nyumba za walimu maeneo ya vijijini husababisha walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa walimu. Aidha, Halmashauri nyingi zikiwemo za Mkoa wa Ruvuma hazina uwezo wa kujenga nyumba za walimu kwa kutumia fedha za ndani. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi vijijini ili kuweka mazingira rafiki ya kufanyia kazi kwa walimu?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi mimi ni kwa namna gani Serikali itoe utaratibu wa jamii, Halmashauri na Serikali Kuu kuweza kuweka nguvu pamoja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu hivi sasa maboma yaliyo mengi katika Halmashauri zetu yamechukua miaka mingi ningeomba basi Mheshimiwa Waziri atume wataalamu kwa baadhi ya maeneo machache ili kunyambulisha ni gharama gani zitakazotumika katika ujenzi wa nyumba hizi za walimu na tuwe na lengo kwa kila Halmashauri kwa zile nyumba ambazo ziko katika lenta ili tuweze kukamilisha kuungana na wananchi. Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kumpongeza Mheshimiwa Issaay nadhani swali lake limejenga katika kujenga suala zima la ushauri na kiufupi kwamba ushauri huu tumeuchukua ndio maana tuliongeza bajeti katika mwaka huu wa fedha kutoka shilingi bilioni 150 npaka kufika shilingi bilioni 246 kwa lengo kubwa kuweza kuhakikisha eneo hilo tunalifanyia kazi. Lakini tunafanya kazi hilo katika maeneo yote sekta ya afya na sekta ya elimu ambapo Mheshimiwa Issaay ndio ulikuwa umejenga hoja ya msingi kipindi cha Bunge lililopita.
Kwa hiyo, naomba niseme tutalichukua hili naamini kwa pamoja tukishirikiana lakini hata hivyo nipende kuwapongeza Wabunge hasa wanaotumia Mfuko wa Jimbo na kwa kushirikiana na maeneo yao ambapo katika tembea yangu nimekuta miradi mingi ambayo Wabunge kupitia Mfuko wa Jimbo wameingiza fedha kuhakikisha nyumba za walimu na madarasa yanafanyika hivyo, kwa hiyo nawapongeza sana kwa hali hiyo.