Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2017-11-17

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-
Ukosefu wa nyumba za walimu maeneo ya vijijini husababisha walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa walimu. Aidha, Halmashauri nyingi zikiwemo za Mkoa wa Ruvuma hazina uwezo wa kujenga nyumba za walimu kwa kutumia fedha za ndani.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi vijijini ili kuweka mazingira rafiki ya kufanyia kazi kwa walimu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Yassin Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa upo upungufu wa nyumba za walimu nchini. Nyumba zilizopo kwa ajili ya walimu wa shule za msingi ni 41,321 wakati mahitaji halisi ni nyumba 222,115 hivyo kuna upungufu wa vyumba 179,794 sawa na asilimia 81. Mkoa wa Ruvuma una upungufu wa nyumba 5,470 za walimu wa shule za msingi.
Mheshmiwa Naibu Spika, Seriakli ina mikakati mbalimbali ya kuboresha utoaji wa elimu Nchini ikiwemo kutenga fedha za ujenzi wa nyumba za walimu. Kwa mwka wa fedha 2017/18 Seriakli imetenga jumla ya shilingi bilioni
• kwa ajili ya uejzi wa nyumba 1,669 za walimu wa shule za msingi nchini. Mkoa wa Ruvuma umetengewa shilingi milioni 470 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 30 za walimu wa shule za msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kuendelea kujenga nyumba za walimu kadri fedha zinavyopatikana kwa lengo la kuboresha mazingira na makazi kwa walimu. Ujenzi wa nyumba za walimu ni jukumu la wadau wote kuanzia Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, wananchi kwa ujumla, hivyo natoa wito kwa wadau wote walimu kuchangia ujenzi wa nyumba za walimu.