Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Sonia Jumaa Magogo
Sex
Female
Party
CUF
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani dhidi ya waajiri ambao hawawaandikishi Watumishi wao katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na kuwasababishia kukosa stahiki zao?
Supplementary Question 1
MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Je, Serikali ina mkakati gani juu ya vijana ambao wamekuwa wakipata ajira za muda mfupi na kushindwa kuendelea na ajira zile, lakini kwa kigezo cha umri wamekuwa wakishindwa kupata mafao yao ambayo yangeweza kuwasaidia katika kuendeleza maisha yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kumekuwa na tofauti ya pensheni za kila mwezi kutoka mfuko mmoja na mwingine. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha wazee hawa wanaostaafu wanapata pensheni iliyo sawa ya kila mwezi na ambayo inaweza kuwasaidia kuendesha maisha yao? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza alikuwa anazungumzia kiujumla kuhusu fao la kujitoa na amewazungumzia vijana ambao bado hawajafikia umri wa kupokea pensheni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumesema awali katika Bunge lako kwamba Serikali inaendelea kulifanyia kazi suala hili la fao la kujitoa. Hivi sasa tupo katika utaratibu wa kushirikiana na wadau ili kutengeneza kwa pamoja mfumo mzuri ambao utawa-cover watu wote katika makundi tofauti tofauti. Hivyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu jambo hili bado linafanyiwa kazi na Serikali tutakuja na mpango mzuri wa kuweza kusaidia kutatua changamoto hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu pensheni, tayari SSRA wameshatoa miongozo kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kulipa kima cha chini cha pensheni sawa kwa mifuko yote na ambayo hivi sasa imeanza kutekelezwa. (Makofi)
Name
Abdallah Ally Mtolea
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Temeke
Primary Question
MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani dhidi ya waajiri ambao hawawaandikishi Watumishi wao katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na kuwasababishia kukosa stahiki zao?
Supplementary Question 2
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika sekta hizi zisizo rasmi na hapa nawalenga hasa wale wanaofanya kazi za daladala kwa maana ya madereva wa madaladala na makondakta wao na hii ni sekta ambayo imeajiri vijana wengi na watu wengi. Kimsingi wana malalamiko mengi ya haki za wafanyakazi, kwamba hawapewi stahiki zao. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, atakuwa tayari kukutana na Madereva na Makondakta wa daladala ili asikilize kero zao na uweze kuzipeleka Serikali kwa ajili ya kuzishughulikia, ukianzia Temeke? (Makofi)
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hii kama Wizara tumekuwa tukiifanya, tutaendelea kuifanya na nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba nipo tayari kukutana nao na kujadiliana nao kuhusu haki ambazo zinawahusu. (Makofi)
Name
George Malima Lubeleje
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpwapwa
Primary Question
MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani dhidi ya waajiri ambao hawawaandikishi Watumishi wao katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na kuwasababishia kukosa stahiki zao?
Supplementary Question 3
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Swali langu ni kwamba, kwa kuwa kuna waajiri ambao wanakata mshahara lakini hawapeleki fedha hizi kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Je, Serikali inawachukulia hatua gani?
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa sheria kila mfanyakazi aliyeandikishwa na anayekatwa makato yake kwa ajili ya hifadhi ya jamii yanapaswa kuwasilishwa katika mfuko husika. Kinyume na kufanya hivyo ni kukiuka taratibu za kisheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana baada ya kuziangalia sheria zetu tukafanya marekebisho ya mwaka 2016 katika Sheria Na. 7 ya Mwaka 2004 ambayo inashughulikia masuala ya Taasisi za Kazi ambapo lengo lake ni ku-compound hizo fences na inapotokea mwajiri amekiuka taratibu hizi tutakachokifanya ni kwenda kumpiga faini ya papo kwa papo ili kufanya deterrence na kumpunguzia mzigo mfanyakazi lakini kumfanya mwajiri awe ana-comply na sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, huo ndiyo mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba jambo hili linafanyika kwa mwajiri kuwasilisha mchango wa mwajiriwa wake ikiwa ni haki yake ya mchango ambao ni sehemu ya mshahara wake.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved