Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 9 | Sitting 6 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu | 68 | 2017-11-14 |
Name
Sonia Jumaa Magogo
Sex
Female
Party
CUF
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani dhidi ya waajiri ambao hawawaandikishi Watumishi wao katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na kuwasababishia kukosa stahiki zao?
Name
Antony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sonia Jumaa Magogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali katika kuhakikisha waajiri wote wanaandikisha wafanyakazi wao kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ni kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii Na. 8 ya Mwaka 2008, Kifungu cha 30 ambacho kimeweka utaratibu unaomtaka mwajiri kuwaandikisha watumishi wake katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Aidha, mwajiri anayekiuka matakwa ya kifungu hiki anastahili adhabu ya kulipa faini ya kiasi kisichozidi shilingi milioni ishirini kwa mujibu wa kifungu cha 55 cha Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuimarisha usimamizi wa Sheria za Kazi, Serikali kupitia Bunge ilifanyia marekebisho ya Sheria ya Taasisi za Kazi Na. 7 ya mwaka 2004 ili kuimarisha mfumo wa kaguzi za kazi mahali pa kazi kwa kuruhusu kutoa adhabu za papo kwa papo kwa waajiri wanaokiuka matakwa ya sheria ikiwa ni pamoja na kutosajili au kuandikisha wafanyakazi katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved