Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Jitihada za wananchi kukaa katika maeneo yaliyopimwa zinakabiliwa na changamoto ya malipo ya shilingi 150,000 ambayo ni kodi ya zimamoto pale wanapotaka kupimiwa ardhi. Je, Serikali ina mpango gani wa kufuta kodi hiyo ili kupunguza ongezeko la makazi holela?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa kibali cha Halmashauri kinatozwa shilingi 16,000, kiwango ambacho ni nafuu, je, zimamoto kutoza 150,000 haioni kwamba kiwango hicho ni kikubwa na hivyo inapelekea wananchi wengi kujenga bila kuwa na kibali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mchanganuo wa tozo kwa mjenzi wa nyumba ya kawaida anatozwa hiyo hiyo shilingi 150,000 sawa na mjenzi wa ghorofa, hii imekaaje?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza ametaka kujua tozo ya shilingi 150,000 kwamba ni kubwa na hivyo inawafanya wananchi washindwe kupata kibali hiki na hivyo kujenga majengo holela. Tozo hizi ni kwa mujibu wa Kanuni na Sheria ambazo tumejiwekea, ukiacha ile Halmashauri ambayo ni shilingi 16,000 anayosema yeye, lakini kwa mujibu wa taratibu ambazo tumejiwekea kwa maana ya Sheria yetu hasa katika Kanuni ile ya [The Fire and Rescue Force, (Fire Precautions in Buildings) Regulations], 2015 Na. 248 imezungumza kiwango ambacho kinapaswa kutozwa ukianzia katika Majiji, Halmashauri, Wilaya lakini vile vile na katika vijiji. Kwa hiyo kiasi kilichowekwa hapa cha shilingi 150,000 ni kwa mujibu wa Sheria yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ametaka kujua kuhusu utofauti wa utozwaji wa tozo hizi. Tozo hizi zinatofautiana kutokana na kiwango cha ukubwa wa jengo au vile vile mita za ujazo wa jengo. Kwa hiyo, haiwezi ikawa kuna mfanano kwa namna ambavyo tozo hizi zimewekwa. Kikubwa kinachoangaliwa hapa ni mita za ujazo. Kwa hiyo, mita za ujazo zinavyozidi kuwa kubwa zaidi ndiyo tozo zenyewe zinazidi kuongezeka.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Jitihada za wananchi kukaa katika maeneo yaliyopimwa zinakabiliwa na changamoto ya malipo ya shilingi 150,000 ambayo ni kodi ya zimamoto pale wanapotaka kupimiwa ardhi. Je, Serikali ina mpango gani wa kufuta kodi hiyo ili kupunguza ongezeko la makazi holela?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na swali la Mheshimiwa Kapufi kuhusiana na hizi kodi za zimamoto, ninachojiuliza na wananchi wanachojiuliza hasa wa Jimbo la Kavuu wanataka kujua, kwa nini hizi tozo zimeanza kutozwa sasa, na watu gani wameshirikishwa? Kwa sababu zinaoneka zimeibuka, hata kama zilikuwepo kwa ujibu wa Sheria, zimeibuka kiasi kwamba hata wale wenye guest houses sasa hivi zimamoto wamekuwa wakiwavamia na kuwa-charge hizi kodi. Kwa hiyo, tunaomba ufafanuzi ni gazeti namba ngapi zilizoruhusu hizi kodi zianze kutumika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ya awali kabisa ni kwamba tozo hizi zinatokana kwa mujibu wa Sheria na Kanuni ambazo tumejiwekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwasababu Mheshimiwa Mbunge ameonyesha interest ya kufahamu namba ya GN ambayo siponayo hapa hiyo namba nitampatia, lakini ni kwamba tozo hizi zinafanyika kwa mujibu wa regulations ambayo niliisema pale awali ya The fire and rescue force fire precaution in buildings regulations ya mwaka 2015. Hivyo kinachofanyika hapa hata ilikuwa ifanyike hapo awali lakini utekelezaji wa Sheria unaendelea kuwa ni halali kwa sababu ilikuwepo Kanuni hii na sasa ndiyo utekelezaji wake unafanyika.