Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 62 2017-11-13

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-
Jitihada za wananchi kukaa katika maeneo yaliyopimwa zinakabiliwa na changamoto ya malipo ya shilingi 150,000 ambayo ni kodi ya zimamoto pale wanapotaka kupimiwa ardhi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kufuta kodi hiyo ili kupunguza ongezeko la makazi holela?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linafanya ukaguzi kwa mujibu wa Sheria Namba 14 Sura Na. 427 (Fire and Rescue Force Act) ya mwaka 2007 kupitaia kanuni zake za ukaguzi na vyeti ya mwaka 2008 ikisomwa pamoja na ya mwaka 2014 [Fire and Rescue Force; (Safety Inspections, Certificate and Fire Levy) Regulalations] za mwaka 2008 na mwaka 2014.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni za Ukaguzi za mwaka 2014 (Fire Levy Category No. 58) kanuni inaelekeza kutozwa tozo ya usomaji na ushauri wa michoro au ramani za majengo. Aidha, kwa mujibu wa Kanuni ya Majengo ya mwaka 2005 [The Fire and Rescue Force, (Fire Precautions in Buildings) Regulations], 2015 Na. 248 Jeshi la zima moto na Ukoaji limekuwa likishiriana na Halmashauri za Miji, Manispaa na Majiji kukagua ramani za ujenzi ili kuhakikisha kuwa nyumba zinajengwa kwa kuzingatia tahadhari na kinga dhidi ya moto na majanga mengine. Kupitia ushauri huu Jeshi la zimamoto na uokoaji hutoza tozo ambapo kiasi cha tozo huzingatia aina ya ramani iliyowasilishwa na kukaguliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia umuhimu wa ujenzi unaozingatia tahadhari na kinga dhidi moto, Serikali haikusudii kufuta tozo hii kwa sasa. Aidha, Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na uokoaji inawaasa Wananchi kwa kujenga nyumba zao kwa kufuata Sheria na Kanuni zinazosimamia mipango miji ili kuwa na miji salama hivyo kupunguza athari zitokanazo na moto na majanga mbalimbali na kuwezesha utoaji wa huduma za kijamii kwa urahisi zaidi.