Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Wilaya za Kakonko, Buhigwe na Uvinza ni Wilaya mpya ambazo hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Kakonko kwa sasa wanapata huduma katika Kituo cha Afya cha Kakonko na kituo hicho kimezidiwa kwa sababu msongamano wa watu ni mkubwa. Kituo hicho kinahudumia wananchi kutoka hadi Mkoa jirani wa Kagera kwa maana ya wananchi wa Nyakanazi, Kalenge pia na wakimbizi kwa sababu katika Wilaya ile kuna kambi za wakimbizi, Waziri amesema kwamba mwaka 2017/2018 zimetengwa shilingi milioni 500.
Je, Waziri yupo tayari sasa kutokana na jinsi wananchi wanavyopata shida pamoja na waganga na wauguzi kwa sababu watu wakiwa wengi waganga nao wanachanganyikiwa, yupo tayari kufuatilia hizo shilingi milioni 500 ziweze kwenda mara moja Kakonko kwenda kuwasaidia wananchi? (Makofi)
Swali la pili; kwa wakati huu ambapo Wilaya ya Uvinza haina Hospitali ya Wilaya, wananchi wanapata huduma katika vituo vya afya na zahanati, lakini vituo hivyo vya afya pamoja na zahanati havina watumishi wa kutosha.
Je, katika mgao huu wa wafanyakazi ambao wataajiriwa kwa sasa, Serikali iko tayari kabisa kupeleka watumishi wengi wa kutosha kwenda kusaidia katika Wilaya ya Uvinza ambayo haina Hospitali ya Wilaya? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Genzabuke kwa jinsi ambavyo anafuatilia huduma hasa kwa wanawake katika Mkoa wa Kigoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza, napenda kumthibitishia kwamba fedha hizo ambazo zimetengwa kwenye bajeti ya 2017/2018 nitazifuatilia na kuzisimimamia mimi mwenyewe binafsi kuhakikisha kwamba zimekwenda haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili, wiki hii iliyopita tumekamilisha upatikanaji wa watumishi 2,008 ambao sasa hivi wanaendelea kugawanywa katika Halmashauri mbalimbali. Leo hii nitahakikisha kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza imepata watumishi wa kutosha angalau kwa mahitaji ya asilimia 50. (Makofi)

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Wilaya za Kakonko, Buhigwe na Uvinza ni Wilaya mpya ambazo hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe
ni moja ya Halmashauri ambayo haina Hospitali ya Wilaya na tuna vituo vya afya vinne, kituo cha afya kimoja cha Lupembe ni cha zamani, hivi karibuni tumefungua chumba cha upasuaji tayari operation zinaendelea pale. Tuna Kituo cha Kichiwa ambacho tunatarajia pia tuwe na theater ili kuwahudumia akina mama wasitembee umbali mrefu kwenda Kibena.
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kujenga au kuanzisha chumba cha upasuaji ili akina Mama katika Kituo cha Afya cha Kichiwa ili akina Mama wasisafiri umbali mrefu kwenda hospitali ya Kibena ambayo ipo mbali sana na wanapoishi ambapo Jimbo la Lupembe lipo. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA
NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kituo cha afya cha Kichiwa kumbukumbu zangu katika programu yetu ya vile vituo vya afya vya kwanza 172, katika vituo vile kuna fedha ambazo tulipata kutoka Canada, fedha zile zimeshaendelea katika maeneo mbalimbali na baadhi ya vituo sasa hivi wameshafika level ya renta, lakini kuna zile fedha kutoka World Bank ni kwamba upelekaji wake wa fedha utakamilika ndani ya wiki hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba wananchi wako watarajie kwamba jinsi gani waweze kushiriki kazi lakini fedha zile tutatumia force account. Niwasihi hasa viongozi wetu huko katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, zile fedha zinapokuja lazima wazisimamie vizuri tupate value or money na wananchi waweze kupata huduma. (Makofi)

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Wilaya za Kakonko, Buhigwe na Uvinza ni Wilaya mpya ambazo hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Halmashauri ya Kibiti ni Halmashauri moja ambayo imetoka Wilaya ya Kibiti na kituo chake kikubwa cha afya Kibiti lakini hivi sasa kimezidiwa kutoa huduma.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Hospitali
ya Wilaya ya Kibiti? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hoja anayoizungumza Mheshimiwa Ungando ni hoja ya kweli na kwa sababu nilikuwa naye katika vile visiwa 40 vya Delta kwa kutwa nzima na changamoto ya afya kule ni kubwa sana, ndiyo maana katika kipindi cha sasa tumepeleka fedha katika kituo cha afya kimoja ambacho mimi na Mheshimiwa Mbunge tulizunguka mpaka usiku pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala zima la progamu ya uanzishaji wa Hospitali ya Wilaya ya Kibiti, naomba nikusihi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutashirikiana kwa pamoja kwa sababu lengo letu kubwa zile Wilaya zote zilizokosa hospitali sasa tuweze kuwa na progamu maalum kwa ajili ya kujenga hospitali. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ungando naomba nikupe faraja kwamba tutashirikiana kwa pamoja tuangalie way forward tunafanyaje tupate Hospitali ya Wilaya ya Kibiti kwa sababu population ya watu pale ni kubwa hasa ukiangalia barabara ya Kilwa lazima tuhakikishe kwamba tunafanya jambo hilo kwa haraka. (Makofi)

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Wilaya za Kakonko, Buhigwe na Uvinza ni Wilaya mpya ambazo hazina Hospitali za Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 4

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza.
Kwa vile matatizo haya ya afya katika Wilaya ya Kakonko yanafanana sana na ukosefu wa Hospitali ya Wilaya ya Uyui na Wilaya ya Uyui tumejitahidi kupitia Halmashauri kujenga hospitali lakini tumeishia kwenye OPD na tungeomba Serikali ituambie; je, inaweza kutuongezea hela ili tuweze kumalizia OPD yetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli pale hawana Hospitali ya Wilaya na wameanza programu ya ujenzi wa OPD, lakini sasa hivi tunafanya needs assessment katika maeneo yote ambayo majengo yalianza bado hayajakamilika. Ndiyo maana katika harakati zetu sasa hivi tunakamilisha Kilolo, Mvomero lakini tunaenda kule Siha ninaamini kwamba Uyui. Naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato tunaofanya hivi sasa na wataalam wangu pale ofisini tutaangalia nini tufanye, lengo kubwa tuikamilishe hospitali yetu ya Uyui na wale Wanyamwezi wa Tabora pale waweze kupata huduma kama Wanyamwezi wengine hapa Tanzania. (Makofi)