Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2017-11-10

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Wilaya za Kakonko, Buhigwe na Uvinza ni Wilaya mpya ambazo hazina Hospitali za Wilaya.
Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko imeidhinishiwa jumla ya shilingi milioni 500 kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Ujenzi wa hospitali hiyo unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 1.5 hadi kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza imetenga eneo la ekari 80 na imekamilisha michoro ya jengo la Hospitali ya Wilaya. Halmashauri imeshauriwa kuweka kipaumbele na kutenga bajeti katika mwaka wa fedha 2018/2019 ili kuanza ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe inaendelea na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya kwa kuanza na jengo la wagonjwa wa nje, utawala na maabara unaogharibu shilingi milioni 450. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imetengewa shilingi milioni 500 kuendelea na ujenzi. Kazi hii inatekelezwa na SUMA JKT na kazi inaendelea. Ujenzi wa hospitali unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha na unakadiriwa kugharimu shilingi bilioni 6.4 hadi kukamilika.